Je, na katika hili tunahitaji watalaam wa uchumi? - ATCL

Ngonalugali

JF-Expert Member
Jan 12, 2008
659
102
Tanzania is exception in the world,
Mambo ambayo utayakuta hapa Tz si rahisi kuyakuta mahala pengine duniani. Kuna mengi ya kuzungumzia juu ya nchi hii na watu tuliowapa dhamana ya kulinda mali za walipa kodi lakini kwa leo naomba tujadili ya ATCL.
Kuna hili swala la ATCL kila siku kuomba pesa serikalini ili kulipa madeni lakini kwa kuangalia harakaharaka utakuta kwamba madeni mengine yanasababishwa na waliopewa dhamana ya kuliendesha shirika hilo.

Je, inawezekana vipi kwa shirika lenye ndege tatu kuwa na wafanyakazi 300? Unaweza wapi kupata faida na wakati huo huo kumudu gharama za uendeshaji kama una wafanyakazi 100 wanaotegemea kulipwa na ndege moja yenye uwezo wa kubeba abiria 50?
 
Tatizo hawafanyi kazi kwa ufanisi. Lakini pia watanzania tuko tayari kuona wafanyakazi wanapunguzwa?
 
Ikifanyika tathmini itaghundulika kuwa kati ya hao wafanyakazi 300, wengine ni marehemu na wengi hawana sifa kwa ajira wanazozitumikia.
 
Nilishawahi changia hoja hii ya ATCL, mkuu swala hapa sio wataalamu wa uchumi Tatizo ni political interest na professional omission kwa Chief Executives wamashirika yetu sio tu ATCL bali hata mashirika mengine. Rais akikwambia shida yako ni pesa nakupa pesa leo kesho nikukute barabarani (Angani), kitaalamu/technically inaweza isiwezekane. kwasababu kunaweza kuwa na mambo mengi ya kusettle kabla hujaanza kuruka. Lakini kwasababu ya nidhamu ya woga CEO anashindwa kutoa hoja za kitaalamu kupinga deadline ya Rais ambaye hanataaluma ya mambo hayo.

Swala jingine, economic recession in the world imepelekea kila siku tunasikia taarifa kutoka mashirika mbalimbali yakiforecast yataathilika vipi na suruhisho ni nini. Utasikia kulingana na haliiliyopo next may be 2 - 5 months tutalazimika kupunguza wafanyakazi say 800. Kwamaana hiyo kama hiyo ndio plan A then Plan B ni kuretain wafanyakazi given itapewa ruzuku na serikali. Sasa nchini kwangu TZ sijawahi sikia shirika linatangaza kupunguza wafanyakazi kutokana na economic distress. Ilinshangaza sana shilika la usafilishaji ''Scandinavian Express'' ilipoyumba kiuchumi iliambua kufukuza wafanyakazi kwa kisingizio hawana nidhamu, hawaperform, wezi na mambo kama hayo na kutowalipa haki yao yamsingi.

Hivyo mkuu toka ATCL ilivyoanza kuyumba ilitakiwa itoe taarifa ya kitaalamu. Kimsingi mashirika mengi bongo hayasemi ukweli kuwa hali ni mbaya inahitaji msaada utasikia malalamiko tu tuka kwa wafanyakazi. Mfano Kile Kiwanda cha mtibwa sugar pamoja na mkopo mkubwa kiliochukua bado haliilikuwa tete wafanyakazi kucheleweshewa mishahara na mambo kama hayo. Ndio hayo mkuu
 
Tatizo hawafanyi kazi kwa ufanisi. Lakini pia watanzania tuko tayari kuona wafanyakazi wanapunguzwa?

Shida si kupunguza wafanyakazi, shida ni kuangalia mazingira yaliyopelekea shirika lililokuwa na ndege mbili za kukodi hapo mwanzo kuamua kuajiri wafanyakazi lukuki namna hiyo.

Je, ni nani aliyepewa jukumu hilo na kusudi ilikuwa nini?
 
Ikifanyika tathmini itaghundulika kuwa kati ya hao wafanyakazi 300, wengine ni marehemu na wengi hawana sifa kwa ajira wanazozitumikia.

Hao marehemu walikuwa wanapokelewa hela na nani?
Na inawezekana vipi kwa mtu kuajiri waajiri hewa? Je, huyo mtu anahuruma na kodi ya watanzania?
 
Back
Top Bottom