Je, kweli CHADEMA ni mpango wa Mungu?

Je, kweli CHADEMA ni mpango wa Mungu?

CDM ni mpango waMungu!!!! njama za mizigo kuiua kwa kutumia masalia ilibuma kwa uwezo wake mola!
 
CDM ni mpango waMungu!!!! njama za mizigo kuiua kwa kutumia masalia ilibuma kwa uwezo wake mola!

Mada hii haihitaji blablaa; ina maswali ya msingi ambayo ni haya hapa: je, kauli hii ilitoka kwa nani, kwenda kwa nani, kwa namna/ njia ipi,lini, wapi, na kwa maudhui yapi? mbona vijana wa cdm gongo imekuwa tatizo sana?toa majibu acha longolongo na ulaghai kibao.
 
Chadenma ni kweli mpango wa Mungu, kama rais wa nchi anashia kusema uvumilivu unamwishio wake jibuni mapigo na anashindwa kutumia vyombo vya kiusalama kudhibiti vurugu basi ujue nchi hiyo imelaaniwa, kwa kifupi fuatilia kifo cha mwangosi, tukio la Ulimboka, bomu la Arusha, mpka leo hii Rais kashindwa kuunda tume ili kupata ukweli anabaki kuimba taarabu hii ni aibu ya kiasi gani? tuna baki kubishana upuuzi...bahati nzuri Nchi hii ni nchi ya iliyo jaa watu wenye akili fupi!

kama kweli kwa maelezo yote hayo bado hujajibu hata kpengele ki1 kuna hatari kubwa sio tu kwa cdm bali kwa jamii/taifa! Na maneno yako mengi yasiyojibu hoja iliyopo mezani inadhihirisha wazi kuwa ww naye una akili fu.. kama ulivyosema mwenyewe
 
Sio la kuuliza hilo, ni kweli CDM mpango wa Mungu.
1. Mpango wa kuhiujumu chadema kanda ya ziwa uliwekwa hapa mwanzoni mwa mwezi januari wajinga kama wewe mliuponda sana mwisho wa siku kilichotokea shinyanga umekiona,kama si mpango wa Mungu kwanini haya tuliyajua kabla.
2. Ugaidi wa kizushi wa Lwakatare, leo fuatilia wale wote waliokua nyuma ya pazia kama Msacky, zzk n.k wako wapi katika nafasi zao = mpango wa Mungu
3. Bomu la Soweto kuwalenga Mbowe na Lema lakini Mungu kawanusuru
4. Kesi mbalimbali zinazofunguliwa na Policcm, serikali na CCM mwisho wanaumbuka wao= mpango wa Mungu
5. Propaganda chafu zinazofanywa na Ccm, Tiss kama udini,ukanda,fujo, ili kuiua Cdm bado zinafeli= mpango wa Mungu
6. Nguvu kubwa inayofanywa na dola,bunge,tiss,policcm,tbccm, uhuru,mzalendo eti kuivuruga cdm tena kwa kununua makada wa CDM lakini hawafanikiwi,wakifanikiwa tayari washagundulika Mpango wa Mungu

Ndio maana mnafeli mitihani! Sasa hapa umejbu kipengele gani cha swali? Aibu Kubwa!
 
Exactly majibu hayo hapo.Usiulize tena we bwana mdogo

kwa akili yako hiyo unafikir ametaja source/sender na receiver wa kauli kuwa `cdm ni mpango wa mungu'? je ametaja muda na mazingira ambapo kauli hii ilitolewa? je amesema njia ( channel) iliyotumika? mbona vijana wa cdm mmelala usingizi wa gongo ya babu yenu slaa?! zinduka utumie bongo kufkir na siyo '---- kama lema
 
Nianze kwa kutaja maslahi yangu ndani ya CDM,mimi ni mwanachama hai wa CDM ambaye kwa vipindi tofautitofauti nimekuwa kiongozi wa CDM katika ngazi mbalimbali kama makamu mwenyekiti wa CDM tawi la chuo kikuu SAUT pia naibu katibu,nikiwa nimejiunga na CDM mwaka 2009 hivyo nakifahamu chama changu japo kwa ufupi kuanzia sera zake,itikadi na falisafa yake bila kusahau historia muhimu ya chama chetu na changamoto zake mpaka kilipofika sasa kuwa chama kikuu cha upinzani tena chenye nguvu za kuwanyima raha na usingizi magamba wa CCM na serikali yake kwa ujumla,mbali na hivyo kama mwananchi mzalendo wa TZ niliyechoshwa na Mavuno madogo ya kiuchumi,kisiasa na kijamii kwa miaka 50 ya uhuru wa bendera na Muungano wenye malalamiko yasiyoisha.
Tangu chama hiki kiasisiwe zaidi ya miaka 20 iliyopita kimepitia mengi na kuona mengi kama mwanamke mgumba,kuanzia hali ngumu ya kisiasa walipokuwa na mafanikio madogo ya kisiasa mpaka sasa kikiwa chama cha pili kwa kuwa na wabunge wengi bungeni,CDM kwa sasa imekomaa na ipo tayari kuongoza nchi hii kwa miaka mingine 100 ukiacha mapungufu madogo madogo ya kimfumo,kiutendaji na ya viongozi wachache ambao wana udhaifu wa kibinadamu.
Lakini pamoja na mambo yote hayo lazima tukili wazi kwamba bila mkono wa Mungu kuwa juu ya CDM pengine leo hii nisingekuwa naandika haya kuihusu,imepita kwenye mabonde na milima,mito na maziwa,miba na tambalale,kuhusu migogoro ni kweli ina athari zake bt zisitufanye turudi nyuma makamanda tusonge mbele,askari mmoja akifa mkiwa mstari wa mbele vitani unaruka maiti yake na kuendeleza mapambano,migogoro ni chanzo cha maendeleo kwa mujibu ya wanafalisafa na ni kielezo cha ukuaji wa demokrasia ndani ya chama,kwa vipindi viwili 1995 -2000 CDM haikusimamisha wagombea urais sio kwamba hawakuwa na watu wenye sifa hizo la hasha bali ni kutokana na mgogoro wa nani amwachie nafasi mwenzake kati ya mwasisi wetu Edwin Mtei na mwasisi mwenzake Bob Makani,bt mgogoro huo ulipita na ukaisha huku ukikiacha chama salama na chenye umoja na mshikamano,hapa si kwa uwezo wa binadamu pekee bali ni kwa uwezo wa Mungu pekee.

Kuna matukio mengi ambayo yamekikumba chama hiki ama yangekiua ama kukijenga mfano mzuri ni issue ya kesi za UGAIDI zilizokuwa zinaratibiwa na Mwigulu Njemba kwa kusaidiwa na watu wa UWT na baadhi ya viongozi wa CDM wasiowaaminifu kwa chama na watanzania kwa ujumla,kuanzia ile ya Rwakatale mpaka ile ya kamanda Kileo zote hizo kwa uwezo wa kibinadamu hasa kwa kuzingatia tupo katika nchi ya UFISADISTANI isingekuwa rahisi kwa majaji kutenda haki na haki hiyo ikaonekana kweli imetendeka,Turudi katika matukio ya mabomu kwenye mikutano ya CDM kuanzia Soweto Arusha na kule Iringa alipofariki Mwangosi(R.I.P)ni ukweli kwamba matukioa hayo hayakuwa yakitokea kwa bahati mbaya bali yalikuwa yakitokea kwa kuratibiwa na watu maalumu wenye kazi maalumu,utapambana vipi kukitoa chama dola kwenye nchi zisizo heshimu demokrasia kama hii,ukabaki salama?hapa lazima mwenyezi Mungu mwingi wa rehema alikuwa pamoja nasi wanaCDM na wananchi wanyonge wenye kuiona CDM kama mkombozi pekee na wa kweli aliyebaki la sivyo msajili angeifta CDM kama ilivyokuwa imepangwa,hakika Mungu utukuzwe,kumbuka matukio ya vifo kwenye maandamno ya CDM Arusha,M4C Morogoro,Singida na kwinginepo japo tunasema kazi yake Mola haina makosa bt kwa matukio yale ile ilikuwa kazi ya Polisi Tz kwa kushirikiana na MACCM,matukio hayo yote yamedhihilisha kwa namna gani Mungu anasiapoti CDM na kuwaongoza vema viongozi wa CDM,Kwani kwa jinsi matukio hayo yote yalivyokuwa yameratibiwa kiufundi na kiustadi aidha yangewavunja moyo wafuasi na wanachama wa CDM nchi nzima ama chama kingefutwa lakini Mungu wetu ailiyehai ameendelea kuwa nasi,
Matukio mengine yanayoelezea uwepo wa Mungu ndani ya chama hiki kikuu cha upinzani nchini ni pamoja na Tukio la aliye kuwa mwenyekiti wa CDM Arusha bwana Samsoni Mwigamba kukamatwa na waraka wa siri uliokuwa umelenga kukiangamiza chama kwa namna mbalimbali,nikitafakari tukio hilo nauona uwepo wa Mungu ndani ya CDM dhahili shahili,hebu we jiulize sikuzote Mwigamba anaitumia Laptop yake kupost mambo mbalimbali yakiwemo ya kukiumiza chama kwenye mitandao ya kijamii akitumia jina la Mkulima Maskini na hakuwa akikamatwa wala kuhisiwa,kama sio nguvu ya Mungu iweje hiyo siku tena akiwa kwenye kikao na viongozi wa Kanda wa CDM apost JF mambo ya kukichafua chama na viongozi wake then Saini ya PC yake itokee kwenye mtandao kama si Mungu basi huyu ni nani aliyeliwezesha hili?hebu tizama tukio zima la kupekuliwa kwa PC ya Mwigamba kulivyoibua waraka wa usaliti na mapinduzi makubwa!tafakali bila Mwigamba kukamatwa na waraka ule leo hii still yeye na kundi lake laililojaa tamaa ya madaraka kina Zitto Kabwe,Mkumbo na viongozi kadhaa wa mikoa na wilaya still wangekuwa wanatembea vifua mbele na kujifanya wafia chama wa kufa mtu.Mungu yupo na anaisimamia CHADEMA kwa kila hatua,angalia wimbi la wafuasi nchi nzima lilivyopolomokakuwafuata viongozi wa usaliti?mgogoro huo ukaisaidia CDM kutambua nani ni mwanachama wa CHADEMA na kina nani ni wafuasi wa wasaliti,chama kinasonga mbele PAMOJA DAIMA,Jambo lingine linalotuonesha uwepo wa Mungu ni kuwapo kwa serikali dhaifu yenye kufanya makosa yanayojirudia kila mara,hali inayopelekea mabalaza ya mawaziri kuvunjwa mara kwa mara na kuipatia CDM hoja za kuongea mbele ya wananchi,angalia CCM inavyoshindwa kuisimamia serikali na kuruhusu mianya ya ufisadi kiasi cha kuiumiza nchi,tizma issue za ufisadi wa Richmond,EPA,mgogoro wa gesi kule Mtwara,kumbuka visa vya kusikitisha vya Operation Tokomeza Ujangiri,jinsi Twiga na wanyama wengine wanavyotoroshwa nchini huku vyombo vya ulinzi vikiwa vimelala fofo,ukosefu wa dawa mahospitalini na huduma zingine za kijamii yote haya hayatokei bahati mbaya bali na Mwenyezi Mungu anawatia upofu viongozi wa CCM na serikali yao na maadui wengine wa CHADEMA ili kuwafumbua macho wananchi waone maovu ya CCM,Hata huu mtindo mpya wa CCM kurithishana madaraka kifalme ama kisultani nahisi ni mpango wa Mungu kuwazindua watanzania na ni ujumbe kwao kwamba CCM haiwezi kuwaletea maendeleo tena.
Nimalizie kwa kuwatia moyo makamanda wa CDM na viongozi wetu nchi nzima kwamba wasikatishwe tamaa na matokeo ya chaguzi mbalimbali zinazoendelea na chama kufanya vibaya kwani ADUI wetu kakazana sana kuwavunja moyo na kuwaogopesha,hivyo mkirudi nyuma na kukata tamaa mtampa kiburi kipya cha kuendelea kututunyanyasa watanzania,tuendelee kuiunga mkono CDM na viongozi wake,tuendelee kupambana na mifumo mibovu popte pale tulipo na tutoe elimu ya uraia nchi nzima mabadiliko soi chmvi useme yanashika haraka bali ni process ya taratibu yenye hatua,baba wa taifa hayati Julias Nyerere alishapata kusema nyakati flani kwamba "Ili taifa liendelee linapaswa kuwa na vijana wabishi na waasi wa mfumo wowote kandamizi"

Niandikie
kilunganicholaus@yahoo.com
0754-926271,0715926271
Kibondo Kigoma Tanzania
 
Kiongozi hebu jaribu kufanya "edit" kwenye andiko lako ili iwe rahisi kulisoma na pengine kuelewa ulichokusudia kuandika. Pamoja na mambo mengine, zingatia matumizi ya Herufi kubwa na herufi ndogo; kuacha nafasi baada ya Kituo Kikubwa au kidogo na kuacha nafasi kati ya neno na neno.

Ninatumaini ulipoandika "Mwigulu Njemba" ulitaka kumaanisha "Mwigulu Nchemba" na ulipoandika "... hayati baba wa taifa Julias nyerere alishapata ..." ulitaka kumaanisha "... Hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere, alikwishapata ..."

Pamoja na yote haya, ninakiheshimu sana Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT)!
 
CHADEMA Wanamtanguliza Mungu Katika Shughuli Zao, Hii Huwa Inaonekana Katika Mikutano Yao Wakiwa Wanafanya Maombi Kabla Na Baada Ya Mikutano.

Kauli Zao Kama "Tulianza Na Mungu Tunamaliza Na Mungu" Na "Sauti Ya Umma Ni Sauti Ya Mungu" Ni Baadhi Ya Ushahidi Kwamba CHADEMA Wanamtanguliza Mungu Mbele.

Mungu Nae Kwa Vile Yeye Siyo Athumani Wala John Ameonekana Akikisaidi Chama Kuvuka Bahari Ya Shamu Na Jangwani Kama Wana Wa Israeli, Kwani CHADEMA Inapitia Misukosuko Mingi Kama Ya "Ugaidi", "Mauaji Ya Dkt Slaa" Na Mengine Mengi.

Lakin Wengne Wamefika Mbali Kuitabilia Kifo Kabla Ya Mda Flani Kwani Walikua Na Uhakika Kulingana Na Mikakati Waliyokuwa Wameweka.

Kwa Wenzangu CCM Sionagi Sehemu Wanapomtanguliza Mungu Zaidi Ya "Kitambi Mbele" Yaani Ufisadi Kama Inavyoonekana Alama Yako Ya Mkono Na Dolegumba.Vile Vile Wanatanguliza "Nyundo" Ya Kuwaponda Na Kuwakandamiza Watanzania.

Kweli CHADEMA Ni Mpango Wa Mungu, Kama Musa Na Wana Wa Israeli.

Mimi Sina Chama, Huo Ni Mtazamo Wangu.
 
Wao wanaamini waganga zaidi,siku hizi wanakuja na fisi katika mikutano yao.Mungu ibariki CHADEMA
 
hivi chadema hawa wapenzi wenu mmewalisha nini? almost all hawajielewi ni kama mazombie
 
Mashabiki ya CCM ndio Mazombi. Leo yanamponda Lowasa kesho yanamshabikia. Muulize Nape alisema Lowasa ni Gamba juz kaenda Arusha anasema Lowasa ni Jembe na ni Mchapa kazi hakuna Mfano. CCm hamueleweki. Ni km Nyoka ndumila kuwili.
 
MUNGU wa kweli atawaonyesha chdm majibu ya dhambi wanazoendelea nazo Oct
 
Back
Top Bottom