Je huu si upotoshaji wa Bw.Bulembo?

Je huu si upotoshaji wa Bw.Bulembo?

Nakapanya

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2012
Posts
2,096
Reaction score
709
Kupitia taarifa ya habari ya ITV leo usiku,nimesikia mwenyekiti wa wazazi Tanzania Bw.Abdala Bulembo akiwahimiza wananchi wilayani Mbozi kupinga baadhi ya vifungu vilivyomo katika rasimu ya katiba.

Moja ya vitu alivyosema ni kuhusu serikali tatu kwamba itavunja muungano na kuwapa faida wenye maslahi na kuvunjika kwa muungano.

Lililonishtua zaidi ni kuhusu wakuu wa wilaya,mikoa,madiwani na serikali za mitaa.Anasema rasimu imefuta wakuu wa mikoa,wakuu wa wilaya,serikal za mitaa na pia imefuta madiwani hivyo waipine kwani itazuia maendeleo ya nchi.

Sasa hoja yangu ipo hivi,rasimu inayjadiliwa hapa ni ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania,hivo masuala ya wakuu wa mikoa,wilaya na madiwani na hata serikali za mitaa vitawekwa kwenye katiba za NCHI WASHIRIKA (Tanzania Bara na Zanzibar).

Sasa leo hii kiongozi wa juu kabisa wa chama anaposimama kwenye jukwaa kuwahutubia wananchi huku akiongea upotoshaji ni kadhia kubwa sana na inaonekana viongozi wengi hawajui wanachokiongea kuhusu rasimu hii hali inayopelekea upotoshaji mkubwa kwa wananchi.

Wanajamvi tulijadili hili ili hata kama mimi niliyoyaandika hapo ni upotofu ili tuzuie kupotosha jamii.

Nawasilisha.
 
Simple, yeye mwenyewe haielewi rasimu inazungumzia nini hasa. Nimemsikia na kumwona pia....
 
Ndugu zangu wana jamvi jioni hii katika taarifa ya habari ya saa mbili leo ITV nimemsikia Mwenyekiti wa wazazi Taifa (ccm) akiwataka wananchi waikatae Rasimu ya KATIBA kwa sababu ni mzigo kuwa na serikali tatu na Raisi watatu.
Sina ugomvi na maoni yake kwani ni haki yake ya msingi kutoa mawazo yake ila ni matamshi yake kuwa katiba imefuta Madiwani na serikali za mitaa na akahoji nchi itaendeshwaje bila serikali za mitaa? Naamini hajui maudhui ya katiba yenyewe aidha ni umbumbumbu wa katiba yenyewe au amejazwa cha kusema kabla hajaisoma katiba yenyewe.
Katika ukurasa wa 131 wa katiba inaeleza wazi kuwa mambo yatakoyoshughulikiwa na serikali ya Muungano ni 7 tu.
Aelewe kuwa katiba hii kwa namna yeyote haitazungumzia madiwani kwa sababu masuala ya serikali za mitaa haziko katika mambo ya Muungano ila uendeshaji wa serikali za mitaa utatamkwa kwenye katiba ya Tanganyika (TANZANIA BARA)baada ya hii kupitishwa. Aelewe kuwa katiba ya Zanzibar ya sasa inatamka wazi nafasi za masheha.Kwa nini adanganye wananchi wa vijijini? Ni kwa maslahi ya nani.Hajaisoma katiba au ameamua kusema uongo tu?
 
mkuu mi mwenyewe nimeliona gamba nikafikiria jambo moja kuwa magamba yamepania kupotosha umma,ccm ni majanga
 
mkuu mi mwenyewe nimeliona gamba nikafikiria jambo moja kuwa magamba yamepania kupotosha umma,ccm ni majanga

sasa sijui wanafanya makusudi au ndio kutokujua wanachokisema,ila inabidi wajitafakari na kujipima upya.
 
mkuu mi mwenyewe nimeliona gamba nikafikiria jambo moja kuwa magamba yamepania kupotosha umma,ccm ni majanga

BULEMBO Is in foolish political age .hana sifa ya kumjadili hapa . Mwache -------- huyu katika upumbava wake
 
Ndugu zangu wana jamvi jioni hii katika taarifa ya habari ya saa mbili leo ITV nimemsikia Mwenyekiti wa wazazi Taifa (ccm) akiwataka wananchi waikatae Rasimu ya KATIBA kwa sababu ni mzigo kuwa na serikali tatu na Raisi watatu.
Sina ugomvi na maoni yake kwani ni haki yake ya msingi kutoa mawazo yake ila ni matamshi yake kuwa katiba imefuta Madiwani na serikali za mitaa na akahoji nchi itaendeshwaje bila serikali za mitaa? Naamini hajui maudhui ya katiba yenyewe aidha ni umbumbumbu wa katiba yenyewe au amejazwa cha kusema kabla hajaisoma katiba yenyewe.
Katika ukurasa wa 131 wa katiba inaeleza wazi kuwa mambo yatakoyoshughulikiwa na serikali ya Muungano ni 7 tu.
Aelewe kuwa katiba hii kwa namna yeyote haitazungumzia madiwani kwa sababu masuala ya serikali za mitaa haziko katika mambo ya Muungano ila uendeshaji wa serikali za mitaa utatamkwa kwenye katiba ya Tanganyika (TANZANIA BARA)baada ya hii kupitishwa. Aelewe kuwa katiba ya Zanzibar ya sasa inatamka wazi nafasi za masheha.Kwa nini adanganye wananchi wa vijijini? Ni kwa maslahi ya nani.Hajaisoma katiba au ameamua kusema uongo tu?

Kiongozi!

M/kiti wao ndio yule, unategemea nini kwa wanao ongozwa? Vuta subira kiongozi, ndani ya miaka hii miwili ndio utawashuhudia MAAMUMA WA MAGAMBA. Hapo bado huja msikia jamaa anaye jiita Le Mutus, ndio utashuhudia viroja vyake!!!
 
Sasa nimeelewa kwa nini Chadema walikua wanalalamika juu ya CCM kuhodhi uwakilishi katika mabaraza ya katiba!

Nimeona eti bulembo anaagiza wale wawakilishi wa kwenye mabaraza kupinga vipengele fulani vya katiba kwa kuwa ccm haitaki?!

Hiki kitu sidhani sidhani kama ni sahihi!!
Nadhani katiba tutakayopata inaweza kutuingiza katika machafuko na hasara kubwa iwapo haitakidhi matakwa ya wengi!
 
Mnamjadili Abdallah Bulembo!
Acheni kupoteza muda... Hana kolote! Anazunguka na yule kijana mzee wa malechela! Unategemea atasema nini
 
BULEMBO Is in foolish political age .hana sifa ya kumjadili hapa . Mwache -------- huyu katika upumbava wake

Huwezi kumtofautisha Bulembo na William Malechela ze mutuz.

Copy and paste pumpkin head.
 
LEE MUTUZ hujampa bosi wako tuition ya rasimu ya katiba?
 
Hata mimi nilimshangaa sana tena sana! Nikajiuliza, "hivi hawa watu kweli wanafikiri kwa ku2mia m@k@|¡¤ au ma2mbo?". Kuna siku nilimsikia Nape akiipinga hoja ya serikali 3 eti kwa 7bu sio sera ya chama chao! Kumbe hii ni rasimu ya chama sio ya jamhuri ya muungano? Hoja ya kibwege kabisa. Unajua wakati mwingine hawa magamba wanajisahau na kudhani kwamba tunataka kutunga katiba ya CCM.

Bulembo anavyodai kwamba rasimu inatimiza matakwa ya wa2 wachache, hv hao 'wa2 wachache' ni kina nani? Mbona hawawekwi wazi? Ninavyojua ni kwamba mfumo wa serikali 3 ni mapendekezo yaliyotolewa na wananchi kupitia tume za majaji Nyalali na Kisanga? Ama kweli magamba wanafikiri kwa ku2mia m@k@|¡¤!
 
Warioba alisema rasimu haijazungumzia kuondolewa kwa wakuu wa wilaya na mikoa.
 
Amesema katiba itafanya shule na hospitali zifungwe kwani wafanyakazi watalazimika kuomba upya kazi........,jamani huyo ndo mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi,daah kichefu chefu.....
 
Amesema katiba itafanya shule na hospitali zifungwe kwani wafanyakazi watalazimika kuomba upya kazi........,jamani huyo ndo mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi,daah kichefu chefu.....

viongozi wa namna hii ni janga kwa taifa,wapo ili mradi wapo na wanaangalia matumbo yao lakini upstairs hamna kitu
 
Sijui hata ni vigezo gani vilimpitisha kuwa mwenyekiti. Au itakua kwa sababu ni mzazi ndio maana akawa mwenyekiti wa wazazi wenye ufikiri kama wake.
 
Back
Top Bottom