Je, hali ingekuwaje kama Dr. Slaa ndiye angeteuliwa kupeperusha bendera ya UKAWA?

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Habari zilizotapakaa jijini ni kwamba siku ya Jumamosi tarehe 28/9/2015 ndio UKAWA imepanga kuzindua kampeni zake kumtambulisha mgombea wake ambaye ni Dr. W. P. Slaa. Wiki moja kabla CCM ilikuwa imezindua kampeni zake kwenye uwanja huo huo ikimtambulisha mgombea wake Dr. J. P. Magufuli.

Hapana, nilikuwa naota tu ingawa hiyo ndoto imeniacha kwenye tafakari kubwa na nzito. Baada ya kufuatilia kampeni zilivyoendeshwa na zinakoelekea najiuliza je, hali ingekuwaje kama Dr. W. P. Slaa ndiye angeteuliwa na Chadema na kupitishwa na UKAWA (hapa sina hakika) kama mgombea Uraisi?

Nianze kwa kukiri kuwa hapo awali nilikuwa mpenzi mkubwa wa Dr. W. P. Slaa lakini kwa sasa nimemkubali E. N. Lowassa, je nilichukua uamuzi sahihi? Tofauti na wengi nilichukua uamuzi huo bila hata kusubiri nijue msimamo wa Dr. P. W. Slaa nikiwa na tumaini kuwa angeunga mkono uteuzi wa E. N. Lowassa.

Yaliyotokea yalitokea, Dr. Slaa alipojitokeza hakuunga mkono na badala yake aliamua kukaa kando na kutokujihusisha kabisa na siasa, uamuzi ambao nilikubaliana nao. Ghafla alijitokeza tena na safari hii alikuja na jipya kwa kusema kwamba hawezi, kukaa kimya, ameamua kuunga mkono upande wa pili.

Siku zote nimeamini adui wetu mkubwa kama taifa ni CCM na mimi ni katika wale wanaoamini kwa dhati kuwa CCM ni ile ile na haiwezi kusimamia mabadiliko. Hapa najaribu kujenga tu kajumba kangu angani...Lowassa na Slaa....nilikuwa naota tu.



Hii ndiyo Mbeya
 
Last edited by a moderator:
Babu slaa angepondwa na magamba sana tu,tusingekuwa tunashine namna hii.

Kwa ufupi ingekula kwetu makamanda.
 
Watakuja watu na kusema Dr. Slaa mzuri kuliko Lowassa. Na sababu watasema Lowassa fisadi. Hapa Tz ni kiongozi yupi ambaye hajawahi kupiga deal. Mimi mwenyewe ni Fisadi mdogo sembuse wakina JK .
 
... nadhani sifa/historia ya kwamba aliwahi kuwa 'upadri' ingemnyima kura nyingi tu
 
ungekuwa na busara ungesha ifuta thread yako. Mpaka leo hujui Dokta kakuza upinzani katika nchi hii.

Mkuu Maistro labda mimi nitakuwa nimeelewa tofauti hii Thread ya jamaa. Unikosoe hapa. Awali alikuwa anampenda DR. Lakini kutokana na kitendo kilichotokea cha kumkana Lowassa ile hali ya mapenzi kwa Dr. imepotea. Kingine ni ile haya ya undumi la kuwili. Unaongea hiki baada ya dk chache unaongea lingine. Na sidhani kama kuna mahala MAG3 ameonyesha kupiga kuhusiana na juhudi za DR. kukuza Upinzani. Unikosoe mkuu..!!
 
ungekuwa na busara ungesha ifuta thread yako. Mpaka leo hujui Dokta kakuza upinzani katika nchi hii.
Sijasema hajakuza upinzani ingawa hata hapo naweza nikakuuliza unamlinganisha na nani? Hivi unajua wako watu waliodai mageuzi na hadi leo hii wako upinzani? Bila watu hao kupigania mfumo wa vyama vingi Dr. Slaa angepata wapi pa kujisetiri alipotemwa na chama chake cha CCM mwaka 1995? Je haya mafuriko ya Jangwani yaliyosababishwa na ujio wa Lowassa Chadema, Dr. Slaa angeyapata? Toa tu sababu ndugu yangu hakuna haja ya kuhamaki, je UKAWA umenufaika na ujio wa Lowassa?




 
Last edited by a moderator:
Mgombea bora bado ataendelea kubaki Magufuli hata kama wakiungana na na huyo gwiji wa maigizo lowassa bado tungewapiga tena asubuhi kweupeeee
 
Magufuli angeshinda kiulani hata mi nisinge MPA kura Mara awe padre amwache mkewe mtu mzima ana mchumba hivo vilinifanya nisimwamini kitendo cha kuacha wito kumtumikia bwana Yesu.
 
>lakini kwa sasa nimemkubali E. N. Lowassa, je nilichukua uamuzi sahihi?<

Of course umechukua uamuzi sahihi. Hii ni kwasababau wewe unajua kuwa kuiondoa rushwa nchini sio kuikemea bali kupata Katiba yenye maana na unajua kuwa there is no way kama Magufuli atatupa Katiba nyengine zaidi ya hii iliyopendekezwa na CCM ambayo inalinda status quo ya CCM tu!
Kwahivyoa Kaka ulichukua uamuzi sahihi kumuunga mkono Lowassa.
 
Mag3

Ungekuwa na busara ungesha ifuta thread yako. Mpaka leo hujui Dokta kakuza upinzani katika nchi hii.

Elewa uzi unazungumzia jambo gani. Imezungumzia Dr Slaa kuwa mgombea wa UKAWA, siyo mchango wake katika kukuza upinzani!
Kama wengi walivyochangia, UKAWA ingeangukia pua, isingepata waungwaji mkono wengi kama tunaowaona sasa. Kama mchangiaji mmoja alivyoacha kung'ata maneno, kura za CUF ingekuwa ni ndoto!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom