Je hili suala lina ukweli wowote?

Je hili suala lina ukweli wowote?

Holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
8,708
Reaction score
19,577
Kuna wakati, matibabu ya hospitali na hata ya waganga wa miti shamba hugota, hufikia mwisho yaani hufikia point of no return.

Imagine umetembelea hospitali zote kubwa hapa nchini mfano BUGANDO na MUHIMBILI NH ikashindikana, ikabidi uende Africa kusini na ukaamua uende India, napo ikagonga mwamba, mkaambiwa mrudi nyumbani akasubiri siku ya kufa tu, mnarudi nyumbani wiki ya kwanza,ya pili mwezi, mwaka, miaka 3 mgonjwa yu hoi kitandani anasubiri kufariki ila hafi sasa.

Hawezi kula ,kunywa, kunya, kujigeuza bila ya usaidizi lakini mdomoni roketo,mgongo umechoka,unatoa funza sasa nyie kama ndugu mnaweza kufanya nini, ni mzigo kwa familia,gharama za kumtunza,muda na mateso ya mgonjwa huyo, nyie wanafamilia mnaweza kufanya nini?

Sasa basi zipo mila au tuseme desturi miongoni mwa jamii kuwa mgonjwa wa namna hiyo hupumzishwa na wanandugu kwa makubaliano kuwa kweli mtu huyu akapumzike, wapo wanaotoboa juu ya paa ili mwanga ukimfikia afe,au wengine humwekea mchi wa kutwangia chini ya mto afe, je suala hili lipo au ni nadharia?
 
Euthanasia ingeruhusiwa tu kwa wagonjwa wa hali hiyo , kuliko kumwacha mtu ateseke.
 
Kwa hali yakawaida mtu huyo tunaweza kusema anaokolewa na oragan nyingne zenye nguvu ambazo hazijakubali kushindwa kama vile moyo, ini, mapafu, figo, ubongo.
Ili mtu afe kuna oragan kuu lazima zikubali kushindwa ila kama zinaendelea na mapambano mtu kama huyo ni ngumu sana kufa

Ulimwengu wa kiroho
Yawezekana mtu huyo anapitia adhabu au fundisho au pia ahadi fulani iliyowekwa juu yake

Kifo chake ni mpaka agano fulani litimie
Aonane na mtu fulani, alishwe chakula fulani, atubu, akutane na mwanga, atolewe kitu fulani kwenye mwili wake
Yapo mambo mengi kulingana na muhusika
 
Je kumfanyia hivyo mgonjwa ikiwa yeye mwenyewe hajaridhia haiwezi Kutafsirika kama mauaji?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom