THE JAGGERS
JF-Expert Member
- Apr 3, 2023
- 444
- 292
Je, kuna ukweli wowote kuhusu ndoto zinazojirudia?
Wakuu uzi huu ninaouleta kwenu unahusu mengi kuhusiana na ndoto ikiwemo ndoto za kujirudia pamoja na ndoto zengine tusizozielewa zina maana gani kwani mimi pia nasumbuliwa na ndoto za ajabu nikiwa sielewi zinahusu nini.
Katika usiku wanane usiku wa kuamkia leo nikiwa katika kitanda nimejifunika blanketi, kutokana na hali ya hewa kuwa na ubaridi katika kipindi hiki cha masika ghafla ikanijia ndoto ambayo nilishawahi kuiota na hii ni mara ya tatu.
Nikiwa katika misere yangu ya hapa na pale nikafika mahali ambapo ni karibu na nyumbani sehemu ile ilikuwa na hewa safi hii ni kutokana na uwepo wa miti mingi katika eneo hilo. Mara ghafla nikaona mti ukiwa na matunda ya malimao ila cha ajabu mti huo haukuwa mlimao. Nikatamani sana kuchuma yale malimao kwani mimi huwa napendelea sana malimao hasa hasa kwenye vyakula vyangu. Wakati najitahidi kutungua yale malimao ghafla nikasikia sauti za vicheko.
Wakuu uzi huu ninaouleta kwenu unahusu mengi kuhusiana na ndoto ikiwemo ndoto za kujirudia pamoja na ndoto zengine tusizozielewa zina maana gani kwani mimi pia nasumbuliwa na ndoto za ajabu nikiwa sielewi zinahusu nini.
Katika usiku wanane usiku wa kuamkia leo nikiwa katika kitanda nimejifunika blanketi, kutokana na hali ya hewa kuwa na ubaridi katika kipindi hiki cha masika ghafla ikanijia ndoto ambayo nilishawahi kuiota na hii ni mara ya tatu.
Nikiwa katika misere yangu ya hapa na pale nikafika mahali ambapo ni karibu na nyumbani sehemu ile ilikuwa na hewa safi hii ni kutokana na uwepo wa miti mingi katika eneo hilo. Mara ghafla nikaona mti ukiwa na matunda ya malimao ila cha ajabu mti huo haukuwa mlimao. Nikatamani sana kuchuma yale malimao kwani mimi huwa napendelea sana malimao hasa hasa kwenye vyakula vyangu. Wakati najitahidi kutungua yale malimao ghafla nikasikia sauti za vicheko.