Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 7,923
- 13,399
Habari wandugu
Nitaenda moja kwa moja kwenye maelezo yangu kidogo sababu hili ni swali wenye majibu watujuze au wachangiaji wengine wachangie zaidi.
Kumekuwa na utaratibu ambao sasa umeonekana kuwa kawaida au mazoea kuwachukua wanyama pori Faru na kuwaweka sijui niite kwenye mabanda ya malezi au Zuu (Zoo)
Kuna taarifa za kuwepo Faru anayeitwa Faru Vicky anayetarajiwa kuwekwa kwenye banda la faru aliyefariki Faru Fausta kwa kile kilichodaiwa ni kumlinda dhidi ya maadui (wanyama wenzake) ambao si majangili.
Hili linanifanya nijiulize huu utaratibu/mazoea ni dili la mtu/watu au kuna sheria inatutaka kufanya hivyo?. Sababu ni gharama sana kuhudumia faru hawa wakiwa katika mfumo huu wa vyumba vya malezi huwenda ikawa ni gharama kuliko hata kuongeza askari wanyama pori wakapambane na ujangili.
Mtazamo wangu hili tuliangalie upya, huwenda tunatumia gharama kubwa bila msingi wowote hasa ikizingatiwa kumetolewa sababu ya eti ni mzee wa miaka 49 hivyo analindwa dhidi ya wanyama wenzake. Kwanini tusiache mfumo wa asili ufuate mkondo kisha sisi tukajikita kupambana na majangili?.
Nasikitika swali langu halijawa fupi kamanilivyo ahidi hapo awali na huwenda limegeuka makala fupi.
Shukrani.
VIIXCCCL GrandLodge,ARUSHA
Nitaenda moja kwa moja kwenye maelezo yangu kidogo sababu hili ni swali wenye majibu watujuze au wachangiaji wengine wachangie zaidi.
Kumekuwa na utaratibu ambao sasa umeonekana kuwa kawaida au mazoea kuwachukua wanyama pori Faru na kuwaweka sijui niite kwenye mabanda ya malezi au Zuu (Zoo)
Kuna taarifa za kuwepo Faru anayeitwa Faru Vicky anayetarajiwa kuwekwa kwenye banda la faru aliyefariki Faru Fausta kwa kile kilichodaiwa ni kumlinda dhidi ya maadui (wanyama wenzake) ambao si majangili.
Hili linanifanya nijiulize huu utaratibu/mazoea ni dili la mtu/watu au kuna sheria inatutaka kufanya hivyo?. Sababu ni gharama sana kuhudumia faru hawa wakiwa katika mfumo huu wa vyumba vya malezi huwenda ikawa ni gharama kuliko hata kuongeza askari wanyama pori wakapambane na ujangili.
Mtazamo wangu hili tuliangalie upya, huwenda tunatumia gharama kubwa bila msingi wowote hasa ikizingatiwa kumetolewa sababu ya eti ni mzee wa miaka 49 hivyo analindwa dhidi ya wanyama wenzake. Kwanini tusiache mfumo wa asili ufuate mkondo kisha sisi tukajikita kupambana na majangili?.
Nasikitika swali langu halijawa fupi kamanilivyo ahidi hapo awali na huwenda limegeuka makala fupi.
Shukrani.
VIIXCCCL GrandLodge,ARUSHA