Je kuna ukweli katika hii dhana?

Je kuna ukweli katika hii dhana?

CharmingLady

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2012
Posts
18,304
Reaction score
12,997
Habari za mchana mabibi na Mabwana,

Kuna dhana moja imeeneza miongoni mwa jamii zetu kuwa "Wacha tufanye mapenzi kiholela mpaka hapo tutakapoingia kwenye ndoa, ili tukishaingia tutulie" dhana hii husemwa sana na wanaume.

Kuna rafiki zangu kadhaa nilisikia wakisema hivyo.

Wazee mliopo humu mmewahi kusikia huu msemo na je unafanya kazi? Wale wanandoa wa sasa je mliwahi kupitia katika hali hii?

Mie nafikiri iwapo mtu atashindwa kutulia katika mahusiano ya awali (BF & GF) ndivyo hivyo atakavvyoshindwa kutulia katika ndoa.
Je kuna ukweli wowote katika hili?

Karibuni akina Babu Dark City, Babu Asprin, Mzee Mtambuzi, Ankal Kaizer, Kaka HorsePower na wadau wooooteeee!!!!
 
Tabia za kuendekeza huishia kuwa kama NGOZI .... inakomaa na kuzeeka na wewe mwanzo mwisho.
Kwani kuna Teja aliyewahi kufikiri ataishia kuwa alivyo sasa wakati anaanza kutejeka? (kujaribu jaribu madawa)
Kwani kuna mwizi anayeamini safari anayoenda kuiba sio ya mwisho (anasema safari ijayo huenda nitakamatwa hii moja ya mwisho) lakini anaiba mwana nenda rudi.

Walio ndani ya ndoa unafikiri wakati wanaacha njia kuu walifikiri wataishia kuwa wateja wa kudumu njia za vumbi? shits just happens

Nachotaka kusema na ambacho nimekuwa nawaambia jamaa zangu.... UTAKAVYO KUISHI KESHO ISHI SASA ILI KESHO IJENGEKE KWENYE MSINGI HUU WA LEO'' vinginevyo usipoweka msingi imara sasa, nyumba yako itayumba yumba sana kesho.
 
Mjukuu charminglady unantafuta nakuambia. Ndo nshasema hivyo.

Mi babu yako kabla sijamuoa bibi yenu nlikuwa nabadilisha vimwana kama mboga. Baada ya kuoa, mwanzoni niliendeleza libeneke. Kalivozaliwa kamalkia kangu Matesha nikatulia tuli na familia. Nitake tena za nini wakati nshajionea za kutosha zenye ladha mbalimbali?

Mpaka sasa babu yenu nimetulia. Labda itokee tu walah.

Kuamua kutulia hakuna uhusiano wowote na tabia za awali. Jasiri haachi asili. Mwanaume kitombi, Mungu labda amtie umaskini tu. Akiwa na mahela atawabadilisha kila siku, hata kama ana wake wanne.

Ila usisahau, mwanaume hajaumbwa kwa ajili ya mwanamke mmoja. Usije ukajidanganya mmeo ni wako peke yako. Tunatofautiana kwenye usiri na idadi ya wanawake wa nje tunaowalabua.

Sijaandika mimi, nimekopi na kupesti toka blogu flani ya Sudani ya Kusini
 
Last edited by a moderator:
swali la msingi kabla sijatoa msimamo wangu kwanini hujamualika C6 ??
 
Last edited by a moderator:
Tabia za kuendekeza huishia kuwa kama NGOZI .... inakomaa na kuzeeka na wewe mwanzo mwisho.

Nachotaka kusema na ambacho nimekuwa nawaambia jamaa zangu.... UTAKAVYO KUISHI KESHO ISHI SASA ILI KESHO IJENGEKE KWENYE MSINGI HUU WA LEO'' vinginevyo usipoweka msingi imara sasa, nyumba yako itayumba yumba sana kesho.
Nimependezwa na mtazamo wako ni kweli kabisa huwezi kuacha tabia chafu baada ya kuoa/kuolewa wanasema jasiri haachi asili. Kama mtu si mwaminifu hata kipindi cha gf na bf , huyo nafsi yake ilishakufa haiwezi kufufuka wakati wa ndoa so be careful kama bf/gf anacheat.
 
Habari za mchana mabibi na Mabwana,

Kuna dhana moja imeeneza miongoni mwa jamii zetu kuwa “Wacha tufanye mapenzi kiholela mpaka hapo tutakapoingia kwenye ndoa, ili tukishaingia tutulie” dhana hii husemwa sana na wanaume.

Kuna rafiki zangu kadhaa nilisikia wakisema hivyo.

Wazee mliopo humu mmewahi kusikia huu msemo na je unafanya kazi? Wale wanandoa wa sasa je mliwahi kupitia katika hali hii?

Mie nafikiri iwapo mtu atashindwa kutulia katika mahusiano ya awali (BF & GF) ndivyo hivyo atakavvyoshindwa kutulia katika ndoa.
Je kuna ukweli wowote katika hili?

Karibuni akina Babu Dark City, Babu Asprin, Mzee Mtambuzi, Ankal Kaizer, Kaka HorsePower na wadau wooooteeee!!!!

kwan vp unataka na ww uanze kungonoka?? Ili baadaye utulie?
 
Tabia za kuendekeza huishia kuwa kama NGOZI .... inakomaa na kuzeeka na wewe mwanzo mwisho.
Kwani kuna Teja aliyewahi kufikiri ataishia kuwa alivyo sasa wakati anaanza kutejeka? (kujaribu jaribu madawa)
Kwani kuna mwizi anayeamini safari anayoenda kuiba sio ya mwisho (anasema safari ijayo huenda nitakamatwa hii moja ya mwisho) lakini anaiba mwana nenda rudi.

Walio ndani ya ndoa unafikiri wakati wanaacha njia kuu walifikiri wataishia kuwa wateja wa kudumu njia za vumbi? shits just happens

Nachotaka kusema na ambacho nimekuwa nawaambia jamaa zangu.... UTAKAVYO KUISHI KESHO ISHI SASA ILI KESHO IJENGEKE KWENYE MSINGI HUU WA LEO'' vinginevyo usipoweka msingi imara sasa, nyumba yako itayumba yumba sana kesho.

TAKAVYO KUISHI KESHO ISHI SASA ILI KESHO IJENGEKE KWENYE MSINGI HUU WA LEO'' bi mdogo, hili ndiyo jibu sahihi. Inategemea unabahave vipi.
 
Karibu sana Dada Ablessed

Uko sahihi kabisa. Mtu anapozoea kitu kinakua ni sehemu yake..... Na kibaya hata nafsi yako inakuwa huru na hiko kitu na unaweza hata kupigana kukitetea. Hadi itokee hali ikufanye ujirudi au mtu akufanye ujirudi na ukubali hicho kitu sio sehemu yako.. vinginevyo sahau.... labda umuulize mlevi yeyote kwa nini analewa hicho anacholewea... atakua na sababu laki nane kwa nini analewa (madawa/pombe kali etc) na anakuona kama wewe ni mshamba hivi kutokulewa. (yupo kwenye ulimwengu wake)

Mwambie mtu una labda mwaka hujafanya ngono.. atabisha hadi kesho kutwa... kwa sababu ameshaiaminisha haiwezekani kuishi hivyo.

Mwambie mtu toka uolewe hujawahi kutoka nje ya ndoa... atakubishia hadi karne ijayo... kwa nini.. kwa sababu ameshajiaminisha na kuweka akili hivyo....

Stay safe.. dont try this at home
Nimependezwa na mtazamo wako ni kweli kabisa huwezi kuacha tabia chafu baada ya kuoa/kuolewa wanasema jasiri haachi asili. Kama mtu si mwaminifu hata kipindi cha gf na bf , huyo nafsi yake ilishakufa haiwezi kufufuka wakati wa ndoa so be careful kama bf/gf anacheat.
 
Kuna mambo yanachangia mtu kuwa kicheche
Kwa machache ni haya

Umri

Umaskini

Ujinga

Kutojitambua

Kutokuwa na majukumu

Hilo la kutokuwa na majukumu linawafanya wengi sana kujiingiza kwenye ngono

Hebu fikiria kama una mipango ya kujenga
Watoto wanasubiri karo [kama wapo]
Unahitaji mkuboresha biashara yako [kama ipo]
Unahitaji kuongeza elimu [kama bado unahitaji kusoma]
N.k

Hivi hayo yote yawe kichwani mwa mtu utawaza kwenda kumvua Mwajuma kyupi kweli?
Hivi yote hayo yawe kichwani utawaza kwenda kumvua Hamisi kyupi kweli?

Kama mtu ni kicheche ni kicheche tu na kuna mengi sana huchangia

Kusingizia kutokuwepo kwenye ndoa ni kujidanganya!!
 
Mjukuu charminglady unantafuta nakuambia. Ndo nshasema hivyo.

Mi babu yako kabla sijamuoa bibi yenu nlikuwa nabadilisha vimwana kama mboga. Baada ya kuoa, mwanzoni niliendeleza libeneke. Kalivozaliwa kamalkia kangu Matesha nikatulia tuli na familia. Nitake tena za nini wakati nshajionea za kutosha zenye ladha mbalimbali?

Mpaka sasa babu yenu nimetulia. Labda itokee tu walah.

Kuamua kutulia hakuna uhusiano wowote na tabia za awali. Jasiri haachi asili. Mwanaume kitombi, Mungu labda amtie umaskini tu. Akiwa na mahela atawabadilisha kila siku, hata kama ana wake wanne.

Ila usisahau, mwanaume hajaumbwa kwa ajili ya mwanamke mmoja. Usije ukajidanganya mmeo ni wako peke yako. Tunatofautiana kwenye usiri na idadi ya wanawake wa nje tunaowalabua.

Sijaandika mimi, nimekopi na kupesti toka blogu flani ya Sudani ya Kusini

Hapo kny nyekundu tukisema na mwanamke hajaumbwa kwaajili ya mwanaume mmoja unakubali na usijidanganye mkeo ni wako peke yako unakubali???
 
Inategemea na mtu kwa mtu, kuna watakaotulia watakapokuwa kwenye ndoa baada ya kumaliza/kufanya starehe kabla ya kuingia maisha ya ndoa, na kuna watakaoendelea hata wakiwa ndani ya ndoa. Kundi la pili tunaweza kusema - kwao ishakuwa kilevi/uteja

Na hali hii ipo hata kwa hao wanaojiita mashehe, wenyewe utawasikia kila kitu haramu, kumbe nyuma ya pazia hawafai hata kidogo, ni bora mtu anaejulikana amepotea, kuliko wale waliopo kwenye njia iliyonyooka machoni mwa watu, kumbe nyuma ya pazia ni kuliko unavyowadhania
 
Hiyo dhana ipo sana na sio katika suala la ngono pekee bali hata katika madhambi mengine mathalani ulaji rushwa n.k.

Tulio wengi hatujui au husahau kuwa leo ni maandalizi ya kesho au kwa kifupi ufanyacho leo matokeo yake huonekana kesho.
 
Back
Top Bottom