Je, ni sahihi kumhurumia Mbatia kwa yanayomkuta!? Je anahitaji msaada na public sympathy?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,845
Huruma ya jumuiya ndani ya jamii kuna watu automatically inawakataa, ama inawasuta kama si kuwabeza! Mwenyekiti wa chama cha upinzani aliyeondolewa madarakani ni mmojawapo!

Harakati za mageuzi Tanzania, kumbukumbu na historia yake tangu kuasisiwa 1992, vinaweza kumuangalia kwa makengeza, ama kumtazama kwa jicho chongo kama si kumuona kwa upofu kwa yale yote aliyoutendea upinzani Tanzania na harakati zake

Akiwa na sura mbili na ngozi ya kinyonga, uhalisia wake nyuma ya pazia ulianza kujionesha hadharani mara baada ya uchaguzi mkuu wa 1995 kwenye kikao kilichofanyika hotel ya Mkonge Tanga, wakati huo NCCR-Mageuzi chini ya mrema kikiwa ndio chama maarufu kilichoitikisa vilivyo CCM...

Mwamko wa mageuzi kipindi hicho ndio ulikuwa unajengeka na ufunguo wa motokari ya kukubalika wakakabidhiwa NCCR.. Matumaini ya wananchi waliokuwa wamechoshwa na CCM yote yakahamia NCCR! Lakini kilichotokea pale Tanga Mkonge hotel kiliwaumiza wengi na kuacha doa kubwa jeusi kwenye harakati za mageuzi nchini..!

NCCR ilifitinishwa, ikachonganishwa na kugombanishwa! Na viongozi wakiwa wamepenyezewa mamluki wakakubali kugombanishwa na kufarakana vibaya mno! Ilikuwa ni aibu kubwa kwakuwa ngumi na ugomvi wa kurushiana vitu. Meza nk vilitumika! Uharibifu mkubwa na majeruhi vikatokea! NCCR - Mageuzi chama kilichokuwa tumaini la wengi kikameguka mapande mawili makubwa na mengine madogo madogo

NCCR ya James Mbatia ndio hii iliyodumu mpaka leo hii lakini kikiwa kama joka la kibisa ama umbwa kibogoyo! Mambo yake mengi yalikuwa meusi huku kikiwa kimejaa mashaka kutokana na kuwa kigeugeu ama kuwazunguka wenzake kila nyakati za chaguzi zilipokaribia

Mifano ni mingi kwenye hili tena ya wazi kabisa, na kwenye hayo mambo yote meusi ya kuhujumu upinzani yalipokuwa yakitokea JM alikuwa na mkono wake ama alikuwa ndio kinara mkuu wa michezo ovu

Uchaguzi wa 2015 ulidhihirisha rangi zake kamili, chama kikazidi kupoteza mvuto na kuthibitisha mashaka ya wengi kwamba kiko upinzani kwa ajili ya kuua upinzani wenye nguvu

Dhambi ya usaliti huwa haifi mpaka kiama! Bali humea,hukua na kuzaana! Inapotunga mimba na kupata familia ambayo baadae hugeuka ukoo, hicho kizalia ndio kinakuja kuwa adui wako wa kukumaliza.. Daima kikulacho ki nguoni mwako!

Kutumika hakujaanza leo lakini daima hakuwi na mwisho mwema! JM na chama chake wana madoa mabaya kwenye mabango ya harakati za mageuzi ya kisiasa nchini.. Mwisho wa kutumika ni kuachwa kwa aibu kama usipotii wanavyotaka wao! Ama ukitaka zaidi, ama ukienda nao kinyume!

Sioni haja ya kumhurumia labda tu kwa unafiki wa kawaida wa kibinadamu.. Hii ni asili inachukua mkondo wake! ISIZUIWE MAANA HAIZUILIKI!

Wengine wajiandae asili inakaribia kubisha hodi malangoni mwao! Bado kitambo kidogo tuu.. Najua KZ na HL wananisoma na kunielewa vema! Hii ni asili na asili ni KARMA! Pole JM...!
 
veiled-chameleon-24044174.jpg
 
Sasa hujaeleza Mbatia alifanyaje kwenye kusambaratisha chama..Maana hata Mrema nae hakua mtu.

Na huo uchaguzi wa 2015 Mbatia alifanya usaliti gani hadi unasema rangi zake zilidhihirika?
Maana alijiunga na UKAWA na akawa nao hadi uchaguzi ukaisha, tofauti na Zito na Lipumba
 
Kweli hakuna haja ya huruma kwa Mbatia kwa kujiingiza japo kidogo katika usaliti.
Hawa watu ndio wamesababisha upinzani kutokufanikisha malengo kwa takribani miaka yote 30 tokea sheria ya vyama vingi ipitishwe.
Kuna watu wameumia, kufungwa, kufilisiwa na wengine wameponea mkono wa Mungu na wanatembea na risasi mwilini huku wasaliti wakilambishwa sukari na kusaliti wapambanaji wa kweli.
Na salama yao ni Watz kuwa vile alivyo sema marehemu Jomo Kenyattq kwa Mwalimu, vinginevyo nchi zingine maisha yao yangekuwa magumu mno mtaani
 
Kweli hakuna haja ya huruma kwa Mbatia kwa kujiingiza japo kidogo katika usaliti.
Hawa watu ndio wamesababisha upinzani kutokufanikisha malengo kwa takribani miaka yote 30 tokea sheria ya vyama vingi ipitishwe.
Kuna watu wameumia, kufungwa, kufilisiwa na wengine wameponea mkono wa Mungu na wanatembea na risasi mwilini huku wasaliti wakilambishwa sukari na kusaliti wapambanaji wa kweli.
Na salama yao ni Watz kuwa vile alivyo sema marehemu Jomo Kenyattq kwa Mwalimu, vinginevyo nchi zingine maisha yao yangekuwa magumu mno mtaani
Kuna watu wameumia, kufungwa, kufilisiwa na wengine wameponea mkono wa Mungu na wanatembea na risasi mwilini huku wasaliti wakilambishwa sukari na kusaliti wapambanaji wa kweli....
 
Sasa hujaeleza Mbatia alifanyaje kwenye kusambaratisha chama..Maana hata Mrema nae hakua mtu.

Na huo uchaguzi wa 2015 Mbatia alifanya usaliti gani hadi unasema rangi zake zilidhihirika?
Maana alijiunga na UKAWA na akawa nao hadi uchaguzi ukaisha, tofauti na Zito na Lipumba
Aliuza siri za UKAWA na baada ya hapo akazawadiwa ubunge na mwanakwenda
 
Huruma ya jumuiya ndani ya jamii kuna watu automatically inawakataa, ama inawasuta kama si kuwabeza! Mwenyekiti wa chama cha upinzani aliyeondolewa madarakani ni mmojawapo!

Harakati za mageuzi Tanzania, kumbukumbu na historia yake tangu kuasisiwa 1992, vinaweza kumuangalia kwa makengeza, ama kumtazama kwa jicho chongo kama si kumuona kwa upofu kwa yale yote aliyoutendea upinzani Tanzania na harakati zake

Akiwa na sura mbili na ngozi ya kinyonga, uhalisia wake nyuma ya pazia ulianza kujionesha hadharani mara baada ya uchaguzi mkuu wa 1995 kwenye kikao kilichofanyika hotel ya Mkonge Tanga, wakati huo NCCR-Mageuzi chini ya mrema kikiwa ndio chama maarufu kilichoitikisa vilivyo CCM...

Mwamko wa mageuzi kipindi hicho ndio ulikuwa unajengeka na ufunguo wa motokari ya kukubalika wakakabidhiwa NCCR.. Matumaini ya wananchi waliokuwa wamechoshwa na CCM yote yakahamia NCCR! Lakini kilichotokea pale Tanga Mkonge hotel kiliwaumiza wengi na kuacha doa kubwa jeusi kwenye harakati za mageuzi nchini..!

NCCR ilifitinishwa, ikachonganishwa na kugombanishwa! Na viongozi wakiwa wamepenyezewa mamluki wakakubali kugombanishwa na kufarakana vibaya mno! Ilikuwa ni aibu kubwa kwakuwa ngumi na ugomvi wa kurushiana vitu. Meza nk vilitumika! Uharibifu mkubwa na majeruhi vikatokea! NCCR - Mageuzi chama kilichokuwa tumaini la wengi kikameguka mapande mawili makubwa na mengine madogo madogo

NCCR ya James Mbatia ndio hii iliyodumu mpaka leo hii lakini kikiwa kama joka la kibisa ama umbwa kibogoyo! Mambo yake mengi yalikuwa meusi huku kikiwa kimejaa mashaka kutokana na kuwa kigeugeu ama kuwazunguka wenzake kila nyakati za chaguzi zilipokaribia

Mifano ni mingi kwenye hili tena ya wazi kabisa, na kwenye hayo mambo yote meusi ya kuhujumu upinzani yalipokuwa yakitokea JM alikuwa na mkono wake ama alikuwa ndio kinara mkuu wa michezo ovu

Uchaguzi wa 2015 ulidhihirisha rangi zake kamili, chama kikazidi kupoteza mvuto na kuthibitisha mashaka ya wengi kwamba kiko upinzani kwa ajili ya kuua upinzani wenye nguvu

Dhambi ya usaliti huwa haifi mpaka kiama! Bali humea,hukua na kuzaana! Inapotunga mimba na kupata familia ambayo baadae hugeuka ukoo, hicho kizalia ndio kinakuja kuwa adui wako wa kukumaliza.. Daima kikulacho ki nguoni mwako!

Kutumika hakujaanza leo lakini daima hakuwi na mwisho mwema! JM na chama chake wana madoa mabaya kwenye mabango ya harakati za mageuzi ya kisiasa nchini.. Mwisho wa kutumika ni kuachwa kwa aibu kama usipotii wanavyotaka wao! Ama ukitaka zaidi, ama ukienda nao kinyume!

Sioni haja ya kumhurumia labda tu kwa unafiki wa kawaida wa kibinadamu.. Hii ni asili inachukua mkondo wake! ISIZUIWE MAANA HAIZUILIKI!

Wengine wajiandae asili inakaribia kubisha hodi malangoni mwao! Bado kitambo kidogo tuu.. Najua KZ na HL wananisoma na kunielewa vema! Hii ni asili na asili ni KARMA! Pole JM...!
andiko zuri nilikuwa sijui kama JM alikuwa vile huko nyuma ulikokusema. This is new news to me!
 
Back
Top Bottom