Je! Kuvuta Sigara ni Dhambi?

Je! Kuvuta Sigara ni Dhambi?

Itoye

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2017
Posts
531
Reaction score
1,026
Wakuu Salaam.

Naamini mko salama, na kwa wale mliopata nafasi ya kuhudhuria ibada ni matumaini yangu mmekuwa na ibada njema.

Moja kwa moja kwenye swali langu, Je! Kuvuta sigara ni dhambi?

Naomba ku - declare interest kuwa binafsi si mvutaji wa sigara na sina mpango wa kuwa mtumiaji, lengo la uzi huu ni kutaka kuongeza ufahamu na uelewa.

Kwa muda nimekua nikisikia watu mbalimbali wanapokuwa wakitoa hotuba za mahubiri na hata leo nimelisikia tena waki-categories uvutaji wa sigara kama mojawapo ya dhambi, ingawa ni kweli uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya lakini Biblia haitaji wazi kuwa uvutaji wa sigara ni dhambi kama ilivyotaja wazi kwa mfano uzinzi, uasherati, wizi, ufisadi, ufiraji nk nk nk kuwa ni dhambi na viko vifungu ktk Biblia vinaeleza hilo kwa uwazi kabisa.

Naomba kwa wataalamu wa maandiko walioko humu wanisaidie kufahamu ni sehemu gani ktk Biblia imeandikwa uvutaji wa sigara ni dhambi au hawa wanao - categories uvutaji wa sigara kama mojawapo ya dhambi wanatumia maandiko yapi na kwa nini.

Thanks in advance kwa elimu nitakayoipata hapa.
 
Kwa sisi waislamu, uvutaji sigara ni haramu, kwa hiyo ni dhambi, ingawa watu watajitokeza kupinga. Ni tabia mbaya sana ambayo inachafua mazingira na ni ishara ya maporomoko ya maadili. Karibu kote duniani, uvutaji sigara hadharani imepigwa marufuku. Nairobi wavutaji sigara wametengewa maeneo maalum vya kuvuta sigara, kuvuta barabarani ni kosa! Hapa kwetu mbona bado haijapigwa marufuku?
 
Wakuu Salaam.

Naamini mko salama, na kwa wale mliopata nafasi ya kuhudhuria ibada ni matumaini yangu mmekuwa na ibada njema.

Moja kwa moja kwenye swali langu, Je! Kuvuta sigara ni dhambi?

Naomba ku - declare interest kuwa binafsi si mvutaji wa sigara na sina mpango wa kuwa mtumiaji, lengo la uzi huu ni kutaka kuongeza ufahamu na uelewa.

Kwa muda nimekua nikisikia watu mbalimbali wanapokuwa wakitoa hotuba za mahubiri na hata leo nimelisikia tena waki-categories uvutaji wa sigara kama mojawapo ya dhambi, ingawa ni kweli uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya lakini Biblia haitaji wazi kuwa uvutaji wa sigara ni dhambi kama ilivyotaja wazi kwa mfano uzinzi, uasherati, wizi, ufisadi, ufiraji nk nk nk kuwa ni dhambi na viko vifungu ktk Biblia vinaeleza hilo kwa uwazi kabisa.

Naomba kwa wataalamu wa maandiko walioko humu wanisaidie kufahamu ni sehemu gani ktk Biblia imeandikwa uvutaji wa sigara ni dhambi au hawa wanao - categories uvutaji wa sigara kama mojawapo ya dhambi wanatumia maandiko yapi na kwa nini.

Thanks in advance kwa elimu nitakayoipata hapa.
Nani kasema dhambi? au nani kasema si dhambi? nasubir kujifunza
 
Uvutaji wa Sigara ni Dhambi kwakuwa.
1. Ni madawa ya kulevya
2. Haina faida yoyote kwa afya ya mwili wako.
3. Ina haribu Afya ya mwili wako uliotengenezwa kwa thamani kubwa sana.
4. Ina haribu Afya ya walio jirani yako.
5. Ina (adiction) inayokupelekea kudhohofisha akili yako ifikirie kuvuta sigara badala yawaza mambo ya maana.
6. Unakupotezea muda na kipato chako bila faida yoyote.
7. Ni Sumu kali unayokudhohofisha siku hadi siku, maisha ya wavuta sigara ni mafupi.
8. Inasababisha kushambuliwa na magonjwa hatarishi kama TB na Kansa
9. Inashawishi wengine kuiga tabia ya uvutaji ambayo haina faida yoyote.
10, Inakuchafua kwa harufu mbaya, uchafu na kuwa kero kwa mkeo na watu wa karibu yako.
NAKADHALIKA.
 
Asante mkuu, full marks to you. Umetoa jibu tosha ambayo haina upingamizi au ubishi!

Uvutaji wa Sigara ni Dhambi kwakuwa.
1. Ni madawa ya kulevya
2. Haina faida yoyote kwa afya ya mwili wako.
3. Ina haribu Afya ya mwili wako uliotengenezwa kwa thamani kubwa sana.
4. Ina haribu Afya ya walio jirani yako.
5. Ina (adiction) inayokupelekea kudhohofisha akili yako ifikirie kuvuta sigara badala yawaza mambo ya maana.
6. Unakupotezea muda na kipato chako bila faida yoyote.
7. Ni Sumu kali unayokudhohofisha siku hadi siku, maisha ya wavuta sigara ni mafupi.
8. Inasababisha kushambuliwa na magonjwa hatarishi kama TB na Kansa
9. Inashawishi wengine kuiga tabia ya uvutaji ambayo haina faida yoyote.
10, Inakuchafua kwa harufu mbaya, uchafu na kuwa kero kwa mkeo na watu wa karibu yako.
NAKADHALIKA.
 
Uvutaji wa Sigara ni Dhambi kwakuwa.
1. Ni madawa ya kulevya
2. Haina faida yoyote kwa afya ya mwili wako.
3. Ina haribu Afya ya mwili wako uliotengenezwa kwa thamani kubwa sana.
4. Ina haribu Afya ya walio jirani yako.
5. Ina (adiction) inayokupelekea kudhohofisha akili yako ifikirie kuvuta sigara badala yawaza mambo ya maana.
6. Unakupotezea muda na kipato chako bila faida yoyote.
7. Ni Sumu kali unayokudhohofisha siku hadi siku, maisha ya wavuta sigara ni mafupi.
8. Inasababisha kushambuliwa na magonjwa hatarishi kama TB na Kansa
9. Inashawishi wengine kuiga tabia ya uvutaji ambayo haina faida yoyote.
10, Inakuchafua kwa harufu mbaya, uchafu na kuwa kero kwa mkeo na watu wa karibu yako.
NAKADHALIKA.
Binafsi sivuti feg ila napenda harufu yake, nadhan ungeifuta namba 10, kisha watu wa dini tusome biblia kitabu cha Mwanzo 1 kuna mistari inahalalisha matumizi ya majani kama dawa na matunda kama chakula na chakula cha kila mnyama.

Je kula Nguruwe ngamia sungura kambare na kuvuta feg ipi ni dhambi?? Tutumie maandiko ili tuelewane maana Bible is perfect book.
 
Dhambi ni nini?
Dhambi ni

1. Kufanya jambo lisilompendeza Mwenyezi Mungu.

2.Kufanya jambo ambalo lina hatarisha hali yako au ya jirani yako.
Yaani jambo lisilokupendeza wewe au Jirani yako.
 
Kwa sisi waislamu, uvutaji sigara ni haramu, kwa hiyo ni dhambi, ingawa watu watajitokeza kupinga. Ni tabia mbaya sana ambayo inachafua mazingira na ni ishara ya maporomoko ya maadili. Karibu kote duniani, uvutaji sigara hadharani imepigwa marufuku. Nairobi wavutaji sigara wametengewa maeneo maalum vya kuvuta sigara, kuvuta barabarani ni kosa! Hapa kwetu mbona bado haijapigwa marufuku?
Shaka -Zulu heshima yako mkuu, kwa uelewa wangu sigara katika uislamu si dhambi bali makuruhu (yaani ni kama kero kwako na kwa Wengine), makuruhu ikizidi hua ni dhambi,
Kama una dalili basi leta (dalili mfano hadithi, aya, kisa n.k )
Nipo radhi kukosolewa
 
Dhambi haiwezi kuwa dhambi kama hamna Katazo/sheria! Ukivunja sheria mojawapo kati za hizi apo chini ndio unamtendea Mungu dhambi, mengine ni makatazo ya kibinadamu wakijaribu kuutawala mwili kwa ukali lakini hayaondoi tamaa za mwili.

KUTOKA 20

1 Mungu akanena maneno haya yote akasema,
2 Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
7 Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.
8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.
9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;
10 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
11 Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
13 Usiue.
14 Usizini.
15 Usiibe.
16 Usimshuhudie jirani yako uongo.
17 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng?ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.


Kama dhambi ya sigara inatokana na madhara yake kimwili, basi tuseje kuhusu mafuta ya kula yenye rehemu au nyama nyekundu tuseme na kula ivyo vitu ni dhambi kisa vinaharibu mwili?
 
Weka reference badala ya hisia. Tupe mistari.
Reference ni Biblia,
Marko 12 : 28-31

" 28 Na mmojawapo wa waandishi akafika, akawasikia wakisemezana naye, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?

29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;
30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi. "

( Usipotenda yanayompendeza Mungu na Jirani yako ni dhambi )
 
Uvutaji wa Sigara ni Dhambi kwakuwa.
1. Ni madawa ya kulevya
2. Haina faida yoyote kwa afya ya mwili wako.
3. Ina haribu Afya ya mwili wako uliotengenezwa kwa thamani kubwa sana.
4. Ina haribu Afya ya walio jirani yako.
5. Ina (adiction) inayokupelekea kudhohofisha akili yako ifikirie kuvuta sigara badala yawaza mambo ya maana.
6. Unakupotezea muda na kipato chako bila faida yoyote.
7. Ni Sumu kali unayokudhohofisha siku hadi siku, maisha ya wavuta sigara ni mafupi.
8. Inasababisha kushambuliwa na magonjwa hatarishi kama TB na Kansa
9. Inashawishi wengine kuiga tabia ya uvutaji ambayo haina faida yoyote.
10, Inakuchafua kwa harufu mbaya, uchafu na kuwa kero kwa mkeo na watu wa karibu yako.
NAKADHALIKA.
Haya ni mawazo yako tunayaheshimu ata soda aifai kiafya mkuu nayo ni dhambi?
 
Unaogopa dhambi mkuu?
Dhambi haigopwi, ila inaachwa kufanywa, kwa maslahi yako au ya jirani yako.

Je wewe utapenda kutendewa kitu usichokipenda, kwakuwa tu anayekutendea anafurahi ?

Kuna dhambi nyingine inapendeza kuifanya lakini inabidi kuiacha ili kuilinda heshima ya jirani yako.
 
Shaka -Zulu heshima yako mkuu, kwa uelewa wangu sigara katika uislamu si dhambi bali makuruhu (yaani ni kama kero kwako na kwa Wengine), makuruhu ikizidi hua ni dhambi,
Kama una dalili basi leta (dalili mfano hadithi, aya, kisa n.k )
Nipo radhi kukosolewa

Asante sana mkuu, kwa kunipa heshima! Dalili kwenye Quran tukufu si wazi kabisa, lakini kuna aya zinazotaja "shajaratul maloona" yaani mti yenye laana, na hii imetafsiriwa na baadhi ya maulema kuwa ni tumbaku. Ni kitu ambayo imejaa laana tupu - hakuna mimea ambayo inamadhara kwa binadamu kama tumbaku. Kwenye kilimo pia tumbaku inadhoofisha rutba ya ardhi na kuicha isiweze kutumika tena kwa miaka kadha! Pombe, ingawa pia ni kitu haramu na kibaya, lakini bado inamanufaa fulani kwenye mwili, mfano kuua bacteria nk., lakini tumbaku haina manufaa hata kidogo kwa binadamu. Tumbaku inazuia baraka na kuvuta balaa mmoja kwa mmoja bila fani!
 
Kwa sisi waislamu, uvutaji sigara ni haramu, kwa hiyo ni dhambi, ingawa watu watajitokeza kupinga. Ni tabia mbaya sana ambayo inachafua mazingira na ni ishara ya maporomoko ya maadili. Karibu kote duniani, uvutaji sigara hadharani imepigwa marufuku. Nairobi wavutaji sigara wametengewa maeneo maalum vya kuvuta sigara, kuvuta barabarani ni kosa! Hapa kwetu mbona bado haijapigwa marufuku?
Mkuu naomba nitofautiane na wewe. Kati Uislam sigara haipo kwenye uharamu. Sigara ipo kwenye MAKRUHU

Makruhu ni jambo ambalo ni bora au vizuri ukaliacha lakini utakapolifanya hupati dhambi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom