ram
Platinum Member
- Oct 5, 2007
- 9,346
- 8,565
sio mfano, ni kweli kabisa, mamangu mzazi (RIP)alipewa kiwanja na aliyekuwa mumewe, hicho kiwanja kilikuwa na jina la huyo baba, mamangu akajenga nyumba pale, wala huyo baba hakutia senti tano yake pale, kilichotokea baada ya ile nyumba kukamilika, yule baba akamuambia mama tusihamie pale badala yake tupangishe coz tulikuwa tunaishi kwenye nyumba ya shirika by that time, nyumba ikapangishwa lakini kwa ufupi tu hatukuwa kutia mguu kwenye ile nyumba kwani yule baba alifariki na tulipojaribu kufuatilia ili tuhamie ndugu zake walisema ile ni nyumba ya ndugu yako, mama hakutaka makuu tuliwaachia, nyumba ipo hadi leo kila siku niendapo kazini lazima nipite pale coz iko barabarani tu, thats why simshauri huyu kaka kuchangia ujenzi ktk hicho kiwanja, yeye atafute kiwanja ajenge nyumba ya familia kwani hiyo nyumba haitakuwa ya familia ni ya mke wake, maybe achangie tu lakini asijihesabie
Hebu tupe mfano mmoja na wengine waelewe unachoongea maana wengine wanamuona zoba