Drama ni kk kwa maana ya Korea kusini ambao tulikuwa sawa nao kwa ngazi ya maendeleo miaka ya 1960s ila Leo wao wako first wold na GDP ya juu sana , sisi bado tuko third world na GDP ndogo sana. Walipata kiongozi mwenye vision akaongoza kwa miaka 30 ndiye aliwafikisha hapo ila aliwanyima Uhuru wa kutoa maoni hakukuwa na demokrasia hata kidogo.
Baada ya kustaafu akasema anajutia kuwanyima wananchi Uhuru Wa kutoa maoni ingawa baada yake Korea kusini kuna demokrasia ya hali ya juu. Hats rais anaweza kushitakiwa akifanya madudu. Lakini mbona nchi nyingi hazina democrasia lakini kimaendeleo zinachechemea .wao ni mabepari.
Sasa ukienda Korea kaskazini wao ni wajamaa hadi Leo ila maendeleo yao ni shida .Kaskazini anatawala yule Kijana mkorofi baada ya kurithishwa toka kwa babu na baba .laiti kuongoza muda mrefu ingekuwa ndio maendeleo basi kaskazini wangekuwa zaidi ya kusini maana maana tangu 1950s wanatawala ukoo Wa KIM IL SUNG babu, KIM JONG IL Mtoto , na sasa ni KIM JONG UN mjukuu, Mambo yao ni ovyo.
Wanatengeneza zana za nuclear nja kila mwaka kwao ,pia wanashindwa hata kuwatibu wananchi minyoo ya tumboni. Hayo maendeleo ya vitu sio watu. Lakini kusini hawajishughulishi na nuclear . kusini ndio wana makampuni yanayotamba dunia nzima mfano SAMSUNG, DAEWOO ,KIA MOTORS NK. Korea zote zina somo kwa viongozi Wa Leo Afrika wanaotaka kuwaletea wananchi wao maendeleo halisi , sio maendeleo ya vitu. Kamchango hako kadogo kwa waliozaliwa hawajafikisha miaka 30.
Kiongozi aliyeiendeleza kusini ni LEE KUAN YEW kama sijakoea . Mwenye interest atagoogle amjue zaidi, lakini alikuwa dictator per se, Ndiyo benovelent dictator (dictator mwema anayeendeleza nchi) ? Asanteni.pia nimalizie kaskazini ni watoto pendwa wa Russia na China , wakati kusini ni watoto pendwa Wa marekani tangu cold war hadi leo. Bila hao yule dogo hawezi kukohoa kwa Marekani.
Ndiyondiyoyoy6ana Trump anaibana China kwa biashara na China ameanza kumbana dogo apunguze jeuri Tukumbuke Marekani ndiyo mteja mkubwa kwa biashara za China. Mpaka kiongozi Wa China akalalamika eti anaonewa akiwekwa vikwazo kwa makosa ya dogo.
Unajua bado Marekani bado anafurukuta ingawa Siku zake za ubabe ni chache mbeleni, kama China hatakwaa kisiki miaka kumi au ishirini ijayo.