Je MNYIKA ALIJIANDAA KUPELEKA HOJA YA KATIBA?

AMARIDONG

JF-Expert Member
Jun 24, 2010
2,502
180
JUMAPILI ILIYOPITA ITV WALIRUDIA KONGAMANO LA KATIBA,NA MIMI NILIPATA BAHATI YA KUSIKILIZA HIYO JUZI KWANI MARA YA KWANZA SIKUWEZA KUSIKILIZA,NILIMSIKIA MBUNGE WA UBUNGO AKIMUULIZA NDUGU SHIVJI

""NAOMBA UNISHAURI NIPELEKE HOJA YANGU AU LA KUTOKANA NA ARTICLE 98 YA KATIBA NAPATA WASIWASI NA MAAMUZI YA RAISI KULINGANA NA HOJA YANGU""

HEE;;NILISHANGAA KWA KWELI NA MASWALI YAFUATAYO NILIJIULIZA

-JE MNYIKA ALIJIANDAA KWELI KABLA YA KUPELEKA PENDEKEZO LA HOJA YAKE OFISI ZA BUNGE
-JE MNYIKA ALIFANYA UCHUNGUZI WA KINA JUU YA HOJA YAKE KABLA YA KUAMUA KUONGEA KWA VYOMBO VYA HABARI?

-JE MNYIKA HANA UELEWA WA SHERIA HATA KWA KIASI KIDOGO KUJUA MADHARA NA MATOKEO YA HOJA ALIYOIANDAA ITAKAPOENDA BUNGENI

NAFIKIRI TZ SASA IMEKUWA NA MABADILIKO YA KISIASA NA ANAFIKIRI YANAENDELEA KUWEPO LAKINI SWALA LA WABUNGE HASA WA UPINZANI KWA MFANO KAFULILA,MNYIKA,LISU NA WENGINE KUKURUPUKA NA KUITA VYOMBO VYA HABARI KUSEMA WANAPELEKA HOJA BINAFSI BUNGENI ILHALI HAWAJAJIULIZA NA KUFANYA UCHUNGUZI WA KINA JUU YA HOJA ZAO KUNASHUSHA HADHI YA UPINZANI NA HUENDA WENGI WAKAISHIA KUZUNGUMZA MADUDU BUNGENI Na HOJA ZAO KUTUPWA KWENYE DUST BIN

FANYENI UCHUNGUZI WA KINA NA UPEMBUZI WA MAMBO KABLA YA KUDHAMIRIA KUPELEKA HOJA BUNGENI
 
Kaka Kuuliza si lazima kumaanishe kutokujiandaa!
Sometimes ni double-checking;On the other hand kutokuuliza si lazima kumaanishe kwambu muhusika amejiandaa!!!
Sikumbuki mara ya mwisho lini wapinzani walileta hoja ya kipuuzi kiasi cha kustahili kuwekwa kwenye dustbin,nonetheless Una haki ya kikatiba ya kuelezea mawazo yako!!!!
 
Hata mimi nilishangaa kwa kweli mheshimiwa mbunge anauliza apeleke au asipeleke hoja yake bungeni??sasa alikuwa anatangazia umma nini au ndio kukurupuka huko????
 
Nadhani alichomaanisha Mhe. Mnyika ni kujiridhisha na kipengele cha 98 kama kinatosheleza katika kuwapa uwezo/ushiriki wa wananchi katika utungaji wa katiba mpya. Hili lilifafanuliwa vizuri sana na Dr. Sengodo Mvungi, alipokuwa katika mjadala wa katiba mpya ulio-ongozwa na Masako katika ITV. Alisema ili wananchi waweze kushiriki kikamilifu katika utungaji wa katiba mpya, ni lazima Bunge liongeze ibara mbili katika kifungu hicho; moja ni kuundwa kwa baraza la kutunga katiba mpya ambapo ibara hiyo itataja wajumbe wake, na ibara ya pili ni kuhusu kura ya maoni itakayopigwa na wananchi, kukubali au kukataa katiba mpya. Ni vizuri mkawa mnatafakari kwanza kabla ya kutoa maoni/kuchangia hoja!
 
jiPANGENI JAMANI MNAAIBISHA CHAMA MNYIKA UNATEGEMEWA SANA CDM BOB MAKANI ANATEGEMEA uTAKUWA MWENYEKITI WA BAADAE KUTOKA UKANDA WA KWETU KULE TAFADHALI USITUANGUSHE
 
JUMAPILI ILIYOPITA ITV WALIRUDIA KONGAMANO LA KATIBA,NA MIMI NILIPATA BAHATI YA KUSIKILIZA HIYO JUZI KWANI MARA YA KWANZA SIKUWEZA KUSIKILIZA,NILIMSIKIA MBUNGE WA UBUNGO AKIMUULIZA NDUGU SHIVJI

""NAOMBA UNISHAURI NIPELEKE HOJA YANGU AU LA KUTOKANA NA ARTICLE 98 YA KATIBA NAPATA WASIWASI NA MAAMUZI YA RAISI KULINGANA NA HOJA YANGU""

HEE;;NILISHANGAA KWA KWELI NA MASWALI YAFUATAYO NILIJIULIZA

-JE MNYIKA ALIJIANDAA KWELI KABLA YA KUPELEKA PENDEKEZO LA HOJA YAKE OFISI ZA BUNGE
-JE MNYIKA ALIFANYA UCHUNGUZI WA KINA JUU YA HOJA YAKE KABLA YA KUAMUA KUONGEA KWA VYOMBO VYA HABARI?

-JE MNYIKA HANA UELEWA WA SHERIA HATA KWA KIASI KIDOGO KUJUA MADHARA NA MATOKEO YA HOJA ALIYOIANDAA ITAKAPOENDA BUNGENI

NAFIKIRI TZ SASA IMEKUWA NA MABADILIKO YA KISIASA NA ANAFIKIRI YANAENDELEA KUWEPO LAKINI SWALA LA WABUNGE HASA WA UPINZANI KWA MFANO KAFULILA,MNYIKA,LISU NA WENGINE KUKURUPUKA NA KUITA VYOMBO VYA HABARI KUSEMA WANAPELEKA HOJA BINAFSI BUNGENI ILHALI HAWAJAJIULIZA NA KUFANYA UCHUNGUZI WA KINA JUU YA HOJA ZAO KUNASHUSHA HADHI YA UPINZANI NA HUENDA WENGI WAKAISHIA KUZUNGUMZA MADUDU BUNGENI Na HOJA ZAO KUTUPWA KWENYE DUST BIN

FANYENI UCHUNGUZI WA KINA NA UPEMBUZI WA MAMBO KABLA YA KUDHAMIRIA KUPELEKA HOJA BUNGENI

Hoja yako ni ya kibinafsi sana kwa sababu hukutaka kumuelewa Mnyika kwa ukomo wa uelewa wako au hupendi apeleke hoja nbungeni. Mimi nilimwelewa kuwa hoja zilizotolewa kwenye kongamano zilikuwa nzuri na zenye changamoto. Katika hali hiyo siyo vibaya kupata mapendekezo mbadala. Kama ni hofu ya hoja kuporwa au kuzimwa bungeni kama ilivyochangiwa na Dr. Shivji sioni ubaya wake ni hofu yake kuwa wabunge wa CCM ni robots hawafikirii. That is unfair.

Ibara inayo husika inatoa wajibu kwa wabunge kama wawakilishi wa "wananchi" siyo chama. Yaani wana haki na wajibu wa kupeleka hoja zenye maslahi kwa wananchi. Kwa hiyo Mnyika alijitayarisha na amejitayarisha vizuri pia. Kumbuka kuwa hoja hiyo si ya Mnyika; ilikuwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chadema. Mimi nitawashangaa wasipopeleka hoja hiyo. Matokeo yo yote bungeni yataashiria mkakati mbadala kwa kutekeleza ilani yao.

Maoni yangu binafsi naona issue iliyopo ni Katiba Mpya siyo Mnyika amejitayarisha au la au si wabunge wengi wa CCM watapora au kuizima.
 
jipangeni jamani mnaaibisha chama mnyika unategemewa sana cdm bob makani anategemea utakuwa mwenyekiti wa baadae kutoka ukanda wa kwetu kule tafadhali usituangushe

it is an old and outdated tactic of personalising issues instead of being analytical with an objective of showing a way forward. Shame on you. Just be objective and help your mps to achieve.
 
Son of Soil,
Mh. Mnyika alitoa hoja nzito kwa mifano lukuki ktk kongamano na pia anatumia mfumo wa kuuliza si ujinga na ndio maana ya Kongamano a.k.a Brain-storming.

Kwa kukusaidia msikilize tena Mh. Mnyika akifanya 'Brain-storming' na waliohudhuria Kongamano, washiriki kama Jenerali Ulimwengu, Prof Shivji mara kadhaa walitumia maneneo nanukuu 'Nafikiri', 'Nadhani', 'Njia Mbadala', 'Sijui' n.k hii yote inadhihirisha heshima ya mijadala ya kisomi kuwa pia wenzio wanaweza kuwa wataalamu zaidi ktk nyanja fulani, sikiliza:


 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom