johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 84,035
- 142,145
Najaribu tu kujiuliza yule Prof nguli wa uchumi kitaifa na kimataifa tuliyeaminishwa na wanangangari kuwa dunia nzima inamtegemea, amepotelea wapi? Ninajua kimikakati na ubunifu Dr Slaa yuko vizuri kuliko Prof Lipumba ndio maana hata UKAWA original ilimtaka Slaa agombee urais na Lipumba agombee ubunge. Lakini katika siasa za leo umaarufu wa mwanasiasa unapimwa kwa jinsi anavyoheshimiwa na CCM, kama tulivyoona kiongozi mkuu wa upinzani Edward Lowassa alipokutana na Mwenyekiti wa CCM umaarufu wake ulipanda, nk....nk. Kwahiyo bado najiuliza kati ya Dr Slaa na Prof Lipumba nani ni maarufu kwa mtazamo ule ule wanavyoheshimika mbele ya wanachama wa CCM na hata wale wa upinzani! Ahsante!