Je, gari yako inatetemeka, engine kumisi au ukiwasha inazima inapokuwa ya baridi?

JituMirabaMinne

JF-Expert Member
May 4, 2020
3,327
9,328
Je, gari yako inatetemeka engine ikiwa ya baridi?

Je, engine ya gari yako inamisi inapokuwa ya baridi?

Je, gari yako ukiwasha inazima yenyewe mpaka uwashe mara kadhaa au uwashe na kupiga resi mara kadhaa ndio itulie isizime?

Kwanza kabisa kama ukiwasha gari unakimbilia kupiga resi basi unategeneza tatizo lingine kubwa na muda ukifika zitakutoka hela nyingi. Kwanza ukiachana na kukumalizia mafuta, kupiga resi baada tu ya kuwasha gari inaweza kupelekea spark plug kuwa fouled (yaani spark plug zako zinakuwa covered na mafuta, Oil au carbon na hivyo kuzifanya zishindwe kufanya kazi katika ubora wake)

Sasa turudi kwenye maada. Kama gari yako inatememeka, kumisi au kuzima kila ukiwasha mpaka uwashe mara kadhaa basi kwa sehemu kubwa matatizo huwa yanakuwa kwenye sehemu mbili au tatu kulingana na aina ya gari. Sehemu hizo ni:-

1. Intanke Air Temperature (IAT) sensor

rh54100002_1.jpeg


images (5).jpeg


Hii sensor ina njia mbili za kufa, Inawez kufa ikawa inapelekea signal kwamba hewa inayoingia kwenye engine ni ya moto(hot signal) au signal ya cold signal. Kama ikipeleka signal ya hot basi gari lako lazima tu likusumbue kuwaka kwa sababu mafuta yatakuwa yanaenda machache na engine ni ya baridi hivyo hayatawaka vizuri. Baadhi ya watu atasema alisolve hili tatizo kwa kubadili MAF sensor ila kama connector ya hiyo MAF sensor ina pin 5 basi ndani ya hiyo maf sensor kuna IAT sensor pia na hakuna namna unaweza kuzitenganisha

2. Engine Temperature sensor(ECT) sensor

images (7).jpeg


images (8).jpeg


Hii sensor ina tabia zinazofanana na za hiyo IAT sensor hapo juu kwa asilimia 100. Utofauti ni kwamba hii yenyewe inapima joto la coolant. Kwa hiyo nayo kama muda wote inapeleka signal ya hot basi lazima gari litasumbua kuwaka au litawaka kwa kumisi na kuvibrate. Ni vizuri mtu akawa makini, usije ukaona tatizo ukakimbilia kwa fundi ukamuambia akubadilishie sensor hii, baadhi ya gari zinakuwa na sensor za aina hii mpaka 3, zingine kwenye rejeta na zingine kwenye engine, hivyo unaweza kubadili na tatizo lisiishe kumbe umebadili sensor nzima.

3. Exhaust Gases Recirculation(EGR) Valve

images (6).jpeg


Kama hii valve ikijaa carbon au solenoid yake ikiwa mbovu basi inaweza kupelekea valve hii kubaki wazi wakati gari inawaka wakati ilitakiwa kuwa imefungwa. Sasa mafuta yanakuwa yanawaka kwa shida halafu kuna exhaust gases zinarudi tena kuja kuchomwa, hapo lazima gari liwake kwa shida. Pia gari nyingi hazina EGR valve labda kwenye SUV na baadhi tu ya sedan/saloon.

Kama kuna kitu ambacho nitakuwa nmekisahau nitakiongeza.

MWISHO.
 
Hiyo Hali ya gari kuzima yenyewe kipindi cha asubuh ilikuwa inanitokea mara nyingi Sana Ila nakumbuka niliongeza silencer kidogo kwasabb ilikuwa chini.

Mpaka nauza hii gari(Carina TI ) bado silencer yake IPO juu pale Kwenye moja( rpm 1) na kama utashusha silencer basi gari huwa inazima daily.....

Pengine Leo unaweza kunisaidia/kutusaidia Hilo TATIZO lilisababishwa na nini?
 
Hiyo Hali ya gari kuzima yenyewe kipindi cha asubuh ilikuwa inanitokea mara nyingi Sana Ila nakumbuka niliongeza silencer kidogo kwasabb ilikuwa chini.
Mpaka nauza hii gari(Carina TI ) bado silencer yake IPO juu pale Kwenye moja( rpm 1) na kama utashusha silencer basi gari huwa inazima daily.....

Pengine Leo unaweza kunisaidia/kutusaidia Hilo TATIZO lilisababishwa na nini?
Kama ina choke huenda ikawa kisababishi.
 
Kwa mwenye kujua aniambie:

Nimepoteza OBD2 reader yangu, sasa imenilazimu kutumia jumper kutizama code kwenye lexus is200. nimepata code 21 ambayo inasema Main O2S and heater signal. Nina 3 O2 sensors ndani ya gari sijajua hio MAIN ndio ipi hapa.

Mambo ya kuread code bila OBD2 scanner unaweza kujikuta unabadilisha vitu vingi aisee mana haisemi exactly tatizo liko wapi.
 
Kwa mwenye kujua aniambie:

Nimepoteza OBD2 reader yangu, sasa imenilazimu kutumia jumper kutizama code kwenye lexus is200. nimepata code 21 ambayo inasema Main O2S and heater signal. Nina 3 O2 sensors ndani ya gari sijajua hio MAIN ndio ipi hapa.

Mambo ya kuread code bila OBD2 scanner unaweza kujikuta unabadilisha vitu vingi aisee mana haisemi exactly tatizo liko wapi.
Cheki nao mafundi Tu Mkuu alafu hata huyu jamaa JituMirabaMinne mtafute akusaidie
 
Hiyo Hali ya gari kuzima yenyewe kipindi cha asubuh ilikuwa inanitokea mara nyingi Sana Ila nakumbuka niliongeza silencer kidogo kwasabb ilikuwa chini.
Mpaka nauza hii gari(Carina TI ) bado silencer yake IPO juu pale Kwenye moja( rpm 1) na kama utashusha silencer basi gari huwa inazima daily.....

Pengine Leo unaweza kunisaidia/kutusaidia Hilo TATIZO lilisababishwa na nini?

Kama ilikuwa inazima wakati wa asubuhi tu basi sababu ni IAT sensor au ECT sensor(Carina haina EGR valve). Ila kama ilikuwa inazima muda wote basi sababu ni Idle Air Control Valve(IACV) ama chafu ama inatoa voltage ambayo ni nje ya range(range huwa ni 6.5V mpaka 8.5V)

Unapopandisha silence maana yake unafungua throttle hivyo gari itakuwa inatumia mafuta mengi ikiwa silence. Hivyo bado inakuwa ni vizuri zaidi kusolve tatizo.
 
Kwa mwenye kujua aniambie:

Nimepoteza OBD2 reader yangu, sasa imenilazimu kutumia jumper kutizama code kwenye lexus is200. nimepata code 21 ambayo inasema Main O2S and heater signal. Nina 3 O2 sensors ndani ya gari sijajua hio MAIN ndio ipi hapa.

Mambo ya kuread code bila OBD2 scanner unaweza kujikuta unabadilisha vitu vingi aisee mana haisemi exactly tatizo liko wapi.

Njia rahisi ni kama unaweza kupata multimeter basi pima resistance au continuity ya heater circuit ya kila O2 sensor yako. Sijajua O2 sensor yako ni ya njia tatu au nne lakini katika hizo nyaya zote za oxygen sensor, nyaya za heater circuit huwa zinakuwa na rangi moja. Hivyo angalia nyaya mbili ambazo zina rangi moja kwenye kila sensor.
 
Kwa mwenye kujua aniambie:

Nimepoteza OBD2 reader yangu, sasa imenilazimu kutumia jumper kutizama code kwenye lexus is200. nimepata code 21 ambayo inasema Main O2S and heater signal. Nina 3 O2 sensors ndani ya gari sijajua hio MAIN ndio ipi hapa.

Mambo ya kuread code bila OBD2 scanner unaweza kujikuta unabadilisha vitu vingi aisee mana haisemi exactly tatizo liko wapi.

Pia katika hizo sensor zako, Nadhani kuna sensor moja imefungwa baada ya catalytic converter(Hiyo usiiweke kwenye hesabu angalia hizo mbili zilizobaki).
 
Kwa mwenye kujua aniambie:

Nimepoteza OBD2 reader yangu, sasa imenilazimu kutumia jumper kutizama code kwenye lexus is200. nimepata code 21 ambayo inasema Main O2S and heater signal. Nina 3 O2 sensors ndani ya gari sijajua hio MAIN ndio ipi hapa.

Mambo ya kuread code bila OBD2 scanner unaweza kujikuta unabadilisha vitu vingi aisee mana haisemi exactly tatizo liko wapi.

Halafu mkuu, umewahi kutumia jumper halafu taa ya check engine ikabaki tu imeganda, yaani haiblink baada ya kuweka switch on.
 
Cheki nao mafundi Tu Mkuu alafu hata huyu jamaa JituMirabaMinne mtafute akusaidie
Nilikwenda kwa fundi akataka nimpe 35,000 kufanya diagnosis ya kuntizamia tu sababu ya check engine kuwaka. Ni very simple thing ku extract hizo code kitu ambacho hakiendani na price. Wenzetu duniani wanafanyiana bure hio kazi. Halafu alichoniudhu wakati namwambia apunguze akacheka akanambia eti anipe mtu aone atakavonifanyia (kuonesha kwamba mtu mwengine atavuruga tu) nikamwambia mimi nilikuwa nnayo obd2 reader ila sijui nimeiweka wapi tu. Nikaondoka zangu na kufanya jumper. Tatizo la kusoma kwa Jumper ndo hilo, kuna vitu itakwambia hichi kumbe sehemu nyingine au haikwambii specific. Sasa ningetumia reader, ingenambia hasa ni sensor ipi kimeo.

Itabidi nikisake kwa udi na uvumba sasa. :D
 
Pia katika hizo sensor zako, Nadhani kuna sensor moja imefungwa baada ya catalytic converter(Hiyo usiiweke kwenye hesabu angalia hizo mbili zilizobaki).
Hii iliokuwa kwenye catalytic converter nimeitilia mashaka kwa sababu, niliwahi kubadilisha before sikukaa mda mrefu ndio nikajiweka kwenye ile project yangu. Nilipoona haiiwi ndio nimerudisha engine yangu ya zamani. Sasa nimekula route kama 15 miles ivi ikawaka ndio leo nimecheki nikakuta hio code. Sasa ishu ni kuwa Exhaust inavuja kwenye joint, wasiwasi wangu labda ile exhaust heat ina escape sana na kusababisha hio sensor kwenye catalytic conv kutopata moto na ECU kuitambua kuwa imebuma.

Halafu naona hii MAIN mara huenda ikawa Bank 1 Sensor 1. Kuna reader nilimpa fundi wangu sijui kama na yeye anacho bado ama kashakitupa mana hakuwa akikitumia.
 
Halafu mkuu, umewahi kutumia jumper halafu taa ya check engine ikabaki tu imeganda, yaani haiblink baada ya kuweka switch on.
Kama umejump pins sahihi halafu haiblink, ECU inatatizo hio.

Muhimu kufanya double checking wakati wa kujump, mfano kule mbele kwenye engine kuna kile kijiboksi kimeandikwa Diagnosis, E1 na TE1 ndio zinatumika kusoma codes, lakini mimi kwenye gari yangu TE1 was blank, hamna connection ya chochote imewekwa kama pambo tu nafikiri itakuwa OBD2 cars zote ziko ivi na inakulazimu u jump kwenye port ya OBD2 which is pin 4 (Ya juu) na pin 13 (chini).

Ukiona haiflash ndio ivo ECU haiko sawa.
 
Hii iliokuwa kwenye catalytic converter nimeitilia mashaka kwa sababu, niliwahi kubadilisha before sikukaa mda mrefu ndio nikajiweka kwenye ile project yangu. Nilipoona haiiwi ndio nimerudisha engine yangu ya zamani. Sasa nimekula route kama 15 miles ivi ikawaka ndio leo nimecheki nikakuta hio code. Sasa ishu ni kuwa Exhaust inavuja kwenye joint, wasiwasi wangu labda ile exhaust heat ina escape sana na kusababisha hio sensor kwenye catalytic conv kutopata moto na ECU kuitambua kuwa imebuma.

Halafu naona hii MAIN mara huenda ikawa Bank 1 Sensor 1. Kuna reader nilimpa fundi wangu sijui kama na yeye anacho bado ama kashakitupa mana hakuwa akikitumia.

Moshi unavuja kabla ya sensor iliyopo kabla ya catalytic converter au kabla ya zile sensor mbili za mwanzo?
 
Nilikwenda kwa fundi akataka nimpe 35,000 kufanya diagnosis ya kuntizamia tu sababu ya check engine kuwaka. Ni very simple thing ku extract hizo code kitu ambacho hakiendani na price. Wenzetu duniani wanafanyiana bure hio kazi. Halafu alichoniudhu wakati namwambia apunguze akacheka akanambia eti anipe mtu aone atakavonifanyia (kuonesha kwamba mtu mwengine atavuruga tu) nikamwambia mimi nilikuwa nnayo obd2 reader ila sijui nimeiweka wapi tu. Nikaondoka zangu na kufanya jumper. Tatizo la kusoma kwa Jumper ndo hilo, kuna vitu itakwambia hichi kumbe sehemu nyingine au haikwambii specific. Sasa ningetumia reader, ingenambia hasa ni sensor ipi kimeo.

Itabidi nikisake kwa udi na uvumba sasa. :D

Sema Jumber unacover vitu vingi tofauti na OBD 2. Uzuri wa OBD 2 ni kwamba iko straight.. Haina kona nyingi.
 
Kama umejump pins sahihi halafu haiblink, ECU inatatizo hio.

Muhimu kufanya double checking wakati wa kujump, mfano kule mbele kwenye engine kuna kile kijiboksi kimeandikwa Diagnosis, E1 na TE1 ndio zinatumika kusoma codes, lakini mimi kwenye gari yangu TE1 was blank, hamna connection ya chochote imewekwa kama pambo tu nafikiri itakuwa OBD2 cars zote ziko ivi na inakulazimu u jump kwenye port ya OBD2 which is pin 4 (Ya juu) na pin 13 (chini).

Ukiona haiflash ndio ivo ECU haiko sawa.

Niliconnect E1 na TE1 taa ya check engine ikabaki tu imeganda. Nilipita mtandaoni nikaona hizo story za ECU ndo inashida ah basi nikaamua kuachana na hiyo gari.
 
Aiseee hapo ni majanga....
Apo cha msingi kama unapata ECU nyengine unaweka na kutest kuona, mana pia isijekuwa hio gari iliwahi kuchezewa wiring ikawa OBD2 port haifanyi kazi.

By the way, leo wakati nafanya Jumping, nimeshuhudia na ku confirm kuwa ECU kama ina immobilizer itakuja code 99 tu, kwenye ile project yangu hii code haikuwahi kutokea, nna machungu mafundi wiring wameniharibia control!
 
Back
Top Bottom