Asanteni wote kwa ushauri, lakini hii saba mara sabini hamuoni ndo itakuwa lift yake kuwa kila akikosea atasamehewa?
Dini ndivyo inavyoshauri.
Binafsi nakushauri samehe (as in kupotezea na kuendelea na mahusiano) pale tu unapoona mhusika anastahili. Zaidi ya hapo utakua unacheza rumba wakati mwenzio kaweka kanda ya bongo fleva na hayuko tayari kubadilisha.
Ni vizuri kusamehe, na pia ni vizuri kujua sababu ya mtu kutenda kosa ...
Kujuwa sababu inaweza kukusaidia kufahamu source ya tatizo na kumshauri kubehave in a way ambayo hawezi kufanya kosa tena. Sabubu zingine zinaweza kuwa hata zimesababishwa na wewe mwenyewe kutokuwa karibu naye ....
Tafakari ....
Hello JF,
Ninapokuwa nimeudhiwa na mpenzi wangu nahitaji kujua sababu ya kwamba kwanini kafanya hivi ama vile au kumweka masharti ya msamaha?
@ Mbu, unajua wengine kiswahili tumekutana nacho shule labda niseme kwanini nihitaji utetezi wake. badala ya kwanini kafanya hivi ama vile.
Asanteni wote kwa ushauri, lakini hii saba mara sabini hamuoni ndo itakuwa lift yake kuwa kila akikosea atasamehewa?