OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 457
- 773
Kauli ya kusema kuwa watu wa nje tunawahitaji kuliko wanavyotuhitaji imetamkwa kwa zaidi ya mara moja na Rais Samia Suluhu. Kauli hii inashida kidogo na tunahaja ya kuhakiki kama ni kweli kuwa tunawahitaji kuliko wanavyotuhitaji
Ili kuangalia namna tunahitajiana ni muhimu kwanza kuangalia vitu ambavyo sisi tunafaidi kutoka kwao ukilinganisha na vitu wanavyofaidi kutoka kwetu. Mataifa yaliyoendelea yana rasilimali fedha na teknolojia, huku taifa kama Tanzania likiwa na mazingira mazuri ya biashara, cheap labour, madini, gesi, mbuga za asili, wanyama nk. Eeekh! Hadi hapo tunaweza sema tunavyo vingi ambavyo wao wanavihitaji huku sisi tukihitaji fedha tu kutoka kwao kwa kuwa suala la teknolojia hatuna muda nalo(Lingekuwepo suala la Leap frogging kwenye uchumi lingetokea zamani sana)
Hivyo basi nadhani kauli sahihi kusema ni kuwa tunahitaji fedha zao. Lakini hata kama tunasema tunahitaji fedha zao tusisahau maneno ya Rais Nyerere kwenye azimio la Arusha kuwa anayeweka hela ndio anayechagua wimbo, ambapo alipinga suala la kutegemea fedha za nje na kuweka kuwa ili tuendelee hatuhitaji hela bali tunahitaji watu, ardhi, siasa safi, uongozi bora
Kauli ya Rais Samia inaonesha kuwa kwa sasa sisi tunahitaji fedha, and only money, sio watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora kama ambavyo misingi ya maendeleo inahitaji.
Fikra hizi ndio zinafanya tukose hata nguvu ya kubargain katika masuala ya kimataifa kisha kupata hasara za kudumu na resource curse mbali na kuwa na vitu vingi ambavyo wao wanavihitaji na tungeweza kuvitumia kujipatia faida
Signed
OEDIPUS
Ili kuangalia namna tunahitajiana ni muhimu kwanza kuangalia vitu ambavyo sisi tunafaidi kutoka kwao ukilinganisha na vitu wanavyofaidi kutoka kwetu. Mataifa yaliyoendelea yana rasilimali fedha na teknolojia, huku taifa kama Tanzania likiwa na mazingira mazuri ya biashara, cheap labour, madini, gesi, mbuga za asili, wanyama nk. Eeekh! Hadi hapo tunaweza sema tunavyo vingi ambavyo wao wanavihitaji huku sisi tukihitaji fedha tu kutoka kwao kwa kuwa suala la teknolojia hatuna muda nalo(Lingekuwepo suala la Leap frogging kwenye uchumi lingetokea zamani sana)
Hivyo basi nadhani kauli sahihi kusema ni kuwa tunahitaji fedha zao. Lakini hata kama tunasema tunahitaji fedha zao tusisahau maneno ya Rais Nyerere kwenye azimio la Arusha kuwa anayeweka hela ndio anayechagua wimbo, ambapo alipinga suala la kutegemea fedha za nje na kuweka kuwa ili tuendelee hatuhitaji hela bali tunahitaji watu, ardhi, siasa safi, uongozi bora
Kauli ya Rais Samia inaonesha kuwa kwa sasa sisi tunahitaji fedha, and only money, sio watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora kama ambavyo misingi ya maendeleo inahitaji.
Fikra hizi ndio zinafanya tukose hata nguvu ya kubargain katika masuala ya kimataifa kisha kupata hasara za kudumu na resource curse mbali na kuwa na vitu vingi ambavyo wao wanavihitaji na tungeweza kuvitumia kujipatia faida
Signed
OEDIPUS