Je, maendeleo ya kweli ni maendeleo ya watu au vitu? Wachumi tusaidieni, uchumi wa Awamu ya 5, unalisaidia Taifa au utaliangamiza?

Je, maendeleo ya kweli ni maendeleo ya watu au vitu? Wachumi tusaidieni, uchumi wa Awamu ya 5, unalisaidia Taifa au utaliangamiza?

Mimi ni mmoja wa watu nilio shabikia sana huyu bwana kuingia pale nyumba kuu ijapokuwa mimi binafsi sina chama

Tatizo nilio anza kuliona mwanzo na nikakosa viunganishi vya tunapokwenda labda huko mbeleni pindi nilipoona sekta binafsi kama hazipo ktk vipaumbele vya serikali hii na hazijengewi mazingira yoyote ya kukua awamu hii ni kama hakuna juhudi za makusudi kujenga hizi sekta binafsi na hasa kwa wajasiriamali ( mind kwamba mimi sijawahi pata ajira yoyote rasmi ktk maisha yangu zaidi ya miaka miwili tu baada ya kutoka high school) maisha yangu yanategemea vi miradi vyangu na najitahidi sana kuwa muadilifu, muaminifu kwa biashara zangu na hii ni falsafa yangu toka sijui yupo JK ( hapa watu wanasema kulikuwa sijui na loopholes nyingi za pesa safi na chafu)

Kiukweli ubunifu wa mtu mmoja mmoja na hasa kwa wajasiriamali umeanguka sana kwa wengi wetu na tuliokuwa tuna simamia 'ethics' za ujasiriamali tunahisi tumeingizwa sehemu si yetu

Kwa ufupi hatujui hii 'overhaul' itatupeleka wapi lkn hapa wengi wetu tupo ktk 'frustration' kuu
 
Tatizo lililopo kwenye ukuaji wa pato la taifa na maendeleo kwa jamii binafsi naona kuna vitu vinatakiwa kubadilishwa kwanza nadhani tuhame kwenye kuliangalia pato sana kuliko maendeleo.

Sekta zinazokuza uchumi wetu kwa kasi kubwa ni sekta ambazo hazitumii binadamu kama nguvu kazi kubwa (Mawasiliano,Mabenki,Viwanda n.k) na zile sekta ambazo zinatumia binadamu kama nguvu kazi kubwa hazina mchango mkubwa kwa pato la taifa (Uvuvi,Kilimo,ufugaji).

Sasa hapa ndipo shida inapokuja kuona pato linapanda ila hali inazidi kuwa ngumu na hii inachangiwa na hakuna kiunganishi kizuri kati ya sekta zisizotumia watu sana na zile sekta zinazotumia watu wengi.

Hivyo baadhi ya vitu vya kubadilishwa kwanza viko pande 2 serikali lakini na mwananchi pia anavitu anatakiwa afanye.

1.Uzalendo - tutukuze vya kwetu sana kama tukitumia bidhaa zetu hata kwa zile sekta za mashine zaidi itasaidia ukuaji na uhitaji wa bidhaa kutoka sekta zinazotumia binadamu sana.

2. Kufanya kazi kwa bidii,watu hawajatofautisha kufanya kazi sana na kufanya kazi kwa bidii.

3.Serikali kutengeneza mazingira mazuri ya uendeshaji na ukuaji wa sekta zinazotumia binadamu zaidi mfano:Mfano awamu ya 5 ni viwanda serikali ingeanza na wakulima ambao watalisha hivyo viwanda,na bidhaa za viwanda zitoke hapa hapa. Hii inamaanisha viwanda vitategemea wakulima/Wavuvi/Wafugaji na pia ukiachia viwanda na wafanyakazi wa viwanda pia watategemea itatengeneza muunganiko wa mzunguko wa fedha za sekta zote 2.

4. Japo tanzania inategemea kilimo sana lakini asilimia kubwa ya wakulima hawafanyi kilimo cha biashara hasa kile ambacho ni cha uhakika wengi wanalima kwa kutegemea kudra.hii inafanya sekta kuwa duni na muda mwingine kusababisha kutafuta hizo malighafi nje.Serikali ipitishe na kutenga maeneo kwa ajili ya ukulima wa zao fulani kwa muda fulani ili kulinda rutuba na matumizi ikiwezekana hata iwe mfano yenyewe.

5. Serikali kutafuta masoko nje ya nchi pia tuna mabalozi nchi kibao na bado ardhi yetu ni kubwa tu na inarutuba, kama serikali ingekuwa inatangaza mfano kuna uhitaji mkubwa wa dengu sehemu fulani na kukiwa ba kilimo cha uhakika wanaweza hata kuchukua tenda na wakulima wakalima kisha wakapeleka zikasafirishwa kw kupitia utaalam na weledi wa kufanikisha hilo.

6.Kupunguza lawana na kufanya kazi, watu wanachukua muda mwingi kulalamika kuliko kuwa sehemu ya utatuzi hili linafanya uchumi usipande na kurudi nyuma zaidi tunajikuta wachache wanaoziona fursa wanafanya kazi wanafanikiwa na uchumi unaonekana uko sawa kumbe wengi walikuwa wanaongea na wachache wamefanya.

Hivyo kuna vingi ila uchumi na maendeleo yanatutegemea sisi na serikali pia
 
Tlichonacho hapo ni kimoja tu.ARDHI ...Baasi

WATU hakuna
SIASA SAFI Hakuna
UONGOZI ndio kabisaaa hakuna..kuna utawala
 
Mahaba kwako mkuu...neno lako la mwisho naomba niliboreshe hivi: NCHI YENYE BARABARA ZA LAMI NA FLYOVERS ILHAHI WATU WANATAABIKA KIUCHUMI NI SAWA NA MAKABURI YALIYOPAMBWA NA ALMASI. Yana manufaa gani mapambo kwa marehemu? Fahari ya marehemu au mtunza makaburi?

Ethiopia ni mfano mzuri. Si yasifiwa kwa madaraja na reli, lakini ndio wanakotoka wahamiaji haramu...wanaondokea nini nchini mwao ikiwa mambo ni safi? Na haya mambo hayaji hivi hivi, utazame uongozi wa Ethiopia, shida ipo. Wanahama kwa kuwa utu wao umepimwa vs maghorofa.

Pascal Mayalla , waambie 'wateule wa mungu' kwamba, Mungu ametupa nafasi moja tu ya kuishi duniani (potelea mbali hata kama dunia yenyewe 'sio yake') basi watuache tuishi (badala ya kudumu) maana if we live well, once is enough. Tusitamanishwe kuifikia Ethiopia maana baadaye tutaitwa WAHAMIAJI HARAMU ambao Baba Yao anamiliki Sheba Miles lakini wanasafiri ndani ya Fuso na kupoteza maisha...YaRabbi tupe moyo wa ustahimilivu au mshana jr anisaidie kugeuka msukule nisijisikie vibaya kukaa 'makaburini'.
mfano mzuri sana
ETHIOPIA
 
GDP ikiongezeka ni rahisi kuimarisha miundo mbinu kwa faida ya kila mwananchi. Mimi ni mlala hoi naishi Tegeta, mke wangu mjamzito kapata tatizo la ghafla apelekwe Mwananyamala hosipitali, maadamu barabara ni imara ni chapchap mpaka hosipitali. Kama barabara ni mbovu angefia njiani. Hivyo maendeleo ya vitu ni muhimu, hata Marekani kuna masikini
 
Mimi sifahamu sana mambo haya,ila niulize kitu,hivi mwalimu Nyerere alikuwa mchumi?na kama alikuwa mchumi vipi alifanikiwa sana kutufanya tuige falsafa zake za kuongoza uchumi?pili,wakati wa utawala wake uchumi wa mtu mmoja mmmoja ulikuwa juu kuliko ulivyo sasa?tatu,nyanja kama za madini zilikuwa na udhibiti wa kutosha kuliko udhibiti huu anaoufanya Magufuli?Nne,Ningeomba ufafanuzi kidogo hapo penye maendeleo ya vitu,ni hayo tu,mnisaidie hapo.
Hili ndo tatizo kubwa la taifa letu. Kwa umri wako hukupaswa kuuliza hayo maswali. Ulipaswa kuwa umejifunza shuleni historia ya Nyerere.Hatuwezi kuleta maendeleo kama hatujui tulikotoka,tulipo na tunataka kwenda wapi.
 
Uliposema Nagufuli secta ya kilimo na ufugaji aliikuta hoi bin taabani bac nikaacha kusoma na post yako.

Mimi nimejiajir katika secta ya kilimo na ufugaji. Ninajua uhalisia.... magufuli kakuta hii secta ikikuuwa kwa kasi ya ajabu. Watu walikuwa na muamko mkubwa kuwekeza katika kilimo. Na hata serkal ya kikwete ilitoa mchango mkubwa sana kati kuwezesha hii secta. Kikwete alijitahidi kutoa pembejeo kwa Luzuku. Pia hata upande wa soko serkal iliweza nunua mazao ya nafaka pale bei zilipokuwa zikishuka sana na kutunza katika maghala ya Taifa. Tanzania ilifanya biashara ya mazao na kenya vizuri bila kuingiliwa na serkal.

Hivi sasa hakuna luzuku. Mkulima haba uhuru wa kuuza mazao yake nch anayotaka. Wadau wamepungua sana.
 
Hili ndo tatizo kubwa la taifa letu. Kwa umri wako hukupaswa kuuliza hayo maswali. Ulipaswa kuwa umejifunza shuleni historia ya Nyerere.Hatuwezi kuleta maendeleo kama hatujui tulikotoka,tulipo na tunataka kwenda wapi.
Nadhani ni bahati mbaya shule niliosoma sikufundishwa historia ya mwalimu Nyerere ndio maana nikauliza hayo maswali..
 
Wanabodi,

Hii ni thread ya swali, ambalo linatakiwa kujibiwa na wachumi wetu, Mwalimu Nyerere alituhusia "Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu na Sio Maendeleo ya Vitu". Wachumi wetu tusaidieni kutuelimisha, huu Uchumi wa Magufuli, Unalisaidia Taifa Kupata Maendeleo ya Watu, au Utatupatia Maendeleo ya Vitu Huku Uchumi wa Mtu Mmoja Mmoja Ukiangamia?.

Kama kawaida yetu kutumia the right to expression kuuliza, Jee awamu hii ya 5 ya rais Magufuli, inatumia falsafa gani ya kiuchumi?, jee uchumi huu wa Magufuli, unalisaidia taifa au unaliangamiza?. Kwa vile mimi sio mchumi, wachumi wetu, tusaidieni, tuelimisheni tunakwenda wapi?, are we heading to the right direction?.

Ili Tuendelee Tunahita Vitu Vinne, Vyote Tunavyo, Tumekwama Wapi?
Tulifunzwa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne,
  1. Watu-tunao
  2. Ardhi- tunayo
  3. Siasa Safi- tunayo?
  4. Uongozi bora-?
Kama vitu hivi vyote vinne tunavyo, sasa sisi Tanzania tumekosa nini?, kwa nini bado ni masikini?.

Kupanga ni kuchagua.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea.
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas ...
Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed ...
Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza ...
Ni swali makini linahitaji majibu makini
Utawala wa Mhe. John Joseph Pombe Magufuli uatisaidia Tanzania kama atatawala kwa vipindi viwili kama katiba yetu ya 1977 ilivyoweka ukomo. Maana kwa kiwango kikubwa anatimiza dhana nzima ya CCM ya ujamaa na kujitegemea. Yeye anaangalia kuogeza uwezo wa jamii kupambana na mazingira yao kwa ujumla wao na sio mtu mmoja mmoja. Ndio maana anawekeza kwenye miundombinu/miundo msingi. Ujenzi wa barabara za lami utaongezeka kwa kiwango kikubwa, bandari zitaimarisha na kupanuliwa kwa kiwango kikubwa, viwanja vya ndege na ununuzi wa ndege zenyewe utafanyika, ujenzi wa reli ya kisasa, kudhibiti wizi wa mali ya umma na hasa maliasili za taifa hili. Kwa uhakika hata nidhamu itarejea kwa baadhi ya viongozi na watumishi wa umma.

Baada ya miaka kumi, tutakuwa na mazingira bora kabisa ya kuendeleza uchumi wetu, lakini atakuwa ameua kwa kiwango kikubwa uwezo wa watu kuwa wabunifu na ujasiliamali. Tutakuwa na kasuku wengi zaidi kuliko watu huru, chama kushika hatamu ya uongozi itashika kasi kupita kiasi. Miradi ya umma itaanza kugharimia shughuli za chama tawala, na miungu watu watakuwa wengi kwa kisingizio cha rekodi nzuri ya uchumi na uzalendo. Nguvu kubwa itatumika kuimarisha utawala uliopo na hatimaye udikiteita uliopitiliza na huo ndio utakao kuwa mwanzo wa anguko la uchumi.

Ni hitimishe kwa kusema tangu rais aingie madarakani hadi sasa matendo yake yanausaidia uchumi wa Tanzania.
 
Mkuu Paskali; Maendeleo ni lazima yawe maendeleo ya watu. Maendeleo ya watu ni nini? Ni watu kuwa na mahitaji ya kijamii (elimu, afya malazi, chakula nk), uhuru, usawa na haki ya kuchagua unachopenda. Kimsingi maendeleo ni haki; ni sehemu ya utu, maendeleo ni utu. Sarakari zoote lazima zitufikishe hapo. Maendeleo ya vitu ni muhimu pia ila sio lengo la mwisho bali ni lengo litakalosaidia kupata maendeleo ya watu (ajira, kipato na mwishowe mahitaji ya kibinadamu kama nilivyoainisha hapo juu). Ardhi, watu, siasa safi na uongozi bora ni muhimu sana kwenye kufikia haya. Binafsi nina masha na Siasa safi na Uongozi bora; kama vimetusaidia sana. Tumekuwa na shida ya pseudo-politics na pseudo-leaders ambavyo vimekuwa vinajitafutia na kujitafuta bila kujali maslahi mapana ya watu.
 
Ethiopia Wana Miundo Mbinu Mizuri Uchumi Wa Vitu Uko Imara Lakini Wananch Wanakimbia Nchi Yao
 
Wewe na genge lako ndio zeroooos hivi unaanza vipi kupinga miundombinu ambapo vifo vingi vya akina mama wajawazito na wagonjwa nawakufa tu kisa barabara ni mbovu za kuwawaisha vituo vya afya au hao watu mnaowasema ni nani?

Huduma mbovu za kijamii zinatokana na miundombinu mibovu kama ukosefu wa umeme.

Nendeni kasome social economic development ndio mtajua huu upuuzi unatakiwa uongelewe vipi?

Hao watu wanapataje ajira kama hakuna miundombinu ya kusapoti viwanda? Huyo mkulima anauzaje Pamba yake usipomuwekea miundombinu bora ya kilimo na usafirishaji?

Pathetic
Mmh very pathetic argument
 
Ili Tuendelee Tunahita Vitu Vinne, Vyote Tunavyo, Tumekwama Wapi?
Tulifunzwa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne,
  1. Watu-tunao
  2. Ardhi- tunayo
  3. Siasa Safi- tunayo?
  4. Uongozi bora-?
1. Watu tunao lakini asilimia kubwa watu hawajielewi kwa kukosa maarifa ya kuleta mapinduzi katika Nyanja za kiuchumi .
( Yaani kutoka kwenye hali mbaya kuwa nzuri au nzuri kuwa nzuri zaidi)
2. Ardhi tunayo lakini under utilized
3. Siasa tunazo lakini sio safi (mifano unayo)
4.Uongozi bora haupo na ndio maana tunayumba.

Ili dhoruba isiwe kubwa USHIRIKIANO kati ya serikali, wanasiasa na wananchi kwa ujumla wake unahitajika sana.
UZALENDO wa kulinda na kutetea KATIBA na MALI ZA UMMA ndio unaohitajika kutuvusha hapa tulivyo na sio vinginevyo.
 
Wanabodi,

Hii ni thread ya swali, ambalo linatakiwa kujibiwa na wachumi wetu, Mwalimu Nyerere alituhusia "Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu na Sio Maendeleo ya Vitu". Wachumi wetu tusaidieni kutuelimisha, huu Uchumi wa Magufuli, Unalisaidia Taifa Kupata Maendeleo ya Watu, au Utatupatia Maendeleo ya Vitu Huku Uchumi wa Mtu Mmoja Mmoja Ukiangamia?.

Kama kawaida yetu kutumia the right to expression kuuliza, Jee awamu hii ya 5 ya rais Magufuli, inatumia falsafa gani ya kiuchumi?, jee uchumi huu wa Magufuli, unalisaidia taifa au unaliangamiza?. Kwa vile mimi sio mchumi, wachumi wetu, tusaidieni, tuelimisheni tunakwenda wapi?, are we heading to the right direction?.

Ili Tuendelee Tunahita Vitu Vinne, Vyote Tunavyo, Tumekwama Wapi?
Tulifunzwa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne,
  1. Watu-tunao
  2. Ardhi- tunayo
  3. Siasa Safi- tunayo?
  4. Uongozi bora-?
Kama vitu hivi vyote vinne tunavyo, sasa sisi Tanzania tumekosa nini?, kwa nini bado ni masikini?.

Kupanga ni kuchagua.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea.
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas ...
Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed ...
Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza ...
Tumekwama kwenye 3&4 No Welfare Economy. Tuna uchumi wa kukomoa Wananchi Wasomi wako Likizo. Read here>welfare economics
 
Wanabodi,

Hii ni thread ya swali, ambalo linatakiwa kujibiwa na wachumi wetu, Mwalimu Nyerere alituhusia "Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu na Sio Maendeleo ya Vitu". Wachumi wetu tusaidieni kutuelimisha, huu Uchumi wa Magufuli, Unalisaidia Taifa Kupata Maendeleo ya Watu, au Utatupatia Maendeleo ya Vitu Huku Uchumi wa Mtu Mmoja Mmoja Ukiangamia?.

Kama kawaida yetu kutumia the right to expression kuuliza, Jee awamu hii ya 5 ya rais Magufuli, inatumia falsafa gani ya kiuchumi?, jee uchumi huu wa Magufuli, unalisaidia taifa au unaliangamiza?. Kwa vile mimi sio mchumi, wachumi wetu, tusaidieni, tuelimisheni tunakwenda wapi?, are we heading to the right direction?.

Ili Tuendelee Tunahita Vitu Vinne, Vyote Tunavyo, Tumekwama Wapi?
Tulifunzwa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne,
  1. Watu-tunao
  2. Ardhi- tunayo
  3. Siasa Safi- tunayo?
  4. Uongozi bora-?
Kama vitu hivi vyote vinne tunavyo, sasa sisi Tanzania tumekosa nini?, kwa nini bado ni masikini?.

Kupanga ni kuchagua.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea.
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas ...
Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed ...
Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza ...
Uchambuzi mzuri lakini naskitika hakuna mwanataaluma yeyote atakayedhubutu kusema ukweli hasa wakihojiwa ama wakitoa chambuzi zao kwenye vyombo vya habari.
HONGera ka Pascal kwakusimamia taaluma yako
 
Wanabodi,

Hii ni thread ya swali, ambalo linatakiwa kujibiwa na wachumi wetu, Mwalimu Nyerere alituhusia "Maendeleo ya Kweli ni Maendeleo ya Watu na Sio Maendeleo ya Vitu". Wachumi wetu tusaidieni kutuelimisha, huu Uchumi wa Magufuli, Unalisaidia Taifa Kupata Maendeleo ya Watu, au Utatupatia Maendeleo ya Vitu Huku Uchumi wa Mtu Mmoja Mmoja Ukiangamia?.

Kama kawaida yetu kutumia the right to expression kuuliza, Jee awamu hii ya 5 ya rais Magufuli, inatumia falsafa gani ya kiuchumi?, jee uchumi huu wa Magufuli, unalisaidia taifa au unaliangamiza?. Kwa vile mimi sio mchumi, wachumi wetu, tusaidieni, tuelimisheni tunakwenda wapi?, are we heading to the right direction?.

Ili Tuendelee Tunahita Vitu Vinne, Vyote Tunavyo, Tumekwama Wapi?
Tulifunzwa, ili tuendelee tunahitaji vitu vinne,
  1. Watu-tunao
  2. Ardhi- tunayo
  3. Siasa Safi- tunayo?
  4. Uongozi bora-?
Kama vitu hivi vyote vinne tunavyo, sasa sisi Tanzania tumekosa nini?, kwa nini bado ni masikini?.

Kupanga ni kuchagua.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali
Rejea.
Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas ...
Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed ...
Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza ...
Uchambuzi mzuri lakini naskitika hakuna mwanataaluma yeyote atakayedhubutu kusema ukweli hasa wakihojiwa ama wakitoa chambuzi zao kwenye vyombo vya habari.
HONGera ka Pascal kwakusimamia taaluma yako
 
Lengo la Mkuu wetu ni kuona tunaishi kama mashetani......sasa akiboresha uchumi wa watu si tutaanza kuishi kama Malaika kinyume kabisa na malengo yake.?

Hapa tusubiri siku akibadili slogani.... kwamba Mashetani tuishi kama malaika
 
Back
Top Bottom