Mkuu nimekupata vizuri lakini kuna kitu bado kinanichanganya. Eneo la uvutano la dunia linaishia EXOSPHERE ambayo ni Km 400 kutoka uso wa dunia. Sasa inakuwaje mwezi ambao uko yapata Km laki nne (nje ya nguvu za uvutano) hatuuachi dunia inapozunguka jua?
Tambua kuwa ukiwa nje ya anga la dunia(exosphere) ni kweli ni vigumu kudetect nguvu za uvutano za dunia(gravity) sio kwa sababu hazipo bali kwa kuwa ni too weak to be detected.
Kuna kitu ambacho tunapaswa kukijua, ni kwamba nguvu za uvutano za maumbo ya angani kama jua, dunia,mwezi, nk zinatend kuvuta zaidi vitu vikubwa kama sayari, mwezi,nk.
Kwa hiyo nje ya exosphere kitu kama binadamu au space rocket vinakuwa vidogo mno kuweza kuvutwa au kudetect gravity yoyote ndio maana vitu vidogo angani vinasafiri kwa uhuru na kwa speed kubwa katika direction yoyote hadi pale kinapokaribia sayari au mwezi maana hapo gravity inakuwa kubwa na kuweza kubadili velocity na direction ya chombo hicho.
Kwa hyo kwenye anga za juu kuna nguvu za uvutano toka jua(na nyota nyinginezo), sayari,mwezi, nk lakini zinaaffect vitu vikubwa tu angani. Ndio maana wakati rocket inasafiri kwa uhuru na kwa kasi kubwa dunia(na sayari nyingine) haina uhuru huo hivyo inabaki katika mzunguko wake kutokana na nguvu za jua za uvutano.
Na ndio maana kuna uvutano kati ya mwezi na dunia ambao unafanya mwezi ubaki kwenye mzuguko wake ukienda pamoja na dunia.
Bahari zinatoa ushahidi wa uvutano kati ya mwezi na dunia kwani wengi tunajua au kusikia kuhusu bahari kupwa na bahari kujaa. Kupwa kwa bahari kunatokea pale maji ya bahari yanaposogea mbali na ufuo na kuingia zaidi baharini na kujaa kwa bahari ni pale maji yanaporudi.
Sababu ni kwamba mwezi unapokuwa juu ya eneo fulano la bahari, kwa kiuwa maji yako flexible ukilinganisha na ardhi, maji yanavutwa juu na nguvu za mwezi hivyo bahari kupwa na mwezi ukishapita maji yanarudi yaani kujaa.
Kwa hiyo basi kwa vitu vikubwa kama dunia na mwezi nguvu za uvutano zinafika mbali sana lakini kwa vitu vidogo mfano rocket nguvu zinafifia baada ya distance fulani mfano nje ya anga la dunia na hivyo kukifanya chombo hicho kutokuwa na uzito(weight) kabisa.