Siyo lazima iwe hivyo lakini unaeza kuua kwa makusudi au kwa kutokukusudia.
Marekani kule anakovamia anaua wengi wasio na hatia wakiwemo watoto wadogo mfano alifanya hivyo kule vietnam lakini hakufanikiwa kupata alichoikitaka zaidi ya kuua tu watu wengi kwa makusudi akarudia tena kwenye mataifa mengine mengi.
Unaposema "Marekani anakovamia" unamanisha nani huyo unayemsema "anakovamia" nani?
Ni muhimu kuwa precise. Marekani kuna taasisi ziko kuondoa roho za watu tu.
N akuna taasisi ziko kuokoa roho za watu.
Kuna mwanajeshi wa Marekani nilikuwa naongea naye, analalamika kwamba jeshi la Marekani lina sheria nyingi sana za kuhakikisha wanajeshi wanapigana vita kwa sheria.
Anasema wakitaka kuvamia sehemu nyingi na kufanyizia wanaweza kirahisi sana, tatizo jeshi linafuata sana sheria kiasi kwamba hata kupigana na ISIS inakuwa tabu.
Analaumu kwamba wanajeshi wanataka kufanyizia lakini sehemu nyingine mpaka wanatishiwa uhai, wanashindwa kujihami kwa kuangalia sana "rules of engagement".
Nenda Arabuni huko angalia ISIA wanavyochinja watu bila kitu cha msingi.
Halafu unakuja hapa unatuambia Marekani ji adui wa ubinadamu.
Uarabuni unaweza kuuawa kwa kuwa dini tofauti na Muislamu tu.
Marekani kuna uhuru wa kuabudu dini yoyote. Ni moja kati ya sababu watu walikimbia Ulaya kuja Marekani na mpaka leo wapenda uhuru tunaondoka nchi zenye majungu huko serikali inakwiba kuanzia kodi mpaka rambirambi.
Halafu Mmarekani anaibuka tu na kusema nitachukua watoto hawa nikawapeleke hospitali Marekani na wakipona nawapa scholarship.
Let that sink in.
Serikali imeiba mpaka rambirambi za wafu. Mmarekani kachukua watoto kawapeleka Marekani wakatibiwe. Na scholarship katoa juu.Mpaka chuo kikuu.
Halafu unaniambia Marekani ni adui wa ubinadamu?
Marekani ni pana kuliko kona moja unayoisema wewe.