kisute
Member
- Oct 6, 2010
- 54
- 3
Juzi rafiki yangu ambaye ni mfanyabiashara mkoani Tabora yalimkuta yafuatayo katika hali isiyo ya kawaida na hakutegemea kama mkewe mpendwa angemfanyia hayo. Akinisimilia alisema; kama ilivyo desturi ya mfanyabiashara yoyote usafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kufuatilia zilipo bidhaa na masoko mazuri. Katika biashara zake uchukua mzigo Mwanza , kupeleka Dar then Dar Kigoma, Arusha na kwingineko.
Wakati mwingine huchua hadi wiki moja hajarudi nyumbani kwake. Anasimulia kwamba; wamekaa na mkewe miaka tisa sasa na wamejenga nyumba kubwa ya kifahari, kwa bahati mbaya hawajabahatika kupata mtoto. Siku hiyo ya tukio, alifika mjini hapo saa mbili usiku na alikwenda moja kwa moja kwa mama yake mzazi kumsalimia. Mama yake alimwandalia chakula akala na baadaye alimwaga mamake na kurejea nyumbani kwake majira ya saa nnne usiku. Alipofika pale kwake alikuta taa za nje zimezimwa na za ndani hali kadhalika. Alipousogele mlango wa mbele akasikia watu wakinong'ona lakini hakutilia shaka, aligonga mlango mara kadhaa pasipo kujibiwa. Basi alizunguka uwani na kufunga komeo la nje la mlango wa kutokea uwani. Kisha alirudi tena kugonga mlango wa mbele, lakini ukimya ulitawala. Akakumbuka kwamba ndani ya nyumba yake alikuwa akiishi na mtoto wa dada yake ambaye anasoma sekondari kidato cha pili. Alimgongea ili amfungulie mlango, na akawa kafunguliwa. Desturi ya rafiki yangu akifika nyumbani huanzia bafuni kuandaa maji kisha huenda chumbani kuvua nguo ili aoge. Baada ya kuandaa maji alielekea chumbani kwake kupitia kwenye korido, lakini roho ilisita kuingia chumbani kwake. Alimwita mkewe akimwomba atoke chumbani, mkewe alifanya hivyo. Rafiki yangu alimhoji mkewe kulikoni chumbani honey mbona naogopa hata kuingia huko? Mkewe alimjibu hakuna kitu mme wangu. Mkewe akimjibu hayo akitembea kuelekea sebuleni ambako alifika na kuzima taa ya sebuleni kukawa giza nene nyumba nzima. Ghafla mmewe alipigwa kikumbo na mtu ambaye alitokea chumbani kwake. Rafiki yangu alijigonga ukutani na kuchanika kichwa, lakini alifanikiwa kuudaka mguu wa mwizi wake. Jamaa kuona sasa anaumbuka alimpiga teke zito usoni na kutokomea nje. Rafiki yangu alinyanyuka pale chini wakanza kufukuzana lakini hakufanikiwa kumpata mwizi wake. Wakati anarudi kwake alimwona mkewe akiwa kashikilia mkoba akitimua mbio, alijaribu kumkimbiza lakini mkewe aliingia nyumba ya tatu tu kutoka pale kwake na mlango alifungwa, baadaye alitoka jamaa mmoja na fimbo nene mithili ya mkono na chumba kingine alitoka kijana mwingine walianza kumpiga rafiki yangu ile mbaya. Rafiki yangu alipiga kelele kuomba msaada hukuakisema mke wangu unaniua ndipo mtoto wa dadake alifika na kuomba msaada zaidi. Rafiki yangu alikuwa kaumizwa vibaya sana. Watu walifika pale kujua kulikoni, nae aliwaeelezea kisa kizima na yaliyojiri. Wakati huo huo alipiga simu kw a wazazi wa mkewe na kwa mamay ke mzazi kumwelea yaliyomsibu. Rafiki yangu alienda Polisi kuchukua PF3 ili apate matibabu.
Anaomba ushauri nini afanye kwa mke wake huyo? kwani tangu akimbie usiku ule hajaonekana hadi sasa. Wazazi aliwapa taarifa nao kimya. Je, hayo ndo mapenzi ya kweli? Je ni vizuri mkewe kumletea wanaume katika nyumba yake? Je huko ni kudata au ni nini? Jamani niusaidieni.
Wakati mwingine huchua hadi wiki moja hajarudi nyumbani kwake. Anasimulia kwamba; wamekaa na mkewe miaka tisa sasa na wamejenga nyumba kubwa ya kifahari, kwa bahati mbaya hawajabahatika kupata mtoto. Siku hiyo ya tukio, alifika mjini hapo saa mbili usiku na alikwenda moja kwa moja kwa mama yake mzazi kumsalimia. Mama yake alimwandalia chakula akala na baadaye alimwaga mamake na kurejea nyumbani kwake majira ya saa nnne usiku. Alipofika pale kwake alikuta taa za nje zimezimwa na za ndani hali kadhalika. Alipousogele mlango wa mbele akasikia watu wakinong'ona lakini hakutilia shaka, aligonga mlango mara kadhaa pasipo kujibiwa. Basi alizunguka uwani na kufunga komeo la nje la mlango wa kutokea uwani. Kisha alirudi tena kugonga mlango wa mbele, lakini ukimya ulitawala. Akakumbuka kwamba ndani ya nyumba yake alikuwa akiishi na mtoto wa dada yake ambaye anasoma sekondari kidato cha pili. Alimgongea ili amfungulie mlango, na akawa kafunguliwa. Desturi ya rafiki yangu akifika nyumbani huanzia bafuni kuandaa maji kisha huenda chumbani kuvua nguo ili aoge. Baada ya kuandaa maji alielekea chumbani kwake kupitia kwenye korido, lakini roho ilisita kuingia chumbani kwake. Alimwita mkewe akimwomba atoke chumbani, mkewe alifanya hivyo. Rafiki yangu alimhoji mkewe kulikoni chumbani honey mbona naogopa hata kuingia huko? Mkewe alimjibu hakuna kitu mme wangu. Mkewe akimjibu hayo akitembea kuelekea sebuleni ambako alifika na kuzima taa ya sebuleni kukawa giza nene nyumba nzima. Ghafla mmewe alipigwa kikumbo na mtu ambaye alitokea chumbani kwake. Rafiki yangu alijigonga ukutani na kuchanika kichwa, lakini alifanikiwa kuudaka mguu wa mwizi wake. Jamaa kuona sasa anaumbuka alimpiga teke zito usoni na kutokomea nje. Rafiki yangu alinyanyuka pale chini wakanza kufukuzana lakini hakufanikiwa kumpata mwizi wake. Wakati anarudi kwake alimwona mkewe akiwa kashikilia mkoba akitimua mbio, alijaribu kumkimbiza lakini mkewe aliingia nyumba ya tatu tu kutoka pale kwake na mlango alifungwa, baadaye alitoka jamaa mmoja na fimbo nene mithili ya mkono na chumba kingine alitoka kijana mwingine walianza kumpiga rafiki yangu ile mbaya. Rafiki yangu alipiga kelele kuomba msaada hukuakisema mke wangu unaniua ndipo mtoto wa dadake alifika na kuomba msaada zaidi. Rafiki yangu alikuwa kaumizwa vibaya sana. Watu walifika pale kujua kulikoni, nae aliwaeelezea kisa kizima na yaliyojiri. Wakati huo huo alipiga simu kw a wazazi wa mkewe na kwa mamay ke mzazi kumwelea yaliyomsibu. Rafiki yangu alienda Polisi kuchukua PF3 ili apate matibabu.
Anaomba ushauri nini afanye kwa mke wake huyo? kwani tangu akimbie usiku ule hajaonekana hadi sasa. Wazazi aliwapa taarifa nao kimya. Je, hayo ndo mapenzi ya kweli? Je ni vizuri mkewe kumletea wanaume katika nyumba yake? Je huko ni kudata au ni nini? Jamani niusaidieni.