Mohamedex121
JF-Expert Member
- Jan 27, 2022
- 1,688
- 3,142
Salam wakuu, naimani humu nyote ni wazima wa afya na mimi pia na mshukuru Mungu mzima kabisa japo harakati ngumu ila sichoki kumshukuru Mungu kwa kila hali.
Turudi kwenye mada jana usiku wakati nimelala kuna ndoto ikanijia na hii ni mara yangu ya kwanza kuota ndoto ya namna hii nashindwa kuelewa hii ndoto ilikuwa inaamaana gani
Iko hivi kwenye ndoto nilijiona natoka nyumbani mlangoni wakati nafunga mlango ili niende zangu nje kwa mbali nikaona mtu kavalia kanzu nyeupe cha kushangaza usoni alikuwa mweusi tii na ana macho makubwa mekundu kiasi cha kuogopesha wakati naendelea kumshangaa ghafla nikaona anaanza kunisogelea mimi nikaanza kutoa sauti za vitisho kumtishia na kumuuita wewe na nani na unataka nini.
Nikaona amesimama nami nikaanza kumsogelea na kumhoji ghafla nikamuona anaanza kukimbia nikaamua nami nianze kumkimbiza. Akawa kila akifika mahali anasimama then ananiangalia kwa nyuma kisha nikiwa karibu nae anaendelea kunikimbia.
Akafika sehemu kama kuna kona ya nyumba hivi alivyokata ile kona nami wakati naisongelea ile kona nyumba ghafla nikamuona amesimama huku ananiangalia tukakutana uso kwa uso then nikastuka usingizi.
Dah aisee kuja kustuka ilikuwa ishafika alfajiri saa 11 hivi nikashindwa kulala kabisa.
Mimi naamini katika ushirikina lakini linapokuja suala la ndoto ya namna hii nashindwa kuielewa, mwenye kujua maana ya hii ndoto anaweza kunisaidia?
Natanguliza shukurani wakuu
Turudi kwenye mada jana usiku wakati nimelala kuna ndoto ikanijia na hii ni mara yangu ya kwanza kuota ndoto ya namna hii nashindwa kuelewa hii ndoto ilikuwa inaamaana gani
Iko hivi kwenye ndoto nilijiona natoka nyumbani mlangoni wakati nafunga mlango ili niende zangu nje kwa mbali nikaona mtu kavalia kanzu nyeupe cha kushangaza usoni alikuwa mweusi tii na ana macho makubwa mekundu kiasi cha kuogopesha wakati naendelea kumshangaa ghafla nikaona anaanza kunisogelea mimi nikaanza kutoa sauti za vitisho kumtishia na kumuuita wewe na nani na unataka nini.
Nikaona amesimama nami nikaanza kumsogelea na kumhoji ghafla nikamuona anaanza kukimbia nikaamua nami nianze kumkimbiza. Akawa kila akifika mahali anasimama then ananiangalia kwa nyuma kisha nikiwa karibu nae anaendelea kunikimbia.
Akafika sehemu kama kuna kona ya nyumba hivi alivyokata ile kona nami wakati naisongelea ile kona nyumba ghafla nikamuona amesimama huku ananiangalia tukakutana uso kwa uso then nikastuka usingizi.
Dah aisee kuja kustuka ilikuwa ishafika alfajiri saa 11 hivi nikashindwa kulala kabisa.
Mimi naamini katika ushirikina lakini linapokuja suala la ndoto ya namna hii nashindwa kuielewa, mwenye kujua maana ya hii ndoto anaweza kunisaidia?
Natanguliza shukurani wakuu