Asante, nimekupata, ubarikiweKwa nini unajionea aibu kuwa huko "virgin"? Kumbuka kuwa huo ni mwili wako na una haki ya kufanya unavyotaka. Je huyo anayetaka kukuoa naelewa kuwa huko virgin?
Ikiwa haelewi mweleze alielewe hilo, kwani anaweza kufikiria kukataa kwako kufanya naye ni kwa sababu hiyo. Sasa siku mnaamua kufunga ndoa akigundua huko virgin, unafikiria hiyo ndoa itaishia wapi?
Sikushauri utoe tu kwa sababu untaka kuolewa, wala huyo jamaa asitake tu kwa sababu kaahidi kukuoa. Ndoa kwa sasa ni hatua ya mwisho katika mahusiano, bora uhakikishe/mhakikishe kuwa kweli mnapendana.
Unaweza kuolewa siku chache ndoa ikavunjika ikiwa hakuna mapenzi, na mnaweza kuishi daima milele bila ya ndoa ikiwa mnapendana.
Kila la heri.