Je, hii ndio maana halisi ya Tume Uhuru ya Uchaguzi?

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Watanzania tumekuwa tukililia sana kuwa na Tume huru ya Uchaguzi. Hivi majuzi Kenya wamefanya uchaguzi wao na karibu asilimia kubwa tumewapongeza kwa kufanya uchaguzi wa wazi kabisa na kushirikisha vyombo vya habari kwa kila hatua

Wengi wameipongeza Tume iliyosimamia uchaguzi huo. Hata hivyo tumeshuhudia dakika za mwisho kabisa tume hiyo hiyo ikigawanyika

Makamu mwenyekiti ametofautiana na Boss wake hadharani jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi kwasababu huu mgawanyiko utaenda hadi kwa mashabiki na wafuasi wa wagombea

Kitendo hiki kimenifikirisha sana. Najiuliza, hii ndo definition sahihi ya kuwa na Tume huru!?

Hivi inawezekana kumbe tukawa na Tume huru halafu ndani yake kukawa na viongozi au wajumbe huru kupita hata tume yenyewe!?

Muhimu ni kuwa na Tume huru au watu huru ndani ya tume!?

Kuwa na Tume huru Kuna maanisha watu ndani ya tume wafanye chochote muda wowote au wanatakiwa waifuate tume muda wote?

Hivi tume huru hasa ni ipi!?

Kama ni ile isiyoweza kuingiliwa na wanasiasa katika maamuzi, hii ya Kenya tuna uhakika gani huyu makamu mwenyekiti na hao wajumbe walio kana matokeo kabla hata hayajatangazwa hawana shinikizo la wanasiasa nyuma ya pazia!?

Mwenyekiti kushindwa kuzuia wajumbe wake wasigawanyike, tuamini kuwa ndo Uhuru wenyewe wa tume au tuamini yeye ndo alikuwa imara kukataa mashinikizo ya wanasiasa?

Kwa mfano hao waliogawanyika na kukana matokeo bila kutoa sababu zaidi ya kusema "wasihusishwe na hayo matokeo" baadae wakawa chanzo cha vurugu na machafuko tuamini ndo Uhuru wenyewe wa Tume?

Mwisho kabisa, nawaombea wakenya wote wayapokee matokeo na wadumishe amani! Wakiliweza hilo hakika dunia nzima itajifunza kwao.

UHURU KENYATTA atabaki kuwa nyota wa mchezo kwa kuamua matokeo kijasusi zaidi maana kibongo bongo mgombea hata wa udiwani tu aungwe mkono na Rais halafu tume isimtangaze nyasi zingechimbika kuanzia kwa mgambo kupiga virugu hadi mwenyekiti kuambiwa hajulikani alipo na amevamiwa na watu wasiojulikana.

Wakenya wakibaki na amani yao Uhuru Kenyatta atakuwa amepindua meza ya kijasusi kibabe na Odinga atakuja kushituka baadae kabisa huu mchezo uliochezwa kijasusi.
 
Hizo ni siasa tume inaangalia Fact, hahaa wale waliteuliwa na Uhuru na wanajua wanacho kifanya, Bahati mbaya wame fanya timing mbaya sana pia Raila alingoja kuona reaction ya Raia ila raia wametulia tuli
Wakenya sio wajinga kama Watanzania, huu ujinga tunao sisi, Wakenya wana akili sana wana Exposure kubwa sana kuwadanganya unahitaji kufanya kazi ya ziada.
Watanzani unaweza danganya hadi Proffesor
 
Hili nimeliona yes kuwa ni tatizo kubwa.

Najiuliza kuna nini cha kujifunza Kenya?

State Heist?
Tume ni huru, na ndio maana kuna transparent ya kutisha, wale Makamishina kwanza waliteuliwa Dakika za mwisho na pia kuangusha Familia tatu ni kazi ngumu sana.

Hawana impact na uzuri Wakenya wanajua mchezo ulivyo, Watanzania ndo hatujui move ilivyo make hizo akili za kujua hatuna.
 
Wale makamishina waliteuliwa ndio utaratibu ulivyo ila Mwenyejiti huwa anatafutwa inatanganzwa nafasi ya kazi.

Kwa mjibu wa sheria za uchaguzi kenya mwenye mamlaka ya kutangaza mshindi ni mwenyekiti, na kafanya hivyo.

Hivi sisi Wabongo tusha ingia kwenye portal ya tume ya Kenya tukajumlisha matokeo?

Hahaaa yaani ile transparent yao imeleta kiwewe kwa Big Familly wakina Uhuru Kenyata

Mipango ya Kenyata ilikuwa ni baadae arudi tena madarakani baada ya miaka 5 sasa inaonekana mpango wake umekufa rasimi
 
Na hakuna Mkenya anataka kusikia story za machafuko wala nini, wamechoka sasa wanataka kufanya kazi, Kwa kifupi imetoka
 
Wale makamishina waliteuliwa ndio utaratibu ulivyo ila Mwenyejiti huwa anatafutwa inatanganzwa nafasi ya kazi.

Kwa mjibu wa sheria za uchaguzi kenya mwenye mamlaka ya kutangaza mshindi ni mwenyekiti, na kafanya hivyo.

Hivi sisi Wabongo tusha ingia kwenye portal ya tume ya Kenya tukajumlisha matokeo?

Hahaaa yaani ile transparent yao imeleta kiwewe kwa Big Familly wakina Uhuru Kenyata

Mipango ya Kenyata ilikuwa ni baadae arudi tena madarakani baada ya miaka 5 sasa inaonekana mpango wake umekufa rasimi
Sikulifahamu hili, kumbe yule makamu mwenyekiti na wajumbe waliojitenga ni zao la uteuzi wa Kenyatta!

Hata ikiwa hivyo, Kama sheria za tume ziko kimya kwa aina ya watu hao bado sio sahihi maana wanaweza kuitia nchi kwenye machafuko muda wowote.

Nadhani tume ili kuwa huru zaidi na kuwa sehemu ya kudhibiti usalama wa nchi, ilitakiwa iweke utaratibu mgumu kwa watu Kama hao (wanaopingana na Mwenyekiti nyakati za hatari Kama hizi) ili baadae wawajibike kisheria
 
Back
Top Bottom