johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,962
- 141,961
Rais wa Kenya mh Uhuru jana aliwaomba msamaha wakenya wote kwa sintofahamu ya kisiasa iliyojitokeza baada ya uchaguzi. Aidha amewataka wakenya wote kuwa wamoja na kuifanya nchi ya Kenya kuwa bora zaidi.
Ndipo sasa najiuliza, Lowassa ambaye pia ni rafiki mkubwa wa Kenyata hapaswi kufanya vivyo hivyo kwa watanzania.
Ni Lowassa aliyezusha taharuki CCM kwa kutaka kulazimisha ateuliwe kuwa mgombea urais 2015 hali iliyopelekea 75% ya wanec waimbe kuwa wana imani naye.
Ni Lowassa huyu huyu baada ya mikakati yake kubuma kule CCM akakimbilia CHADEMA ambako amesambaratisha kile kilichoitwa UKAWA na sasa ameielekeza CHADEMA kibra.
Kiukweli siasa za Tanzania zimevurugika kabisa sababu ya wafuasi wa mtu huyu, Je, Lowassa hapaswi sasa kuwaomba radhi watanzania na kushiriki kikamilifu katika kuijenga Tanzania mpya yenye uchumi wa viwanda?...Ahsante!
Ndipo sasa najiuliza, Lowassa ambaye pia ni rafiki mkubwa wa Kenyata hapaswi kufanya vivyo hivyo kwa watanzania.
Ni Lowassa aliyezusha taharuki CCM kwa kutaka kulazimisha ateuliwe kuwa mgombea urais 2015 hali iliyopelekea 75% ya wanec waimbe kuwa wana imani naye.
Ni Lowassa huyu huyu baada ya mikakati yake kubuma kule CCM akakimbilia CHADEMA ambako amesambaratisha kile kilichoitwa UKAWA na sasa ameielekeza CHADEMA kibra.
Kiukweli siasa za Tanzania zimevurugika kabisa sababu ya wafuasi wa mtu huyu, Je, Lowassa hapaswi sasa kuwaomba radhi watanzania na kushiriki kikamilifu katika kuijenga Tanzania mpya yenye uchumi wa viwanda?...Ahsante!