Je, ni kweli maisha hayana formula?

Je, ni kweli maisha hayana formula?

Eeehe , na hivi Mshana na thread zake za uchawi humu Jf unaeza ukatufanya tukaamini hili ujue...
Usinielewe vibaya mtaalamu. Hapa unaongelea jinsi unavyopigwa na baridi na hatari zote za usiku wakati ukiwa katika mambo yako ya kishirikina na matunguli? Nimesoma hiyo sentensi moja kwa moja wazo likanijia nikakuona kabisa laivu ukisafiri kwa ungo usiku kutoka Upareni kwenda DRC kupeleka ripoti. Pole sana mkuu. Ndo maisha ati!
 
Your right Manuu, Mimi nadhani katika maisha kila mtu alizaliwa na bahati yake! Ndiyo maana tunatofautiana
Bado naamini maisha hayana formula kabisa kwa sababu watu wawili wanaweza kupita katika njia za kufanana sana chukulia mfumo wa elimu mmeanza wote toka primary mpaka chuo na mmesoma course moja na uelewa wenu ukawa unashabiiana sana katika matokeo ya darasani mkamaliza wote lakini kuja kwenye mafanikio ya kimaisha mkaja kuwa tofauti sana mwenzako akapata kazi mapema tena shirika linalopita sana wewe ukaja pata kazi miaka 4 ijayo tena kwa robo ya mshahara wa yule mwenzako na hii ipo sana ...So kama maisha yangekuwa na formula watu hawa wawili sababu wametumia njia moja ilibidi wote wapate majina sawa katika maisha lakini kwa mfano huo tu umeona walivyotofautiana...
 
Kila kitu duniani kina sheria zake za asili. Nyota na sayari zinatii sheria na kanuni zake za mizunguko. Mm inatengeneza chakula chake kwa kuzingatia kanuni, wanyama wanazaliana kwa kuzingatia kanuni za asali nk nk, hivyo hata mafanikio maishani yana kanuni zake za asili.
 
Maisha hayana kanuni/formula. Hilo kiko wazi.

Hoja kwamba yangekua hayana kanuni basi tusingeenda shuke nk nk haina mashiko. Tunaenda shule ili kupata ufahamu wa mambo na kuongeza uelewa ili kutatua changamoto zinazotukabili.

Maisha hayana kanuni kwa maana kwamba hakuna njia au utaratibu ulionyooka unaotakiwa kufuatwa na kila mtu ili kufikia mafanikio anayoyataka. Ingekua hivyo kila mtu angetumia au angefuata njia aliyopitia bill gates kupata utajiri ili kila mtu awe tajiri.

Ili kufikia mafanikio ya kila mtu duniani kila mtu huoitia anakopitia, sio lazima ufuate njia aliyofuata mwenzako ukafanikiwa kama yeye.

Maisha bado yanabaki kua hayana kanuni. Kusema maisha yana kanuni/au utaratibu flani ili kila mtu aufuate tuambie huo ni utaratibu gani.
 
Maisha hayana formula kabisa, ndio maana kuna watu wanatumia pesa sana na bado maisha yao yapo vizuri kuliko mtu mbahili hapa nimetolea mfano watu wenye kufanya kazi moja.

Kuna msemo usemao tumia pesa ikuzoee. Huu msemo una maana kubwa sana japokuwa watu huutumia kama kukejeli. Ilikupata pesa nyingi zaidi shariti utumie nguvu, akili na pesa kupata pesa.
TUMIA PESA KUPATA PESA.
Sina hakika kama nimetoka nje ya mada kwa kujikita zaidi katika pesa kwani tafsiri ya neno mafanikio ni pana. Binafsi huwa na judge mafanikio kwa kiwango cha fedha au thaman za vitu mtu alivyonavyo.
 
Duuh ndugu yangu umenikumbusha mbali mno nakumbuka miaka ya themanini,niliifanya hiyo kazi Sweden nusura nikiue kibb cha kizungu,ile naweka gazei mlangoni kwake alfajiri na chenyewe kinafungua mlango, tukakutana uso kwa uso,na vile nilivyo mweusi kibibi kikajua ni gorilla, kikaanguka na kuzimia.

LOL!
 
Maisha hayana fomula na wala huwezi kuyatabiri, Maisha unaweza ukayapatia miaka 20 wa 21 ukaanguka na ukaweza kurudi kama ndio unaanza sasa maisha. kama yangekua na fomula ilikwenda wapi?

Maisha ni utaratibu wa Mungu mwenyewe alivopanga leo anampandisha huyu kesho anamshusha mwingine. Wenye uwezo na mali zao wanaishia jela hiyo fomula si wangeitumia ili wanusurike kwenda jela? Miaha hayana mjanja, utakua mjanja pale unapoyapatia tuu lakini ukianza kushuka hujui jinsi gani ya kuyarejesha katika hali yake ya kawaida.
 
Katika ulimwengu huu uliojaa mahangaiko na machungu watu tunazaliwa tukiwa hatuna ufahamu wowote wala kuelewa mambo ya mbele zaidi ya kutabili namna mambo yatakavyokuwa.....ndio maana kwenye masuala ya kutafuta ridhki haishangazi kumuona mtu aliyetumia miaka mingi kusomea masuala ya sheria anakuja kuwa mfanyabiashara maarufu......
Kwa kifupi ni kuwa maisha ni vita vinavyohitaji jitihada na maarifa ili kuweza kuvishinda na hatimaye kuyaona mafanikio.....lakini jitihada zetu na maarifa yetu havitafaa kitu bila ya kumtegemea muumba na kumtumainia yeye kwani yeye ndiye mtoaji na RIDHKI na humpa amtakaye kwa muda anaoona unafaa......wapo watu waliokuwa mafukara lakini neema zimewaangukia sasa hivi wanaogelea katika fedha.....ili hali kuna watu kibao nyuma ya pazia bado wanapambana na muda unazidi kwenda.......
Watu wenye vipaji kama alichonacho Diamond ni wengi sana mitaani na kila uchao wanajitahidi kwa kadri ya uwezo wao ili kufikia alipofikia huyo msanii lakini jitihada zinashindikana.....
Wapo watu walianza biashara pamoja na watu fulani lakini leo hii wenzao wakipiga hatua huku wao bado wakiendelea kusua sua kwenye biashara hiyo hiyo....

Kitu kimoja kikubwa kinachokosewa na vijana au tuseme kuwa wachakarikaji wa miaka hii ni kutafuta maisha au ridhiki kwa nia au kujiringanisha na fulani au nimpite fulani.....hiyo ni mbaya kwani kamwe hutakuja kuyaona wala kuyafurahia mafanikio yako kwani maisha hayataki haraka wala pupa...bali yanataka uvumilivu na busara za hali ya juu......huwezi kujua kuwa huyo unayetaka kuwa kama yeye imemchukua miaka mingapi hadi kufikia hapo alipo sasa na je upo tayari kupita njia hizo ili nawe ufike hapo.....!!!???
Stori na sifa huvuma baada ya mafanikio kuja lakini nyuma ya hayo mafanikio kumejaa vita kubwa sana hadi kufikia hapo....??

Usitafute maisha kwa kushindana na fulani bali jiwekee malengo yako na mikakati yako na upambane kwa uwezo wako wote ili kufanikisha mipango yako huku ukiwa na ndoto zenye kutekelezeka.......pia tujifunze kushukuru hata kile kidogo tulichojaaliwa.......
Safi sana, hata mimi naamini maisha hayana kanuni hizo kanuni zingekuwepo kila mtu angezifuata ili awe tajiri, maisha hupangwa na MUNGU. Nyote mnaweza kuwa mnauza mitumba mwenzako akatoka kimaisha wewe ukashindwa kutoka ukaja kutokea sehemu nyingine. Hiyo ndo dhana ya maisha hayana formula. GOD HELPS WHO HELP THEMSELVES.
 
Unakesha njecgizani kwenye baridi ukifanya nini? Umenikumbusha kazi ya kugawa magazeti majumbani saa saba usiku hadi saa 12 alfajiri (aftenposten) niliyoifanya miaka ya 2012/13 nchi flani ulaya. Unapanda ngazi hadi ghorofa ya 8 kwa miguu kwa masaa 2.30, unasukuma toroli kipindi cha winter unateleza kwenye barafu, mvua , baridi vyote vyako.
Toroli limejaa magazeti kazi ya kusukuma sasa uwe umeshiba kweli....

Hopefully ulirudi bongoland na something tangible after all that hustling....
 
Nasikia wewe ni Gentamycine.. Kwanini unakua na account nyingi Jf?
Mpotezee aliita reply zetu zisizo na maana matokeo yake ule upuuzi wake wote umefutwa pamoja na reply nyingi sana zilizokuwa zimejaa ujinga huku nyingine zilirekebishwa lugha
Angekuwa kaandika vitu vya maana kama anavyojinasibu naamini visingefutwa... hapa ndio unapata kwa usahihi ile tafsiri ya usemi usemao DON'T ARGUE WITH A FOOL...
 
Back
Top Bottom