Je ni Haki Tanzania kuingilia uchaguzi wa DRC na kupeleka Wanajeshi wetu?

Mzalendo80

JF-Expert Member
Oct 30, 2010
2,508
1,338
Kwa kweli nimesikitishwa na Serikali za Tanzania na SA kuingilia Uchaguzi wa DRC kwa kumtetea Kabila kubaki kwenye dola kwa Gharama yoyote ile.

Je ni Haki Tanzania kuingilia uchaguzi wa DRC na kupeleka Wanajeshi wetu?

Habari zaidi download Doc ujue Serikali yetu inataka kutuingiza kwenye matatizo mengine zaidi ya haya tuliyokuwa nayo
 

Attachments

  • Fraude_Electorale[1].pdf
    158.2 KB · Views: 237
ccm wanaogopa wasibaki wenyewe ukanda huu'si unaona wanavyomwogopa sata wa zambia?sasa watafanya lolote lile kabila na museveni wabakie'si unamwona kikwete akiwa na wakenya anavyotetemeka?
 
Huyu Kikwete anataka kutuingiza kwenye Vita isiyokuwa yetu, tanzania tunanufaika vipi na DRC? Mambo yetu humu ndani yanatushinda. Kikwete anashindwa kuwachukulia Mafisadi Hatua, Je atawaweza Waasi wa DRC? Kikwete kama nakuomba rudisha Jeshi letu Nyumbani matatizo ya Wakongo watamaliza wenyewe
 
Tanzania imeshaanza kuchafuka toka Libya, Al shabaab, sasa Congo tunakoelekea si kuzuri.
 
Nazani Kabila ni sisime c na siamekulia bongo kisisiem. Sitashangaaa
 
Haya majina ya kina jk ?? Jk (julias kambarage) alijitahidi kwa uwezo wake kuijenga tz na hii jk(jakaya kikwete) huyu ndiyo hovyo kbs keshaibomoa tz sasa anataka kuipoteza kbs kwenye uso wa dunia.

Anataka kurudia makosa aliyoyafanya mzee wake kwa kumsaidia swaiba wake wa uganda kumng'oa idd amin ili swaiba wake achukue nchi.Matokeo yake 2kanyukana na uganda mpaka ikamfanya gaddaf kumsaidia idd amin baada ya kubaini ushenzi huo.
Sasa na huyo kimbora wa leo anataka ku2ingiza tena matatizon.
Haya sawa kapeleka wanajesh na kabila akashinda wale wapinzan wakasirike na kuanza kuishambulia tz je 2taweza kustahimil na kuwazuia??

Ikiwa kukabiliana na vibaka,wez na majambaz wenye siraha huwa unakuwa mzito.
Je mziki wa waasi wa kong 2tauweza??

Nch ye2 mpaka sasa ni hoi bin taaban kiuchumi je 2kijiingiza kwenye chokochoko na waasi itakuwaje ??
 
Serikali ya Tz ndo mtoa mafunzo mkuu wa wizi wa kura East and Central Africa. Hao wanajeshi wamekwenda kuiba kura ili wamsaidie Kabila kuiba kura ashinde.

Kila auaye kwa upanga atakufa kwa upanga! Mungu si dhalimu, huyu mtu mmoja anatutendesha dhambi nchi nzima hakika nawaapieni Mungu hatamwacha, subirini mtaona
 
kwa kweli nimesikitishwa na serikali za tanzania na sa kuingilia uchaguzi wa drc kwa kumtetea kabila kubaki kwenye dola kwa gharama yoyote ile.

Je ni haki tanzania kuingilia uchaguzi wa drc na kupeleka wanajeshi wetu?

Habari zaidi download doc ujue serikali yetu inataka kutuingiza kwenye matatizo mengine zaidi ya haya tuliyokuwa nayo

mimi nilivyosoma ktk media kuwa mtu kajiandikisha kinshasa lkn jina wakti wa kupiga kura limeonekana lubumbashi,nikajua kuwa fitina za kina lewis makame zimeshapelekwa drc. Nimesikia kuwa tendwa yuko huko pia. Kabila mwenyewe sio mkongo wacha wakongo wamchague mkongo mwenzao.
 
nashindwa kuelewa viongozi wa tz.inchi inafaika vipi kiuchhumi na kijamii,kumbukumbu bado tunazo,tumesaidia harakati za ukombozi wa kusini mwa africa.Je? imepata faida gani je raia wa zimbabwe,msumbji,nambia na africa kusini wa wanatambua kama tumetumia rasrimali zetu kwa ajili ya uhuru wa inchi zao? kuna nini DRC au nimasilai ya kina shimbo? Mahitaji ya ndani pesa hakuna,je hizi za kusaidia vita zinatoka wapi?
 
Kuweni na uzalendo kuwa Taifa lenu pamoja na matatizo yenu ya Ndani lakini Nje bado mna heshima,tusiwe watu wa negetive hata kwa yale ya msingi.Hakuan kitu Mwalimu nyerere alipigania kwa nguvu zake zote kama Congo,na ukweli kwa mtizamo wangu,hakuna Taifa lilifaidaika na hisani ya Mwalimu kwa watu wake kama Congo.

Kama sio Mwalimu leo hii hata Hsitoria yetu ya Utamaduni wa Muziki na vionjo vya muziki kabla na zaidi baada ya uhuru imejaa viojo na ladha ya kikongo.Kwa kuwa Mwalimu kama Rais wa Nchi angeweza kufanya banning kwa wakongoman kuingia tanzania na kupewa vibali na kufanya muziki na biashara kama wao kwao.

Leo hii tumekuwa na wakongoman watanzania ambao wameifia Nchi,mfano ni Remmy Ongara, na na wengineo walio waliotangulia mbele ye haki na wengineo wliohai lakini nyimbo zao zinabeba nafasi ya utaifa kwa vionjo vyake kama KING KICK.

Hivyo msiaangalie kwenye uwanja na mizania ya kisiasa angalia kwenye undugu.Mwalimu wakati wa bidii hizi nikitathimini leo naoana maaamuzi yake mengi hayakuangalia maiangira ya kisiasa zaidi aliangalaia utu wa mwafrika.Mwalimu aliamchukia sana MOBUTU alimuona mobutu kama pandikizi,hivyo nina hakika mkono wa mwalimu kuona pandikiza hilo linatoweka ulikuwepo,leo hii kongo kuna amani japo misuko suko ipo na kuwa wakati mwingine tutambue viongozi wao wengi walipata kuishai Tanzania na kusomea Tanzania wakati wakiangaika kuikombia Nchi yao toka mikononi mwa Mobutu.

Hivyo sio siri ya kutisha ni sawa na Mmarekani na IRAQ au AFAGHANISTAN eti kuwa watanzania hatuijui Kongo,tuache unafaiki,ingekuwa kama ni kisiasa na sio bidii za mwalimu binafsi kwa mataifa mengi sana ya Afrika,yamekuwa huru huku nyuma yake wana mkono wa Mwalimu.Wakati Mwngine tukijiona maskini sio kwa hiari yetu bali ni kuwa tulivaa viatu vya vya wenzetu hivyo tukalazimika kuwasaidia kwa mujibu wa utu na si kitu.Leo hii tumepoteza aina hiyo ya Muono tunaanglia KITU badala ya UTU.

Mkono wa Mwalimu umefanya kazi MSUMBIJI,ANGOLA,ZAMBIA, SOUTHA AFRICA,ZIMBABWE,SOUTHA AFRICA, BOTSWANA, UGANDA, RWANDA , BURUNDI,ZAIRE /KONGO DRC.UGANDA NA SUDAN.

Mkono wa Mkapa umefanya kazi KONGO DRC ,RWANDA NA BURUNDI

Mkono wa Kikwete umefanya kazi KENYA,NJUANI, NA MISSION ZINGINE ZA KIMATAIFA.

Tufike sehemu hata na yo Serikali iwe na muda wa kutunza siri zingine ziwekwe wazi umma ujue gharama za Watanzania kwenye mataifa mengine.Tuna miaka Hamsini ya uhuru Taifa la Marekani ukaa na SILIKUU NYINGI SANA MIAKA ISHIRINI NA TANO NA KUENDELEA UZIWEKA WAZI.NIMATUMAINI YANGU KUWA MIAKA ISHIRINI NA MITANO SILI KUWEKWA NJE PIA INASAIDIA WALIOHUSIKA KWENYE MIKAKATI [MISSION]NAO KUPUMUA KAMA BINADAMU,NA HIVYO KUTOA ASSESSMENT YA MIMKATI HIYO YA SIRI YA WAKATI HUO.
 
Kila auaye kwa upanga atakufa kwa upanga! Mungu si dhalimu, huyu mtu mmoja anatutendesha dhambi nchi nzima hakika nawaapieni Mungu hatamwacha, subirini mtaona

Dua la kuku.

Maneno haya yanafanana na yale yanayotolewa na watu wasiotahiriwa.
 
Aibu sana, kwetu ngumu halafu ukasaidie kwa jirani?

Kuna mtandao wao wanaoutetea
 
Back
Top Bottom