Ripoti za CAG na TAKUKURU zilizowasilishwa mbele ya Rais Mapema leo Machi 29, 2023 zimeonyesha ufisadi mkubwa katika Mashirika Makubwa ya TRC, ATCL na TANESCO, Mhe Rais amesema waondoke swali je mnasubiri nini?
ATCL
“Kuna mradi hapa tumetengeneza Ndege ya mizigo ambayo tunakaribia kuipokea, last Installments ilikuwa tulipe dola milioni 37, invoice imekuja dola milioni 86….. unauliza mkataba ulisemaje? hii imetokana na wapi?, ooh vifaa vimepanda bei, vipi? mkataba wetu ulisemaje”
“Na bado aliyepokea anakuletea Serikalini hii ilipwe ndio invoice tumepokea….. stupid, ulipopokea umechukua hatua gani? umeuliza nini? umefanya nini? ukilitazama kwa undani hili ongezeko limeanzia huku ndani kuna Watu wameongea huko”
“Hatuwezi kwenda hivyo na nadhani hawa wanaopokea hizo invoice wakazileta kwa raha zao kabisa Serikalini watupishe, hawafai kuwa kwenye hizo nafasi, kama wanafaa angepokea huko akalihoji” Rais Samia.
TANESCO
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Salum Hamduni amesema Takukuru ilidhibiti hasara ya Sh81.99 bilioni ambayo Serikali ingepata kutokana na Shirika la Umeme Tanesco kutozingatia masharti ya mkataba baina yao na Kampuni ya Pan-African Energy Tanzania (PAET).
TRC
TRC ILIMKATAA MZABUNI WA TSH BILIONI 616.4 NA KUMPA WA TSH. TRILIONI 1.119 BILA SABABU ZA MSINGI
Akiwasilisha Ripoti ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo mbele ya Rais Samia, Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesema uamuzi huo ulisababisha ongezeko la matumizi ya Tsh. Bilioni 503.2 (82%) lisilokuwa na ulazima
Pia, katika ununuzi wa 'Locomotives' na Makochi ya Abiria, Shirika la Reli (TRC) lilitekeleza Mkataba bila dhamana ya Utendaji na kusababisha hasara ya Tsh. Bilioni 13.7 kutokana na Mkandarasi kushindwa kutimiza Masharti ya Mkataba
Aidha, CAG Kichere amesema Ukaguzi wake umebaini uwepo wa Manunuzi yenye Gharama Kubwa, Upotevu wa Fedha na Majadiliano ya Mikataba Yasiyolinda Maslahi ya Taifa na kusababisha kutofikiwa kwa Malengo yaliyokusudiwa
ATCL
“Kuna mradi hapa tumetengeneza Ndege ya mizigo ambayo tunakaribia kuipokea, last Installments ilikuwa tulipe dola milioni 37, invoice imekuja dola milioni 86….. unauliza mkataba ulisemaje? hii imetokana na wapi?, ooh vifaa vimepanda bei, vipi? mkataba wetu ulisemaje”
“Na bado aliyepokea anakuletea Serikalini hii ilipwe ndio invoice tumepokea….. stupid, ulipopokea umechukua hatua gani? umeuliza nini? umefanya nini? ukilitazama kwa undani hili ongezeko limeanzia huku ndani kuna Watu wameongea huko”
“Hatuwezi kwenda hivyo na nadhani hawa wanaopokea hizo invoice wakazileta kwa raha zao kabisa Serikalini watupishe, hawafai kuwa kwenye hizo nafasi, kama wanafaa angepokea huko akalihoji” Rais Samia.
TANESCO
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Salum Hamduni amesema Takukuru ilidhibiti hasara ya Sh81.99 bilioni ambayo Serikali ingepata kutokana na Shirika la Umeme Tanesco kutozingatia masharti ya mkataba baina yao na Kampuni ya Pan-African Energy Tanzania (PAET).
TRC
TRC ILIMKATAA MZABUNI WA TSH BILIONI 616.4 NA KUMPA WA TSH. TRILIONI 1.119 BILA SABABU ZA MSINGI
Akiwasilisha Ripoti ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo mbele ya Rais Samia, Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, amesema uamuzi huo ulisababisha ongezeko la matumizi ya Tsh. Bilioni 503.2 (82%) lisilokuwa na ulazima
Pia, katika ununuzi wa 'Locomotives' na Makochi ya Abiria, Shirika la Reli (TRC) lilitekeleza Mkataba bila dhamana ya Utendaji na kusababisha hasara ya Tsh. Bilioni 13.7 kutokana na Mkandarasi kushindwa kutimiza Masharti ya Mkataba
Aidha, CAG Kichere amesema Ukaguzi wake umebaini uwepo wa Manunuzi yenye Gharama Kubwa, Upotevu wa Fedha na Majadiliano ya Mikataba Yasiyolinda Maslahi ya Taifa na kusababisha kutofikiwa kwa Malengo yaliyokusudiwa