PreGE2025 Je, Mbowe anatumika ama anatumiwa?

PreGE2025 Je, Mbowe anatumika ama anatumiwa?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Nitakuwa wa mwisho kuamini Muasisi wa chama kugeuka na kuanza kukigalaliza kwa watawala chama alichokijenga kwa miaka zaidi ya 30 kwa damu na jasho, vifo vya wanachama, kufilisiwa, vilema yote hayo asahau kisa tu kakosa uongozi wa chama.

Unless habari za uasisi wake zilikuwa ni famba.

Yaani ni sawa mtu mzima kuamua kuuza nyumba yake moja kwa makusudi na kuhamia kwa kimada, yaani wakose wote yeye pamoja na wanafamilia.wake. Sababu tu wanafamilia wameona hafai kuwa baba anawapeleka ambako siko.
 
Hatimaye kaongea...

Wakati Hamahama bandia ya G55 ikiendelea, Mbowe amewakana watu hao ambao amesema wanatumia jina lake kuwahadaa watu.

Kuna taarifa kuwa Mbowe aliongea na Sugu na Mungai akiwataka wasiondoke CHADEMA wala wasirubuniwe na G55 ambao wamekuwa wakilitumia jina lake vibaya kuwahadaa wanachama wa CHADEMA.

Hayo yanakuja baada ya viongozi wengi wa mikoa na majimbo kupigiwa simu na viongozi wapya wa CHAUMMA wakiwaambia kuwa eti Mbowe anawataka waende CHAUMMA na watafute wanachama wapya wa CHAUMMA kwenye maeneo yao.

Baada ya tamko la Mbowe kwa watu wake wa karibu na waliomuunga sana mkono kwenye uchaguzi, kuwa wailinde CHADEMA na wasirubuniwe na wahuni, viongozi hao wamekuwa wakiwapigia simu viongozi mbalimbali ambao walimuunga mkono Mbowe kwenye uchavuzi, na kuwaambia kuwa wasithubutu kuhadaiwa na wahuni waliohongwa kuhamia CHAUMMA kwa kudhani kuwa wataidhoofisha CHADEMA.

Viongozi hawa waaminifu wakubwa wa Mbowe wamekuwa wakiwaambia wanachama kuwa, kama kuna matatizo au migongano yoyote ya chama katika maeneo yao, itamalizwa kwa amani kwa njia ya mashauriano, lakini wasikubali kurubuniwa.

Timu Mbowe kwa sasa imeingia front kuilinda na kuitetea CHADEMA. Siku zijazo zitakuwa ngumu sana kwa wale walioenda CHAUMMA ambao Mbowe amewaita ni wahuni.
 
wanaosema mbowe asisakamwe kwa sasa, wanashangaza sana. Ni mbowe huyuhuyu alishiriki kujenga imani kwa wafuasi wake kuwa CDM, ndio chama mama kwa matumaini mapya.

Roho nyingi za waja, zikateketea kwa ajili ya harakati zake na chama kama taasisi. damu zikamwagika kwa ajili ya vita watu kuwa upande wake.

Ni vibaya Mbowe kujitenga kwenye mchakato huu, maana damu za akina akwilina zinamdai jambo. jambo lenyewe ni Tanzania mpya ambayo watoto wa wataifa moja watasoma shule bora, ambazo hazitoleta ubaguzi wa kipato.

Nchi ambayo, watu wake hawatashindia mlo, nchi ambayo famalia fukara hazitoishia kuzishangaa familia tajiri za kisiasa.

Binafsi sio fundi wa elimu za kiroho, ila nina imani kwa vita ambayo mbowe aliianzisha, bado ana deni kubwa sana akikikwepa kikombe hiki.

Sawa, anaweza kujiona ameshinda kwa macho ya nyama na akaamua kuuchuna asijue nini kinaendelea. anaweza kuitazama misukosuko ya kina Heche na Lissu, kupitia kwenye side mirror, akiona nyakati zake pia zilishapita, ila kiroho bado ana deni linalomkata maini.

kimsingi, kama anaitwa mwamba wa siasa za kipinzani, basi afanye hayo hadi tone lake la mwisho. ajifunze kusamehe kama ambavyo walimpokea lowasa na kugombea urais. ajifunze kukubali mwanzo mpya, ikumbukwe hata yeye walimvumilia.

Sidhani huko aliko anafurahia kina lissu kuswekwa ndani, kama anafurahia, sioni kama ni siha njema kwa mustakabali wa damu ziizokwisha kumwagika kwa ajili yao.

Aidha nijuavyo, mwanasisa shupavu huenda na dira ya msimamo wake hadi mwishoni.
Hayo ya kulambwisha mlungura, hatuyafahamu, tunachojua ni kwamba mbowe una haja kumaliza kazi.ulioanzisha na kuaminisha wanazengo kuwa CDM, ndio kimbilio lenu.

kama waswahili hunena, kila mmoja atabeba msalaba wake, mimi naamini msalaba wa CDM, Pia utaubeba. haiwezekani watu waingizwe kingi kisha waache solemba.
 
Tabia yakumtegemea mtu ni dhambi na laana, Mbowe mbowee kilasiku huo ni ujinga.
Mungu kainua wengine kushikwa nafasi badala tuungane nao kusongambele kilasaa mtu anaheuka nyuma lumtafuta Mbowe!!! Huo niuzwazwa tuu
 
Paka kashaonja panya mwenye chumvi ...tuliombee tu Taifa
 
Mlishashinda uchaguzi na Lisu wenu pambaneni na hali zenu msimsumbue Mbowe
Kawaacha mfanye lolote mtakalo bila kuwaingilia sababu mlisema kazeeka kapitwa na wakati apishe wengine mshike kawapisha
Kaachake ilihali ndie anachochea kupitia CHAUMA?
 
Ninapo muona mtu anamsifu mbowe kama meanasiasa makini namuona mtu huyo kama Hana uelewa wa mambo ya siasa,mbowe sio mpinzani ma Wala hata kuwa mpinzani,muda sio mrefu mtajua kuwa huyu mbowe ni mtu wa aina Gani.Muda si mrefu mbowe atajitokeza na kuwaacha midomo wazi wale wote walio muamini



Mbowe ni mtu wa deep state.
Kwahiyo kupewa kesi ya ugaidi ilikuwa maigizo?
Kunyang'anywa Billicanas ni maigizo?
Kubomolewa green house yake na Ole Sabaya haya yote ni maigizo?

Hivi unaelewa hata maana ya Deep state?
 
Tujifunze kuweka akiba ya maneno muda utaongea.

Kama kweli Mbowe ana mpango wa kwenda CHAUMMA muda utaongea hakuna haja ya kumlisha maneno.

Na kama CDM wana ushahidi usio shaka kuwa Mbowe anawahujumu basi wafanye maamuzi magumu wamchukulie hatua za kinidhamu ikiwemo kumvua uanachama.

Kinyume na hapo hizi kampeni za vijembe hazisaidii chochote.
 
Back
Top Bottom