Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,372
Kuna baadhi ya wanasiasa kutoka Chama cha Mapinduzi(CCM) huwa ni wepesi sana kuongelea maswala ya uchaguzi mitandaoni kama vile kupost tweet za kupongeza ushindi wa wagombea wa chama chao huku wengine wakisindikiza tweet hizo na vijembe vya kisiasa kwa wapinzani.
Cha kushangaza ni kuwa nimepitia akaunti za twitter za makada hawa asubuhi hii sijaona popote walipoongelea habari hii ya uchaguzi wa jana wala kutoa pongezi kwa wagombea waliotangazwa washindi na hata kurusha vijembe kwa wapinzani kama ilivyo kawaida yao.
Je, hali hii ni matokeo ya hata wao nafsi zao kuona hawana uhalali wa kushangilia ushindi huu ambao ni wazi si wa haki?
Je, wameanza kutambua hatari iliyopo hata kwa upande wao?
Je, huu si ushahidi kuwa hata kampeni za kuwanadi wagombea wa chama chao wameshiriki kwa shingo upande tu?
Si mawaziri wanaopenda ku-tweet wala wabunge wanaopenda kufanya hivyo ambao mpaka muda huu wameandika chochote akiwemo na bwana slow slow mwenyewe.
Je, ni hivi hivi tu au kuna jambo nyuma ya pazia?
Wacha tuendele ku-observe hali hii tutapata majibu.
Cha kushangaza ni kuwa nimepitia akaunti za twitter za makada hawa asubuhi hii sijaona popote walipoongelea habari hii ya uchaguzi wa jana wala kutoa pongezi kwa wagombea waliotangazwa washindi na hata kurusha vijembe kwa wapinzani kama ilivyo kawaida yao.
Je, hali hii ni matokeo ya hata wao nafsi zao kuona hawana uhalali wa kushangilia ushindi huu ambao ni wazi si wa haki?
Je, wameanza kutambua hatari iliyopo hata kwa upande wao?
Je, huu si ushahidi kuwa hata kampeni za kuwanadi wagombea wa chama chao wameshiriki kwa shingo upande tu?
Si mawaziri wanaopenda ku-tweet wala wabunge wanaopenda kufanya hivyo ambao mpaka muda huu wameandika chochote akiwemo na bwana slow slow mwenyewe.
Je, ni hivi hivi tu au kuna jambo nyuma ya pazia?
Wacha tuendele ku-observe hali hii tutapata majibu.