Je, Lembrus Mchome na Monalisa Ndala bado ni wanachama wa CHADEMA na ACT?

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
464
Reaction score
687
Lembrus Mchome na Monalisa Ndala watakumbukwa kuwa ni viongozi wa upinzani walioshirikiana na Msajili wa vyama vya siasa kuvuruga vyama vyao.

Lembrus Mchome aliishitaki CHADEMA kwa msajili, secretariat yote ya chama chake ikafukuzwa.

Kadhalika, Monalisa Ndala ameshitaki ACT kwa msajili, mgombea wao wa urais amefukuzwa.

Swali la muhimu linabaki, hivi hawa bado ni viongozi na makada wa hivi vyama walivyovishitaki? Je, bado wanaaminika na vyama vyao?
 
SWALI ZURI SANA
 
Lembrus Mchome yuko Chaumma na Ndala bado mwanachama wa ACT-WAZALENDO.

Mchome aliandamwa na kejeli na matusi. Viongozi kama Boni Yai waliunga juhudi za kumchafua. ACT-WAZALENDO wanaheshima uhuru wa mwanachama wao wa kukosoa chama chake.

Hiyo mpaka sasa ndio tofauti kati ya Chadema na ACT-WAZALENDO. Mpaka sasa maana ACT-WAZALENDO nao wanaweza kubadilika.

Amandla....
 
Lembrus Mchome, ni project ya serikali kupitia msajili wa vyama. Huyu alikuwa akilipiwa pango na msajili.....Ebu unganisheni dots.
 
Kwa mbeleko ya mlezi wa vyama bado.
 
Kosa la ACT wamekiuka makubaliano acha moto uwawakie. Mgombea Urais alikiwa ni yule mama - sasa sijui ni kiongozi gani kamleta Mpina dk ya 90.

Haya sasa wapambane na hali yao, CCM mtandao si watu - ni msiba mzito ACT na huko mahakamani wanakwenda kupoteza muda wao.
 

Mchome alitumika akidhani atafaidi. Wewe hujahudhuria Mkutano ulijuaje akidi haijatimia?. Wala CHADEMA hawakuangaika naye aliondoka mwenyewe CHADEMA. Very stupid guy. Mpo CHADEMA kama mipelelezi. Very stupid
 
Wekeni ushahidi kuwa alilipiwa panga na msajili. Mnapenda mno kuzushia watu mambo ya ovyo.

Amandla...
Tatizo hufuatilia vitu....UNAKURUPUKA TU. Haya mambo yalishawekwa wazi, kila mtu anajua, umemuuliza yeye mwenyewe kwanini alikuwa analipiwa na msajili? Haya maneno sikusema mimi......Haya maneno yapo na mwenyewe hakubisha. Mnataka ushahidi gani? Endelea kutumika na wewe, ila haina mwisho mzuri.
 
Mchome alitumika akidhani atafaidi. Wewe hujahudhuria Mkutano ulijuaje akidi haijatimia?. Wala CHADEMA hawakuangaika naye aliondoka mwenyewe CHADEMA. Very stupid guy. Mpo CHADEMA kama mipelelezi. Very stupid
Mchome alifanyiwa visa toka kwenye tawi lake. Pamekuwa na drumbeat toka mnaojiita wafuasi wa Chadema kuwa aondoke. Ameondoka lakini bado mko nae.

Unaniita stupid wakati unadhani ushahidi wa quorum ni mtu kusema "nilihudhuria na kuona quorum imetimia!" Haujui kuwa kinachoangaliwa ni attendance register ambayo kama kweli palikuwa na quorum ingetolewa kama ushahidi. Kushindwa kuitoa ni dalili ya uzembe au kuwa kweli hapakuwa na quorum.

Nimekuvumilia sana lakini hili la kuniita stupid ni beyond the pale. Nakuweka kwenye ignore list yangu kwa hiyo usijisumbue kunijibu maana sitaona majibu yako.

Amandla...
 
Kama ushahidi upo wazi si ungeuweka? Hearsay haijawahi kuwa ushahidi.

Amandla...
 
🚮🚮🚮
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…