chabuso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 6,379
- 5,887
Habari za mitandaoni Dunia nzima Ni kuhusu kifo cha Mmarekani Mweusi George Floyd.
Katika dini ya Kiislam Mitume iko mingi wengine wanajulikana na wengine hawajulikani. Kuna Mitume Kama 123 ambayo inajulikana, kuna Mitume inaliyopewa vitabu na isiyopewa vitabu.
Mitume inafanya kazi ya Mungu katika jamii iliyomzunguka au hata kuleta mabadiliko Dunia nzima. Yesu aka Issa aka Jesus kabadilisha Dunia, Muhamad kabadilisha Dunia, kuna akina Musa, Sulemani nk ambao wamebadilisha jamii zao.
Uonevu kwa watu weusi unaofanywa na Polisi katika nchi ya Marekani haujaanza leo. Kifo cha George Floyd kimeleta mtazamo mwengine katika vitendo vya uonevu vinavyofanywa na Polisi kwa watu weusi.
Hivi sasa dunia nzima, nchi za Ulaya, Marekani, Australia nk watu wanaandamna mbele ya balozi za Marekani kupinga unyanyasaji wa Polisi kwa watu weusi.
Katika Jimbo la California Polisi leo wameungana na waandamanaji kupinga vitendo vya unyanyasaji wa watu weusi. Cha kushangaza, wengi wa waandamanaji ni watu weupe; cha kushangaza zaidi, nchi za Kiafrika ambazo ni chimbuko la watu weusi hamna hata nchi moja watu wameandamana kupinga uonevu huo.
Donald Trump leo kalazimika kupelekwa kwenye handaki chini ya White House kwa usalama wake baada ya waandamanaji kuandamana mbele ya White House.
Jeshi limeingia mitaani kuungana na Polisi, kafuu ya kukataaa watu wasitoke majumbani mwao imewekwa nchi Marekani. Haijawahi kutokea, Marekani kama vile kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Je, George Floyd ni Mtume asiejulikana alietumwa na Mungu kuibadilisha mitazamo ya watu kuhusu mtu Mweusi nchini Marekani?
Katika dini ya Kiislam Mitume iko mingi wengine wanajulikana na wengine hawajulikani. Kuna Mitume Kama 123 ambayo inajulikana, kuna Mitume inaliyopewa vitabu na isiyopewa vitabu.
Mitume inafanya kazi ya Mungu katika jamii iliyomzunguka au hata kuleta mabadiliko Dunia nzima. Yesu aka Issa aka Jesus kabadilisha Dunia, Muhamad kabadilisha Dunia, kuna akina Musa, Sulemani nk ambao wamebadilisha jamii zao.
Uonevu kwa watu weusi unaofanywa na Polisi katika nchi ya Marekani haujaanza leo. Kifo cha George Floyd kimeleta mtazamo mwengine katika vitendo vya uonevu vinavyofanywa na Polisi kwa watu weusi.
Hivi sasa dunia nzima, nchi za Ulaya, Marekani, Australia nk watu wanaandamna mbele ya balozi za Marekani kupinga unyanyasaji wa Polisi kwa watu weusi.
Katika Jimbo la California Polisi leo wameungana na waandamanaji kupinga vitendo vya unyanyasaji wa watu weusi. Cha kushangaza, wengi wa waandamanaji ni watu weupe; cha kushangaza zaidi, nchi za Kiafrika ambazo ni chimbuko la watu weusi hamna hata nchi moja watu wameandamana kupinga uonevu huo.
Donald Trump leo kalazimika kupelekwa kwenye handaki chini ya White House kwa usalama wake baada ya waandamanaji kuandamana mbele ya White House.
Jeshi limeingia mitaani kuungana na Polisi, kafuu ya kukataaa watu wasitoke majumbani mwao imewekwa nchi Marekani. Haijawahi kutokea, Marekani kama vile kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Je, George Floyd ni Mtume asiejulikana alietumwa na Mungu kuibadilisha mitazamo ya watu kuhusu mtu Mweusi nchini Marekani?