Beesmom
JF-Expert Member
- May 30, 2016
- 17,221
- 28,666
Ni tukio limetokea jana jioni hapa uyole. Ndoa ina miaka mitatu mke hajabahatika kushika ujauzito. Sasa mama mtu alikuwa anapiga kelele juu ya hilo. Nataka mjukuu nataka mjukuu, mnataka nife sijaona wajukuu na kadhalika.
Ni mama mkwe hivo binti akawa hana la kusema zaidi ya tutapata mama na mume kumwambia mama yake kuwa na subra. Nadhani huyu mama aliona kelele za mbali hazifanyi kazi, akamwomba mwanae amtumie nauli aje awasalimie hivo akasafiri na tangu mwezi wa 6 yupo pale nadhani alikuwa anataka ashuhudie tumbo likinyanyuka akiwa pale pale.
Sasa kisa cha ugomvi ni nini? Unaambiwa tangu afike ni kelele hizohizo, sasa jana binti kamfuma mama anamwambia mwanae "Au uoe mke mwingine mwanangu?" Binti hakutaka kupepesa akamrukia mama na kumpa mabanzi ya mashavu ya maana. Mama kizunguzungu chali.
Mwenye mama kaghadhibika kamrukia mke. Kwanini unanipigia mama yangu wakati mimi nakuvumilia na maneno mengi mengi. Ndio hivo ugomvi ukawa ugomvi mpaka majirani kwenda kuamua.
Ni mama mkwe hivo binti akawa hana la kusema zaidi ya tutapata mama na mume kumwambia mama yake kuwa na subra. Nadhani huyu mama aliona kelele za mbali hazifanyi kazi, akamwomba mwanae amtumie nauli aje awasalimie hivo akasafiri na tangu mwezi wa 6 yupo pale nadhani alikuwa anataka ashuhudie tumbo likinyanyuka akiwa pale pale.
Sasa kisa cha ugomvi ni nini? Unaambiwa tangu afike ni kelele hizohizo, sasa jana binti kamfuma mama anamwambia mwanae "Au uoe mke mwingine mwanangu?" Binti hakutaka kupepesa akamrukia mama na kumpa mabanzi ya mashavu ya maana. Mama kizunguzungu chali.
Mwenye mama kaghadhibika kamrukia mke. Kwanini unanipigia mama yangu wakati mimi nakuvumilia na maneno mengi mengi. Ndio hivo ugomvi ukawa ugomvi mpaka majirani kwenda kuamua.