OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,225
- 103,839
Hii ndoto nimetoka kuiota hivi punde saa 10 hii ya usiku.
Nimeota nipo masomoni sekondari. Baadhi ya watu niliota kuwa nao katika mazingira ya shule ni madogo tuliowahi kusoma nao mimi nikiwa Advance wao wakiwa O-Level, wengine ni mdogo wangu wa kike mtoto wa Mama Mkubwa ni mtu mzima na maisha yake. Mwingine ni jamaa yangu tulisoma naye chuo kikuu zaidi amebaki kuwa jamaa yangu sana mpaka leo. Huyu ijumaa niliwasiliana naye kupeana mitikasi maana amenizidi uwezo wa mafanikio.
Sasa pale shuleni kulitokea msiba kuna mwanafunzi alifariki. Ule msiba ulikuwa chini ya usalama wa taifa ilisemekana kuna tukio dogo kafanya ikabidi usalama wamdhibiti. Kwa hiyo pale shule palijaa usalama kila kona.
Tulikuwa tunajua aliyefariki ni dogo fulani, lakini ghafla marehemu akajifunua kwenye shuka ikawa siyo yule tuliyeambiwa,kumbe ni dogo mwingine. Tukiwa pale kwenye jeneza marehemu ananyanyuka na kuzua taharuki.
Pale pale msibani yule mdogo wangu akanipa simu yake(nimesahau alinipa ili kufanya nini). Baadae kidogo nikawa na yule jamaa yangu niliyesoma naye chuo, tukawa tunapiga stori na washikaji.
Ghafla nikashtuka toka kwenye ndoto kuchek simu ni saa 10.40 asubuhi. Nikafikiria kuandika hii ndoto. Kidogo tu nikasikia alarm ya gari nje,nikachukua upinde na mshale na panga kwenda sitting room. Kumbe kulikuwa na kibaka kafungua mlango wa gari.
Kutaka kufungua mlango kibaka akaruka fensi akakimbia. Nikatoka nje kufunga mlango na gari. Nimemsikilizia pale sebuleni, bado kimyaaa nadhani amesepa.
Hii ndoto ina maanisha nini?
Nimeota nipo masomoni sekondari. Baadhi ya watu niliota kuwa nao katika mazingira ya shule ni madogo tuliowahi kusoma nao mimi nikiwa Advance wao wakiwa O-Level, wengine ni mdogo wangu wa kike mtoto wa Mama Mkubwa ni mtu mzima na maisha yake. Mwingine ni jamaa yangu tulisoma naye chuo kikuu zaidi amebaki kuwa jamaa yangu sana mpaka leo. Huyu ijumaa niliwasiliana naye kupeana mitikasi maana amenizidi uwezo wa mafanikio.
Sasa pale shuleni kulitokea msiba kuna mwanafunzi alifariki. Ule msiba ulikuwa chini ya usalama wa taifa ilisemekana kuna tukio dogo kafanya ikabidi usalama wamdhibiti. Kwa hiyo pale shule palijaa usalama kila kona.
Tulikuwa tunajua aliyefariki ni dogo fulani, lakini ghafla marehemu akajifunua kwenye shuka ikawa siyo yule tuliyeambiwa,kumbe ni dogo mwingine. Tukiwa pale kwenye jeneza marehemu ananyanyuka na kuzua taharuki.
Pale pale msibani yule mdogo wangu akanipa simu yake(nimesahau alinipa ili kufanya nini). Baadae kidogo nikawa na yule jamaa yangu niliyesoma naye chuo, tukawa tunapiga stori na washikaji.
Ghafla nikashtuka toka kwenye ndoto kuchek simu ni saa 10.40 asubuhi. Nikafikiria kuandika hii ndoto. Kidogo tu nikasikia alarm ya gari nje,nikachukua upinde na mshale na panga kwenda sitting room. Kumbe kulikuwa na kibaka kafungua mlango wa gari.
Kutaka kufungua mlango kibaka akaruka fensi akakimbia. Nikatoka nje kufunga mlango na gari. Nimemsikilizia pale sebuleni, bado kimyaaa nadhani amesepa.
Hii ndoto ina maanisha nini?