Je, ni halali mke arithi mali mumewe akitangulia?

Je, ni halali mke arithi mali mumewe akitangulia?

Nyenyere

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
14,842
Reaction score
10,765
Wakuu umuofia kwenu,

Nianze kwa kukiri kuwa hii ni mojawapo ya mada ngumu kabisa kuijadili mbele ya kizazi cha leo, yaani kizazi kipya. Najua si kila mtu ataipokea kwa mtazamo wa kupingana kwa hoja, bali wako ambao wataibuka na matusi na kejeli, kwa wakuu wa mtazamo huo, niombe tu tuvumiliane. JF where we dare to talk openly ndio motto yetu.

Nianze kwa kuelezea mtazamo wangu kuhusu mchakato mzima wa ndoa hapo awali na kisha nioanishe na kile kinachofanyika hii leo.

Mtazamo wa awali
Ndoa ilikuwa na pande mbili, kwanza kabisa ni muunganiko wa ukoo wa mwanamke na mwanamume, halafu pia ilikuwa ni muunganiko wa mume na mke na kuwa familia moja, ama mwili mmoja. Kwa kawaida mwanamke alitakiwa kusubiri nyumbani kwa wazazi wake mpaka pale atakapochumbiwa, kisha kutwaliwa na mume. Wazazi wa mume ndio waliokuwa na jukumu la kuchagua kati ya mabinti wengi ili kumpata ambaye walidhani ataweza kuendana na kijana wao kwa kuzingatia jinsi walivyomlea.

Kijana yeye alionyeshwa tu kuwa tunataka uoe binti wa familia fulani, naye alipokea kwa mikono miwili. Wazazi walishafanya uchunguzi wote kujua ni familia gani inafaa, binti ni mwenye adabu na kujua malezi, hakuna magonjwa ya kurithi kwenye ukoo husika (mfano ukoma) n.k. Taratibu za posa zilifanyika, mahari ikatolewa na harusi ikapangwa. Binti kwa upande wake hakuwa na hoja ya kujadili, wazazi wake walichunguza ukoo na familia iliyoleta posa kuona kama ni wenye maadili na wachapa kazi, ili asije akapata dhiki mara aolewapo, hakuna magonjwa ya kurithi n.k. Ndio maana ilikuwa kawaida kuambiwa tutawapeni majibu siku zijazo, mtupe muda wa kutafakari.

Sasa katika dunia ya leo utaratibu huu unaweza kudhaniwa kuwa ni wa kipuuzi na kandamizi. Mtazamo huu hasa umejengwa kwenye jamii za kiafrika na wale wa kipato chini huko ulaya na Marekani. Nasema hivyo kwa sababu mfano jamii za kihindi bado wana mchakato huo mpaka sasa, ndio maana sio rahisi kwa mmakonde kuoa binti wa kibaniani. Ndivyo ilivyo kwa familia tajiri huko ulaya na marekani, binti hawezi kukurupuka tu kuolewa na mwanamume yeyote. Sasa jambo hili lina sababu muhimu sana kwa jamii hizi:

1. Vijana wadumu katika ndoa
Sikumbuki ni mara ngapi nimesikia maharusi kutoka koo tajiri wametengana. Siongelei wasanii ambao maisha yao ni usanii, naongelea matajiri wanaojulikana hivyo, waliotulia vema na familia zao. Hawa huhakikisha watoto wao wanaoa na kuolewa kwenye familia zinazoeleweka na vijana wenye maadili. Kama familia ni tajiri lakini wana sifa mbaya (mfano wauza unga) basi wazazi hukataa posa. Wanawalinda watoto wao.

2. Kukwepa magonjwa ya kuambukiza
Wazazi walikuwa makini kuona magonjwa ya kurithi hayaingizwi kwenye ukoo. Hili lilikuwa jambo la muhimu sana kwa magonjwa kama asthma, sickle cell anaemia, reprosy n.k.

3. Kulinda mali za ukoo/ familia
Kwa sababu wazazi waliwandaa watoto wao wa kiume kulingana na shughuli wanazofanya, kijana alitarajiwa aje kuwa mrithi wa kuendeleza mali za ukoo. Wazazi walihakikisha legacy yao haifi na kwa kuwa wanadamu muda wetu ni mfupi, ilikuwa ni muhimu kuhakikisha kuwa kijana anakua katika misingi ya kuendeleza hilo.

4. Kuendeleza kizazi bora
Utaratibu wote huu ulilenga kuhakikisha mwanamume anajenga kizazi bora kabisa kama mwendelezo wa ukoo. Kama mwanamke hakuwa na sifa za kuwa mke hangeweza kuolewa kwani uzao wake ungekuwa usio na maadili. Mwanamke ndiye mwalimu mkuu wa watoto katika familia.

5. Kupunguza uwezekano wa kutokea migogoro
Kwa sababu wazazi walitazama tabia na mwenendo wa mwanamke na mwanamume, hii ilipunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kutokea migogoro mikubwa isiyoweza kupata suluhu.

6. Kumfanya mwanamke kuwa sehemu ya ukoo
Mwanamke aliyeolewa kwa utaratibu huu alifanywa kuwa sehemu ya ukoo. Alibadili jina lake la mwisho kuwa la ukoo alikoolewa na ilikuwa heshima kubwa kwake. Ukoo mzima ulimpokea kama mwanafamilia na alikuwa na haki sawa na wanaukoo wengine. Kwa muktadha huu, hata matatizo yaliyojitokeza kwenye kati yake na mumewe, kimbilio la mke ilikuwa ni kwa wazazi wa mumewe (ukoo wake mpya) ambako alisikilizwa zaidi kuliko hata mumewe. Mke hakupaswa kupeleka shauri lolote kwao bali kama kungekuwa na tatizo kubwa la kuweza kufikia kushirikisha wazazi wake, basi wazazi wa mume wangehusika katika hilo, sio mwanamke ama mume wake.

Ndoa za siku hizi
Siku hizi ndoa si kati ya koo mbili, mchakato umetekwa na watoto. Mtoto anatafuta mke wake mwenyewe, anampeleka kwa wazazi wake kumtambulisha. Sasa mke wa namna hii hawawezi kamwe kuchangamana na wazazi wa mume, ndivyo ilivyo pia kwa upande wa wazazi wa mwanamke, hawawezi kwenda sawa na kijana muoaji.

Utakuta mtazamo wa ndoa kwa kijana ni tofauti kabisa na wazazi. Kinachofanyika ni wazazi kuamua kuruhusu tu waoane ili kuepusha lawama za kizazi kipya. Wazazi wa binti wataruhusu binti aolewe hata bure kwa sababu anaweza kuzalia nyumbani, kwani mara nyingi inapoletwa posa, ujue watu hao walishachomana sana tu. Sasa wamelewa penzi, ndipo wakaamua watafute ushahidi kwa jamii kwamba wanalala pamoja.

Sasa athari za ndoa ya aina hii
1. Hakuna muunganiko kati ya mke na wazazi wa mume
Mara nyingi muunganiko huu haupo kabisa. Wazazi hawaafikiani na mwenendo wa mwanamke na hivyo kuona mwana wao amepotea. Wakati binti akiolewa hapo zamani ilikuwa kawaida kabisa kumtembeza kwa ndugu mbalimbali ambako alipewa heshima kubwa na kutambulika rasmi kama mmoja wa wanaukoo. Lakini kwa mfumo wa kisasa, si ajabu kwa mwanamke kujulikana na wazazi wa mume tu, nasema kujulikana na si kuchangamana.

2. Hakuna muunganiko kati ya mume na mke
Kwa sababu wamekutana na kujenga mahusiano kwa kuzingatia mambo ya juu juu (false premises), pindi mambo hayo yanapoyumba ufa hutokea. Kila mmoja ana namna ya ku-react pale hali inapobadilika, hawana tabia zinazofanana. Sasa ijulikane kuwa ndoa sio mali bali ni character. Kama hamuendani kwenye tabia na mitazamo, basi ndoa haiwezi kuwa na maisha marefu. Ndipo tulipopata ule msemo ndoa ni kufanana, sio kufaana!!

3. Wazazi wanapoteza imani na kijana wao
Kama hapo juu, kwa vile wazazi wamemhesabu kijana wao kama amepotea, basi ni ushahidi kwao kuwa hana uwezo wa kujenga ukoo bora na pia kusimamia mali za familia. Hawawezi kukubali kamwe kumwamini katika hilo na pia hata mke watamwona kama ni mporaji tu. Wanaanzaje kuwa na imani na mwanamke ambaye hata historia yake hawaijui wala ukoo aliotoka?

4. Mume atatatoka kwao lakini mke atabaki kwao
Wakati mwanamume anatarajiwa kuwaacha wazazi wake akiambatana na mkewe wakaendeleze ukoo, ukweli ni kuwa mke atabaki kwa wazazi wake na mumewe atakuwa part time. Ni kawaida kwa mwanamke huyu pale akipishana na mumewe kusema sijafukuzwa kwetu, kama umenichoka nirudishe n.k. Huyu sio mwajiriwa wa kudumu, ni kibarua tu ndani ya ndoa asiye na mkataba. Kwani hata akiona mambo yamekuwa magumu kimaisha hachelei kumwacha mumewe kwa sababu hana muunganiko wa kweli naye. Tena anaweza hata kuanzisha project za siri akishirikiana na watu wa kwao (akimwibia mume). Ni aina ya mwanamke ambaye mara tu anapoingia kwenye ndoa huanza kujiandaa kutoka.

5. Mke atakuwa adui wa kudumu wa ndugu wa mume
Mwanamke wa namna hii huwa ugomvi wa kudumu na ndugu wa mumewe, hasa wanawake wenzake. Hii hutokana na ama mafundisho potofu kuwa usiruhusu ndugu wa mume wakuzoee watavunja ndoa, ama sababu ya kutokubalika kwake ndani ya ukoo. Jambo hili litampelekea mwanamume kutothaminiwa na ndugu zake na hivyo wengi wa wanaume hujikuta wakijipambanua zaidi na ukoo wa mwanamke na hivyo wao kuolewa. Nyumba hugeuka kaa la moto kwa ndugu wa mume huku ndugu wa mke wakikaa kwa nafasi, mwanamume kwa vile hajui maana ya ndoa huona kuwa jambo la kawaida huku aliwatupia lawama ndugu na wazazi wake.

Vipi kuhusu mali?
Kufuatia mazingira ndoa za zamani, mwanamke hakuhitaji kurithi mali kwa sababu tayari alikuwamo kwenye ukoo wa mumewe. Hata kama mumewe angefariki, wazazi/ndugu wangesimamia mali hizo pamoja na matunzo ya mwanamke na watoto mpaka watoto wa kiume wapate ufahamu. Mwanamke kama mwolewaji asingeweza kurithi mali za ukoo kwani mali kwenda kwa mwanamke ni kuhamishia kwenda ukoo wake. Hata mtoto wa kike hakurithi kutoka kwa baba yake kwa sababu ataolewa kwenda kujenga ukoo mwingine. Pia kama mambo yangemshinda alipaswa kurudi nyumbani kwao ambako mali za ukoo zilitunzwa.

Mazingira ya namna hii yaalipelekea wazazi kuacha mali zao zisimamiwe na watoto wao wa kiume kwani walijua ziko kwenye mikono salama. Lakini leo hii hakuna mzazi anakubali kutoa mali zake kwa mtoto wa kiume kwa sababu ya mwenendo usiofaa. Kwa sababu ile misingi ya kuendeleza mali imekiukwa, vijana wamekuwa wanahisa kwenye ndoa, asilimia 50 kwa 50, hakuna muoaji wala muolewa. Vijana wanaanzisha koo zao wala si kuendeleza ukoo, yaani kilichobaki ni kujitambulisha kwa majina tu, mimi ni ukoo wa Lizarazu lakini kiuhalisia ni ukoo mpya kabisa. Ni kawaida siku hizi kuwaonyawazazi wasiingilie mahusiano ya watoto, tena mada hizi fitinishi zikitokea mpaka kweenye nyumba za ibada. Wazazi wako waliojinyima kukujengeamaisha ya baadaye unawatosa kwa sababu ya tamaa za kimwili. Baada ya kujidhiki ili mtoto wao awe na maisha bora, anakuja kuwalinganisha na mali na kuona hawaenei. Dunia inakwenda kasi sana.

Wako wanaojipambanua kudai wao wametafuta mali peke yao wakiwa na wake zao, hivyo mali hizo ni zao. Hawa huanzisha ukoo mpya kwa kutazama mali ambazo ikitokea zikaisha, wao ama watoto wao hutaabika sana kwa kukosa ndugu wa kuwa karibu nao. Walitumainia mali kuliko kuwekeza katika kuendeleza ukoo. Ndio maana siku hizi kumeibuka vita kubwa ya kugombea mali punde mume anapofariki. Hebu waza tu kwa akili ya kawaida, marehemu mzee wetu alietuacha màjuzi halafu mali zote zirithiwe na mke na hivyo ukoo wake kupotea kwenye ramani ya matajiri, kuna usawa hapo? Mwanamke atahamisha mali kwenda kwa ukoo wake.

Hizi ni baadhi ya sababu kwa nini mwanamke hakuwekewa kurithi mali tangu enzi. Tusubiri hoja za Mh Makonda kama zitaleta mabadiliko ya sheria.
 
النساء (12) An-Nisaa

Na fungu lenu ni nusu walicho acha wake zenu ikiwa hawana mtoto. Wakiwa na mtoto basi fungu lenu ni robo ya walicho acha, baada ya wasia waliyo usia au kulipa deni. Na wake zenu watapata robo ya mlicho kiacha, ikiwa hamna mtoto. Mkiwa mna mtoto basi sehemu yao ni thumni ya mlicho kiacha, baada ya wasia mlio usia au kulipa deni. Na ikiwa mwanamume au mwanamke anaye rithiwa hana mtoto wala wazazi, lakini anaye ndugu mume au ndugu mke, basi kila mmoja katika hawa atapata sudusi. Na wakiwa zaidi kuliko hivyo basi watashirikiana katika thuluthi, baada ya wasia ulio usiwa au kulipa deni, pasipo kuleta dhara. Huu ndio wasia uliotoka kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mpole.
 
Kwa uzi huu Nyenyere umechemka vibaya vibaya. Sina muda wa kuchanganua yote lakini mengi umekengeuka.
Mifano:
  1. Unasema ndoa za matajiri Ulaya hazivunjiki. Princess Diana na Prince Charles walikuwa masikini?
  2. Ati muwachagulie watoto wachumba ili kukwepa magonjwa ya kurithi kama ukoma? Ugonjwa wa ukoma siyo wa kurithi, kila siku kuna matangazo ya afya redioni kuhusu hiyo fact.
  3. Eti mume akifa ndugu zake wasimamie mali wakisubiri watoto wa kiume wakue? Na wa kike hawana haki? Huu ni ujima! Mimi wanangu wote wana haki sawa bila kubagua jinsia. Wote wamesoma shule za hadhi sawa na nimewaandikia urithi kabisa, sawa bi sawa. Kile nilichofanya nikapata mtoto wa kike ndicho hicho hicho nilichofanya nikapata wa kike, na thamani yao mbele yangu ni sawa kwa 100%, wote ni wanangu.
Mengine nimeacha ku-comment. Lakini nikuulize, kwanini usubirie ndugu yako afe ukarithi mali yake? Kwanini usitafute ya kwako?
 
Tatizo laanza kwa familia kumuona mke kama adui yao. Tukiondoa huo uchawi ndoa zetu zitakuwa imara sana na kuanzia hapo ndio mali na biashara zetu zitaendelea vizazi na vizazi.
Tukiwachukulia wanawake kama wachumaji tu. Au pale tunapokufa basi familia iwaone hawafai na familia ndiyo yenye haki ya kutawala mali ambazo wamechuma wao kutokea chini, hii ndo sababu kubwa ya hawa wanawake kujihami mapema
 
النساء (12) An-Nisaa

Na fungu lenu ni nusu walicho acha wake zenu ikiwa hawana mtoto. Wakiwa na mtoto basi fungu lenu ni robo ya walicho acha, baada ya wasia waliyo usia au kulipa deni. Na wake zenu watapata robo ya mlicho kiacha, ikiwa hamna mtoto. Mkiwa mna mtoto basi sehemu yao ni thumni ya mlicho kiacha, baada ya wasia mlio usia au kulipa deni. Na ikiwa mwanamume au mwanamke anaye rithiwa hana mtoto wala wazazi, lakini anaye ndugu mume au ndugu mke, basi kila mmoja katika hawa atapata sudusi. Na wakiwa zaidi kuliko hivyo basi watashirikiana katika thuluthi, baada ya wasia ulio usiwa au kulipa deni, pasipo kuleta dhara. Huu ndio wasia uliotoka kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi na Mpole.
Wakuu umuofia kwenu!
Nianze kwa kukiri kuwa hii ni mojawapo ya mada ngumu kabisa kuijadili mbele ya kizazi cha leo, yaani kizazi kipya. Najua si kila mtu ataipokea kwa mtazamo wa kupingana kwa hoja, bali wako ambao wataibuka na matusi na kejeli, kwa wakuu wa mtazamo huo, niombe tu tuvumiliane. JF where we dare to talk openly ndio motto yetu!!

Nianze kwa kuelezea mtazamo wangu kuhusu mchakato
Mwandishi umeandika, lakini ulichoandika huna taarifa sahihi.
Umeandika mambo msingi katika maisha ya binadamu. Hapa umeandika Ndoa, Mume na Mke, Mali na urithi.
Ingefaa ukaelewa kama kila mume na mke wanaoishi pamoja ni ndoa?
Aidha, ungejiuliza: mume na mke wana sifa sawa? Ukweli ni kuwa, mume na mke wameumbwa tofauti hivi kwamba, mke ni msaidizi wa mume.
Kwa maneno mengine, na hapa nisieleweke kama nadharau wanawake la hasha! Kwa sababu hivi ndivyo walivyoumbwa. Mwanamke hana uwezo wa kumiliki mali, bila mwanaume!
Kuhusu mali hili ni suala ambalo lina misingi yake. Mali ili uipate na ili wengine waweze kuindeleza inahitaji sifa au sheria. Bila ya hizo sifa au sheria hakuna mali pia hakuna kurithi au kuendeleza mali.
 
Mkuu Nyenyere,

Mtazamo wako upo sahihi kabisa.

Shida siku zinakimbia sana, mambo mengi yanabadilika: elimu, utamaduni, siasa, Imani, n.k. vyote vinabadilika kwa kasi sana kutokana na kuongezeka kwa muingiliano kati ya watu.

Ndio maana ndoa badala ya kuwa taasisi ya upendo inakuwa hisa ya 50% kwa 50%.
 
Mali zangu nikifa kama nina mke wakati huo zote anabeba mke, sio ndugu wala nani mwingine, hadi tumependana na kuoana means I trust her 100% na ni my other half, nikiondoka kila kitu anabaki nacho. Kama nina watoto wakati huo najua sitooa jinga la kuwatupa, atawajali vizuri tu, na hakuna kulea watoto waje kua lazy, watoto walee wajue kujitafutia wenyewe, wakifika in their 20s hawahitaji hata hela za wazazi, wanakua na uwezo wa kujianzishia biashara wenyewe. Swala ni kua na mke mwema tu, ukiwa na kilaza na mwenye tabia za kijinga sijui umeoa kwa sababu ipi. Ndugu watajijua aisee, wao kama walishindwa kunitumia vizuri wakafungua biashara zao wakati mi mzima, wasisumbue familia yangu kabisa nikiwa nimekufa, ni sawa na kusema mzee afe alafu uone ndugu wa baba waje kumsumbua mama, haimake sense kabisa.

Watu mnamuona mke ka chui, kama mwanamke huwezi kumuamini 100% basi usioe. I date a woman I can trust period. Love does exist
 
Kwa uzi huu Nyenyere umechemka vibaya vibaya. Sina muda wa kuchanganua yote lakini mengi umekengeuka.
Mifano:
  1. Unasema ndoa za matajiri Ulaya hazivunjiki. Princess Diana na Prince Charles walikuwa masikini?[/B]

    Tunaongelea wingi mzee, nikuulize swali. Ina maana ni Princess Diana pekee mwenye ndoa ya kitajiri ulaya? Kww nini si wengine? Unapojadili hoja elewa exceptional cases zipo, itakusaidia. Pili ndoa ya Diana ni ya kisiasa zaidi hivyo haqualify hapa.

    [*]Ati muwachagulie watoto wachumba ili kukwepa magonjwa ya kurithi kama ukoma? Ugonjwa wa ukoma siyo wa kurithi, kila siku kuna matangazo ya afya redioni kuhusu hiyo fact.

    Kwani hoja ni ugonjwa wa ukoma? Mbona yapo mengine hapo? Jifunze kujua kiini cha mada kuliko kujadili vionjo vy pembeni. Kuhusu hilo la ukoma mimi nimeandika kufuatia jamii ilivyoamini zama hizo, kama si kweli vipo kuhusu sickle cell? Unajishusha mkuu, jadili kiini cha hoja.

    [*]Eti mume akifa ndugu zake wasimamie mali wakisubiri watoto wa kiume wakue? Na wa kike hawana haki? Huu ni ujima! Mimi wanangu wote wana haki sawa bila kubagua jinsia. Wote wamesoma shule za hadhi sawa na nimewaandikia urithi kabisa, sawa bi sawa. Kile nilichofanya nikapata mtoto wa kike ndicho hicho hicho nilichofanya nikapata wa kike, na thamani yao mbele yangu ni sawa kwa 100%, wote ni wanangu.

Hoja yangu ni kwa mtazamo wa awali na pia maana ya kwa nini mwanamke hakurithi mali. Mambo ya kugawia watoto wako wa kiume na wakike ni yako na wanao. Soma hoja changia tu kiustaarabu, hujaelewa hata kiini cha mada. Ulipaswa kujibu swali kuwa wake wa ndoa warithi mali ama la, basi.


Mengine nimeacha ku-comment. Lakini nikuulize, kwanini usubirie ndugu yako afe ukarithi mali yake? Kwanini usitafute ya kwako?

Wapi nimesema usubiri ndugu afe urihi mali? Mkuu hunitendei haki kutoa povu bila kusoma. Nimesema mali zinatunzwa mpaka watoto WAKIUME wanapopata ufahamu. Hakuna ndugu anarithi mali, wala hakuna mahali nimesema hivyo.

2. Lakini pia, hata kama ikitokea mume kafa bila watoto, unadhani ni sawa mke wa ndoa asombe kila kitu? Hili linakuja kwa ndoa zenu za kisasa ambazo mke na mume ni wanashea. Ni kampuni inayojiita ndoa, lakini machoni pa kweli ya Mungu si ndoa hata kidogo. Ndoa ya kweli ni mke kutolewa na baba kwenda kwa baba wa kijana wakaunganishwa kwa ndoa. Ndoa ya kweli haifungwi kanisani wala msikitini, huko ni ushuhuda tu kuwa mmeoana. Baba wa binti akomtoa binti yake kwa baba wa kijana ndio ndoa hiyo mbele za Mungu.

Zamani wazee wakienda kuchumbia wqlikuwa wanasema "tunaomba kuzaliwa kwenye familia yenu," maana yake wanaomba binti akaendeleze ukoo wao kwa kuwazaa, yaani kuwazalia watoto. Siku hizi ndio tunasikia hayo ya, "nimesomesha sawa, nimegawa mali sawa n.k."
 
Tatizo laanza kwa familia kumuona mke kama adui yao. Tukiondoa huo uchawi ndoa zetu zitakuwa imara sana na kuanzia hapo ndio mali na biashara zetu zitaendelea vizazi na vizazi.
Tukiwachukulia wanawake kama wachumaji tu. Au pale tunapokufa basi familia iwaone hawafai na familia ndiyo yenye haki ya kutawala mali ambazo wamechuma wao kutokea chini, hii ndo sababu kubwa ya hawa wanawake kujihami mapema


Mkuu umesema kweli, ila tatizo linaanza na muoaji kutozingatia maagizo ya wazazi. Tunaoa vituko halafu tunawataka wazazi wawapokee, badala yake kwa sababu za kitabia wanapishana. Huo ndio mwanazo wa ugomvi. Tukianza kwa kuwasikiliza wazazi mengine yatakaa sawa.
 
Mwandishi umeandika, lakini ulichoandika huna taarifa sahihi.
Umeandika mambo msingi katika maisha ya binadamu. Hapa umeandika Ndoa, Mume na Mke, Mali na urithi.
Ingefaa ukaelewa kama kila mume na mke wanaoishi pamoja ni ndoa?
Aidha, ungejiuliza: mume na mke wana sifa sawa? Ukweli ni kuwa, mume na mke wameumbwa tofauti hivi kwamba, mke ni msaidizi wa mume.
Kwa maneno mengine, na hapa nisieleweke kama nadharau wanawake la hasha! Kwa sababu hivi ndivyo walivyoumbwa. Mwanamke hana uwezo wa kumiliki mali, bila mwanaume!
Kuhusu mali hili ni suala ambalo lina misingi yake. Mali ili uipate na ili wengine waweze kuindeleza inahitaji sifa au sheria. Bila ya hizo sifa au sheria hakuna mali pia hakuna kurithi au kuendeleza mali.
Nakiri kuwa sijakuelewa hasa hoja yako ni ipi, naomba ufafanuzi zaidi
 
hoja yako ni ipi, naomba ufafanuzi zaidi
Hoja yangu hapa ni hayo mambo uloyoyabainisha (Ndoa, Mke na Mume, Mali na Urithi).

Umeandika suala la wanawake kurithi mali kama ni halali.

Kwa kweli mwanamke alivyoumbwa hana uwezo wa kumiliki mali. Anaweza kufanya hivyo: kumiliki mali na hata mambo mengine, chini ya mwanaume.

Nguvu ya mali inapita kwa mwanaume kwenda kwa mwanamke.

Hii haina maana kwamba mwanamke hana nafasi katika mali na mambo mengine ya maisha.

Nafasi ya mwanamke katika maisha ni msaidizi. Ukijua nafasi ya msaidizi utaelewa nafasi ya mwanamke.

Kuhusu mali na kurithi mali. Hapa ni vizuri kufahamu kuwa mali ni jambo ambalo halina majibu ya moja kwa moja katika uwezo wa mwanadamu.

Kwa kweli suala la mali ni la sheria na sifa fulani. Mtu anaemiliki mali ana sifa fulani. Mali alizonazo hakuzipata tu isipokuwa kwa sifa na sheria fulani.

Hivi ndivyo itawezekana kurithi mali. Kama baba ana mali ili uweze kuzirithi na kuziendeleza lazima uwe ulimsikiliza mwenye mali.

Ndoa, hapa kwa kweli, licha ya kuangali vitu vingi kama imani, tabia na magonjwa, lakini haya yote kwa yenyewe hayafanyi mtu mume na mtu mke waishi pamoja na kwa tendo hilo liitwe ndoa, isipokiwa kwa njia ya sakramenti ya ndoa.

Hiki tunachokishudia hii leo kina sababu kuu mbili.

Sababu ya kwanza watu wengi hawana ndoa. Hawa kwa vyovyote vile hawawezi kuishi salama.
Sababu ya pili, wale walio na sakramenti ya ndoa hawaishi sheria ya ndoa. Wanachanganya.

Niseme kuwa, kama watu wanaishi bila sakramenti ya ndoa, au wana sakramenti ya ndoa, lakini hawaiishi, hakuna chochote kinaweza kuwa na manufaa kwao wao wenyewe, watoto na jamaa zao.
 
Wakuu umuofia kwenu!
Nianze kwa kukiri kuwa hii ni mojawapo ya mada ngumu kabisa kuijadili mbele ya kizazi cha leo, yaani kizazi kipya. Najua si kila mtu ataipokea kwa mtazamo wa kupingana kwa hoja, bali wako ambao wataibuka na matusi na kejeli, kwa wakuu wa mtazamo huo, niombe tu tuvumiliane. JF where we dare to talk openly ndio motto yetu!!

Nianze kwa kuelezea mtazamo wangu kuhusu mchakato mzima wa ndoa hapo awali na kisha nioanishe na kile kinachofanyika hii leo.

Mtazamo wa awali
Ndoa ilikuwa na pande mbili, kwanza kabisa ni muunganiko wa ukoo wa mwanamke na mwanamume, halafu pia ilikuwa ni muunganiko wa mume na mke na kuwa familia moja, ama mwili mmoja. Kwa kawaida mwanamke alitakiwa kusubiri nyumbani kwa wazazi wake mpaka pale atakapochumbiwa, kisha kutwaliwa na mume. Wazazi wa mume ndio waliokuwa na jukumu la kuchagua kati ya mabinti wengi ili kumpata ambaye walidhani ataweza kuendana na kijana wao kwa kuzingatia jinsi walivyomlea.

Kijana yeye alionyeshwa tu kuwa tunataka uoe binti wa familia fulani, naye alipokea kwa mikono miwili. Wazazi walishafanya uchunguzi wote kujua ni familia gani inafaa, binti ni mwenye adabu na kujua malezi, hakuna magonjwa ya kurithi kwenye ukoo husika (mfano ukoma) n.k. Taratibu za posa zilifanyika, mahari ikatolewa na harusi ikapangwa. Binti kwa upande wake hakuwa na hoja ya kujadili, wazazi wake walichunguza ukoo na familia iliyoleta posa kuona kama ni wenye maadili na wachapa kazi, ili asije akapata dhiki mara aolewapo, hakuna magonjwa ya kurithi n.k. Ndio maana ilikuwa kawaida kuambiwa tutawapeni majibu siku zijazo, mtupe muda wa kutafakari.

Sasa katika dunia ya leo utaratibu huu unaweza kudhaniwa kuwa ni wa kipuuzi na kandamizi. Mtazamo huu hasa umejengwa kwenye jamii za kiafrika na wale wa kipato chini huko ulaya na Marekani. Nasema hivyo kwa sababu mfano jamii za kihindi bado wana mchakato huo mpaka sasa, ndio maana sio rahisi kwa mmakonde kuoa binti wa kibaniani. Ndivyo ilivyo kwa familia tajiri huko ulaya na marekani, binti hawezi kukurupuka tu kuolewa na mwanamume yeyote. Sasa jambo hili lina sababu muhimu sana kwa jamii hizi:

1. Vijana wadumu katika ndoa
Sikumbuki ni mara ngapi nimesikia maharusi kutoka koo tajiri wametengana. Siongelei wasanii ambao maisha yao ni usanii, naongelea matajiri wanaojulikana hivyo, waliotulia vema na familia zao. Hawa huhakikisha watoto wao wanaoa na kuolewa kwenye familia zinazoeleweka na vijana wenye maadili. Kama familia ni tajiri lakini wana sifa mbaya (mfano wauza unga) basi wazazi hukataa posa. Wanawalinda watoto wao.

2. Kukwepa magonjwa ya kuambukiza
Wazazi walikuwa makini kuona magonjwa ya kurithi hayaingizwi kwenye ukoo. Hili lilikuwa jambo la muhimu sana kwa magonjwa kama asthma, sickle cell anaemia, reprosy n.k.

3. Kulinda mali za ukoo/ familia
Kwa sababu wazazi waliwandaa watoto wao wa kiume kulingana na shughuli wanazofanya, kijana alitarajiwa aje kuwa mrithi wa kuendeleza mali za ukoo. Wazazi walihakikisha legacy yao haifi na kwa kuwa wanadamu muda wetu ni mfupi, ilikuwa ni muhimu kuhakikisha kuwa kijana anakua katika misingi ya kuendeleza hilo.

4. Kuendeleza kizazi bora
Utaratibu wote huu ulilenga kuhakikisha mwanamume anajenga kizazi bora kabisa kama mwendelezo wa ukoo. Kama mwanamke hakuwa na sifa za kuwa mke hangeweza kuolewa kwani uzao wake ungekuwa usio na maadili. Mwanamke ndiye mwalimu mkuu wa watoto katika familia.

5. Kupunguza uwezekano wa kutokea migogoro
Kwa sababu wazazi walitazama tabia na mwenendo wa mwanamke na mwanamume, hii ilipunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kutokea migogoro mikubwa isiyoweza kupata suluhu.

6. Kumfanya mwanamke kuwa sehemu ya ukoo
Mwanamke aliyeolewa kwa utaratibu huu alifanywa kuwa sehemu ya ukoo. Alibadili jina lake la mwisho kuwa la ukoo alikoolewa na ilikuwa heshima kubwa kwake. Ukoo mzima ulimpokea kama mwanafamilia na alikuwa na haki sawa na wanaukoo wengine. Kwa muktadha huu, hata matatizo yaliyojitokeza kwenye kati yake na mumewe, kimbilio la mke ilikuwa ni kwa wazazi wa mumewe (ukoo wake mpya) ambako alisikilizwa zaidi kuliko hata mumewe. Mke hakupaswa kupeleka shauri lolote kwao bali kama kungekuwa na tatizo kubwa la kuweza kufikia kushirikisha wazazi wake, basi wazazi wa mume wangehusika katika hilo, sio mwanamke ama mume wake.

Ndoa za siku hizi
Siku hizi ndoa si kati ya koo mbili, mchakato umetekwa na watoto. Mtoto anatafuta mke wake mwenyewe, anampeleka kwa wazazi wake kumtambulisha. Sasa mke wa namna hii hawawezi kamwe kuchangamana na wazazi wa mume, ndivyo ilivyo pia kwa upande wa wazazi wa mwanamke, hawawezi kwenda sawa na kijana muoaji.

Utakuta mtazamo wa ndoa kwa kijana ni tofauti kabisa na wazazi. Kinachofanyika ni wazazi kuamua kuruhusu tu waoane ili kuepusha lawama za kizazi kipya. Wazazi wa binti wataruhusu binti aolewe hata bure kwa sababu anaweza kuzalia nyumbani, kwani mara nyingi inapoletwa posa, ujue watu hao walishachomana sana tu. Sasa wamelewa penzi, ndipo wakaamua watafute ushahidi kwa jamii kwamba wanalala pamoja.

Sasa athari za ndoa ya aina hii
1. Hakuna muunganiko kati ya mke na wazazi wa mume
Mara nyingi muunganiko huu haupo kabisa. Wazazi hawaafikiani na mwenendo wa mwanamke na hivyo kuona mwana wao amepotea. Wakati binti akiolewa hapo zamani ilikuwa kawaida kabisa kumtembeza kwa ndugu mbalimbali ambako alipewa heshima kubwa na kutambulika rasmi kama mmoja wa wanaukoo. Lakini kwa mfumo wa kisasa, si ajabu kwa mwanamke kujulikana na wazazi wa mume tu, nasema kujulikana na si kuchangamana.

2. Hakuna muunganiko kati ya mume na mke
Kwa sababu wamekutana na kujenga mahusiano kwa kuzingatia mambo ya juu juu (false premises), pindi mambo hayo yanapoyumba ufa hutokea. Kila mmoja ana namna ya ku-react pale hali inapobadilika, hawana tabia zinazofanana. Sasa ijulikane kuwa ndoa sio mali bali ni character. Kama hamuendani kwenye tabia na mitazamo, basi ndoa haiwezi kuwa na maisha marefu. Ndipo tulipopata ule msemo ndoa ni kufanana, sio kufaana!!

3. Wazazi wanapoteza imani na kijana wao
Kama hapo juu, kwa vile wazazi wamemhesabu kijana wao kama amepotea, basi ni ushahidi kwao kuwa hana uwezo wa kujenga ukoo bora na pia kusimamia mali za familia. Hawawezi kukubali kamwe kumwamini katika hilo na pia hata mke watamwona kama ni mporaji tu. Wanaanzaje kuwa na imani na mwanamke ambaye hata historia yake hawaijui wala ukoo aliotoka?

4. Mume atatatoka kwao lakini mke atabaki kwao
Wakati mwanamume anatarajiwa kuwaacha wazazi wake akiambatana na mkewe wakaendeleze ukoo, ukweli ni kuwa mke atabaki kwa wazazi wake na mumewe atakuwa part time. Ni kawaida kwa mwanamke huyu pale akipishana na mumewe kusema sijafukuzwa kwetu, kama umenichoka nirudishe n.k. Huyu sio mwajiriwa wa kudumu, ni kibarua tu ndani ya ndoa asiye na mkataba. Kwani hata akiona mambo yamekuwa magumu kimaisha hachelei kumwacha mumewe kwa sababu hana muunganiko wa kweli naye. Tena anaweza hata kuanzisha project za siri akishirikiana na watu wa kwao (akimwibia mume). Ni aina ya mwanamke ambaye mara tu anapoingia kwenye ndoa huanza kujiandaa kutoka.

5. Mke atakuwa adui wa kudumu wa ndugu wa mume
Mwanamke wa namna hii huwa ugomvi wa kudumu na ndugu wa mumewe, hasa wanawake wenzake. Hii hutokana na ama mafundisho potofu kuwa usiruhusu ndugu wa mume wakuzoee watavunja ndoa, ama sababu ya kutokubalika kwake ndani ya ukoo. Jambo hili litampelekea mwanamume kutothaminiwa na ndugu zake na hivyo wengi wa wanaume hujikuta wakijipambanua zaidi na ukoo wa mwanamke na hivyo wao kuolewa. Nyumba hugeuka kaa la moto kwa ndugu wa mume huku ndugu wa mke wakikaa kwa nafasi, mwanamume kwa vile hajui maana ya ndoa huona kuwa jambo la kawaida huku aliwatupia lawama ndugu na wazazi wake.

Vipi kuhusu mali?
Kufuatia mazingira ndoa za zamani, mwanamke hakuhitaji kurithi mali kwa sababu tayari alikuwamo kwenye ukoo wa mumewe. Hata kama mumewe angefariki, wazazi/ndugu wangesimamia mali hizo pamoja na matunzo ya mwanamke na watoto mpaka watoto wa kiume wapate ufahamu. Mwanamke kama mwolewaji asingeweza kurithi mali za ukoo kwani mali kwenda kwa mwanamke ni kuhamishia kwenda ukoo wake. Hata mtoto wa kike hakurithi kutoka kwa baba yake kwa sababu ataolewa kwenda kujenga ukoo mwingine. Pia kama mambo yangemshinda alipaswa kurudi nyumbani kwao ambako mali za ukoo zilitunzwa.

Mazingira ya namna hii yaalipelekea wazazi kuacha mali zao zisimamiwe na watoto wao wa kiume kwani walijua ziko kwenye mikono salama. Lakini leo hii hakuna mzazi anakubali kutoa mali zake kwa mtoto wa kiume kwa sababu ya mwenendo usiofaa. Kwa sababu ile misingi ya kuendeleza mali imekiukwa, vijana wamekuwa wanahisa kwenye ndoa, asilimia 50 kwa 50, hakuna muoaji wala muolewa. Vijana wanaanzisha koo zao wala si kuendeleza ukoo, yaani kilichobaki ni kujitambulisha kwa majina tu, mimi ni ukoo wa Lizarazu lakini kiuhalisia ni ukoo mpya kabisa. Ni kawaida siku hizi kuwaonyawazazi wasiingilie mahusiano ya watoto, tena mada hizi fitinishi zikitokea mpaka kweenye nyumba za ibada. Wazazi wako waliojinyima kukujengeamaisha ya baadaye unawatosa kwa sababu ya tamaa za kimwili. Baada ya kujidhiki ili mtoto wao awe na maisha bora, anakuja kuwalinganisha na mali na kuona hawaenei. Dunia inakwenda kasi sana.

Wako wanaojipambanua kudai wao wametafuta mali peke yao wakiwa na wake zao, hivyo mali hizo ni zao. Hawa huanzisha ukoo mpya kwa kutazama mali ambazo ikitokea zikaisha, wao ama watoto wao hutaabika sana kwa kukosa ndugu wa kuwa karibu nao. Walitumainia mali kuliko kuwekeza katika kuendeleza ukoo. Ndio maana siku hizi kumeibuka vita kubwa ya kugombea mali punde mume anapofariki. Hebu waza tu kwa akili ya kawaida, marehemu mzee wetu alietuacha màjuzi halafu mali zote zirithiwe na mke na hivyo ukoo wake kupotea kwenye ramani ya matajiri, kuna usawa hapo? Mwanamke atahamisha mali kwenda kwa ukoo wake.

Hizi ni baadhi ya sababu kwa nini mwanamke hakuwekewa kurithi mali tangu enzi. Tusubiri hoja za Mh Makonda kama zitaleta mabadiliko ya sheria.
Yaan tuvune wote af ukifa achukue mwingine jasho langu hivi naona😂😂
 
Asante mkuu, nimekuelewa vema. Nadhani hatutofautiani sana, sijasema mwanamke anaweza kurithi mali, hapana. Mwanamke hana sifa hiyo kwa mujibu wa sheria na mila na desturi pia. Ni kizazi hiki tu ndio kwa kutoelewa maana wanalilia wanawake warithi mali. Nazipitia hoja zako kama ifuatavyo:

Hoja yangu hapa ni hayo mambo uloyoyabainisha (Ndoa, Mke na Mume, Mali na Urithi).

Umeandika suala la wanawake kurithi mali kama ni halali.

Kwa kweli mwanamke alivyoumbwa hana uwezo wa kumiliki mali. Anaweza kufanya hivyo: kumiliki mali na hata mambo mengine, chini ya mwanaume.

Nguvu ya mali inapita kwa mwanaume kwenda kwa mwanamke.

Hii haina maana kwamba mwanamke hana nafasi katika mali na mambo mengine ya maisha.

Nafasi ya mwanamke katika maisha ni msaidizi. Ukijua nafasi ya msaidizi utaelewa nafasi ya mwanamke.

Nakubaliana nawe mkuu, mwanamke ni msaidizi tu, wala sijasema arithi mali. Mali ni za ukoo wa mwanaume, yeye ameletwa kuendeleza ukoo tu, naye amekuw sehemu ya ukoo huo, sio mrithi.

Kuhusu mali na kurithi mali. Hapa ni vizuri kufahamu kuwa mali ni jambo ambalo halina majibu ya moja kwa moja katika uwezo wa mwanadamu.

Kwa kweli suala la mali ni la sheria na sifa fulani. Mtu anaemiliki mali ana sifa fulani. Mali alizonazo hakuzipata tu isipokuwa kwa sifa na sheria fulani.

Hivi ndivyo itawezekana kurithi mali. Kama baba ana mali ili uweze kuzirithi na kuziendeleza lazima uwe ulimsikiliza mwenye mali.

Hapa pia hatupishani. Ili kurithi mali ni lazima umsikilize mwenye mali yaani baba, ndipo nikasema vijana wa siku hizi hawasikilizi baba zao, ndio maana nao hawawezi kuwaamini kurihi mali. Baba anasubiri mpaka anakufa matokeo watoto na ukoo wanaanza kugombana hovyo.

Ndoa, hapa kwa kweli, licha ya kuangali vitu vingi kama imani, tabia na magonjwa, lakini haya yote kwa yenyewe hayafanyi mtu mume na mtu mke waishi pamoja na kwa tendo hilo liitwe ndoa, isipokiwa kwa njia ya sakramenti ya ndoa.

Hapa tutatofautiana kidogo. Tendo la ndoa linakamilika pale wazazi wa mwanamke wanampokabidhi binti yao kw wazazi wa mwanamume. Makanisani huwa ni kuweka ushuhuda tu, soma ndoa zote zilizofungwa kwenye biblia. Kama wazazi hawataridhia basi ujue hakuna ndoa hapo, wala mkono wa Mungu haupo. Makanisa siku hizi yameteka mchakato wa ndoa na kuufanya kuwa ni wa kanisa, hili si sawa kabisa. Jambo hili pia limechangia kukengeuka kwa vijana wengi na kudharau nafasi ya wazazi.

Hiki tunachokishudia hii leo kina sababu kuu mbili.

Sababu ya kwanza watu wengi hawana ndoa. Hawa kwa vyovyote vile hawawezi kuishi salama.

Nakubaliana nawe kabisa

Sababu ya pili, wale walio na sakramenti ya ndoa hawaishi sheria ya ndoa. Wanachanganya.

Niseme kuwa, kama watu wanaishi bila sakramenti ya ndoa, au wana sakramenti ya ndoa, lakini hawaiishi, hakuna chochote kinaweza kuwa na manufaa kwao wao wenyewe, watoto na jamaa zao.

Hili msingi wake ni utii kwa wazazi na kuzingatia mafundisho toka utotoni. Leo hii tuna zama za zoa zoa!
 
Yaani unaoa kwa kufuata maelekezo ya wazazi? Kwani lazima wampende? Au wanakusaidia kutomba.a?
Oa kwa ajili yako na sio kwa ajili ya wazazi au mtu mwingine.

Mimi nilioa nikiyetaka mimi.

Wazazi wako walifanya jukumu la kukulea
Mkuu umesema kweli, ila tatizo linaanza na muoaji kutozingatia maagizo ya wazazi. Tunaoa vituko halafu tunawataka wazazi wawapokee, badala yake kwa sababu za kitabia wanapishana. Huo ndio mwanazo wa ugomvi. Tukianza kwa kuwasikiliza wazazi mengine yatakaa sawa.
 
Back
Top Bottom