Je Cremation Ni Mbaya?!

Je Cremation Ni Mbaya?!

TheCrazy Mchokozi

Senior Member
Joined
Apr 7, 2017
Posts
181
Reaction score
252
Ungependelea Mwili wako upitie hali ipi siku ya kifo chako, Udongoni au kwenye moto mkali

Nimekuwa na huu mjadala na baadhi ya marafiki wangu wa karibu kwani tupo katika Mazingira ya hospitali na tunaona watu wakija kuchukua miili ya wapendwa wao kwa ajili ya mazishi

Ila kwa sasa Mazishi yameanza kuwa ya gharama kubwa na pesa nyingi zinatumika katika Procedure nzima ya burial ( Kama umeona mazishi ya siku hizi)

Baada ya kuona haya ilifika mahali tukahoji swala la Cremation,... Je ni kosa au vibaya kumchoma mtu mpaka kuwa jivu (disposing corpses by burning them to Ashes)

Cremation kwa kuangalia inapunguza unnecessary costs za msiba ukizingatia wengi sasa wamefanya mazishi kuwa njia ya kipato.

Je kisheria mtu ana haki ya kuchagua cremation kama njia ya burial ikitokea amefariki?!

Baada ya cremation wahusika wa marehemu uchukua jivu(ashes of the deceased); Wengine urushia lile jivu baharini, wengine utafuta chungu(pot or urn) na kuweka hii jivu kama njia ya kumbukumbu

Wengi wanaoachagua cremation over burial ni wale ambao wanachukia ile fact ya kuoza kwa mwili.

Labda Nijue kwa Wengine kama Swala la Cremation ni swala sahihi na je wewe ungependa mwili wako upitie huduma gani ukifa?!
 
Kwakweli mimi swala la kunichoma na moto silitaki kama wamenichoka sana bora wanitupe tu kuliko kunichoma na moto...
What if mtu akifa anakuwa anasense maumivu (maana hakuna mtu aliyewahi kurudi kutoka kifo akwatwambia ukifa unakuwaje)

Mimi kunichoma hapa aiseh tutamaindiana na mtu nikifa akatoa wazo la kunichoma
 
Kwa wale wasiojua cremation ninini ......ni kuchoma moto mwili wa mfu kulingana na tamaduni husika
Binafsi naipenda kwakuwa tunaipunguzia ardhi kuilisha uozo na uvundo laana na mabalaa
Mimi binafsi nafikiri ni njia nzuri yakuyalinda mazingira,...
Cremation ni njia nzuri sana na inaokoa gharama na kupunguza matumizi mabaya ya ardhi
 
Dunia iliumbwa kwa namna ya pekee sana na namna hiyo ni kurecycle kila kitu kilichopo juu ya mgongo wake.

Binadamu, wanyama au kiumbe hai chochote kinapokufa na kuzikwa ardhini minyoo wanawahi kuchukua viini lishe na kusambazia ardhi then ardhi inapokea na kuwa na rutuba na kuipa mimea ili iistawi na binadamu wengine wale na kurutubisha miili yao. Hivyo kuzika ardhini kunawapa fursa minyoo kusambaza vile viini lishe ardhini then kwa binadamu waliobaki kwa kupitia vyakula vinavyotoka ardhini then maisha yanazidi kustawi Duniani.

Hata mvua hajawahi kuja mvua mpya ...maji ni yale yale kutoka baharini na Kwenye maziwa yanapanda juu kama mvuke then yananyesha baadae kama mvua tena..and the cycle continues.

Hivyo kuzikwa ardhini ndio njia sahihi kabisa ya kuifanya Dunia iwe sustainable(endeleveu) maana si ajabu roho ni zile zile zinajirudia Duniani bila kujua maana ukizaliwa unakuwa huna kumbukumbu ya unapotoka na kwa vile God ana recycle kila kitu...probably souls and spirits zetu zina reincarnate tu kwa kwenda na kurudi Duniani. Labda! Sina hakika sana.

Na tunapojifanyaga tuna akili zaidi kuliko yeye basi anacheeeeka huko enzini!

God is the beste designer and first infinity genius.

Cc the crazy mchokozi Mshana Jr
 
Kwakweli mimi swala la kunichoma na moto silitaki kama wamenichoka sana bora wanitupe tu kuliko kunichoma na moto...
What if mtu akifa anakuwa anasense maumivu (maana hakuna mtu aliyewahi kurudi kutoka kifo akwatwambia ukifa unakuwaje)

Mimi kunichoma hapa aiseh tutamaindiana na mtu nikifa akatoa wazo la kunichoma
Ata kama ukifa unapata hisia bhasi pia wakati mchwa wanakula nyama yako utasikia,..

Ila mwili haupati hisia zozote kama ubongo wako haupo active... bhasi njia zote mbili ni njia za kutupa uchafu (Maiti haina thamani tena na ingekuwa nayo tungeishi nazo nyumbani)
 
Tatizo ni taratibu za kiimani ambazo tumekua nazo. Mimi kwa mawazo yangu binafsi huwa nawaza nikifa nitoe sadaka viungo ambavyo vinaweza kutumika kwa watu wengine walio hai na kitakachobaki basi kikachomwe tu. Sidhani kama roho ikishatoka kiwiliwili huwa na thamani tena.
 
Ata kama ukifa unapata hisia bhasi pia wakati mchwa wanakula nyama yako utasikia,..

Ila mwili haupati hisia zozote kama ubongo wako haupo active... bhasi njia zote mbili ni njia za kutupa uchafu (Maiti haina thamani tena na ingekuwa nayo tungeishi nazo nyumbani)
Yote tisa lakini mimi kuchomwa moto hapana aiseeh huo utaratibu waachie wahindi na wakorea sisi watuzike tu chini...kama ni ardhi tunayo ya kutosha hadi nyingine watu hawajawahi kuikanyaga
 
All in all mm sitaki kufa jamanii
Kama unaishi bhasi tambua kwamba ipo siku tu
Heheh ni swala la kujilinda sasa ivi uweze kuongeza muda wa kuishi dunia tu ila 'Man Is Mortal being' ipo siku pumzi itakutoka
 
Yote tisa lakini mimi kuchomwa moto hapana aiseeh huo utaratibu waachie wahindi na wakorea sisi watuzike tu chini...kama ni ardhi tunayo ya kutosha hadi nyingine watu hawajawahi kuikanyaga
Hufai kuogopa kwani ni njia za mazishi kwani mwili wako umepoteza hisia na imebaki kuoza tu,...

Sema ni vizuri kuwa na msimamo lakini Cremation sio mbaya fanya kuifikiria pia utaona manufaa yake
 
Tatizo ni taratibu za kiimani ambazo tumekua nazo. Mimi kwa mawazo yangu binafsi huwa nawaza nikifa nitoe sadaka viungo ambavyo vinaweza kutumika kwa watu wengine walio hai na kitakachobaki basi kikachomwe tu. Sidhani kama roho ikishatoka kiwiliwili huwa na thamani tena.
Mkuu Hili Pia Nilitaka Kulizungumzia

Kuliko kuacha Macho yaoze, Figo zioze, Mapafu yaoze mbona watu wasingekubali kwamba viungo ivi vitolewe sadaka kwa waliohitaji

Lakini kama unavyosema 'IMANI' zimetufunga pia tunaamini kwenye kuzikwa na kuoza na kila kitu

Wazo zuri sana Mkuu
 
Ni wazi kabisa kuwa misiba ya kimagharibi ni gharama mno na inapoteza sana rasilimali,mara mbao sijui vyuma sijui zege yaani ujinga ujinga tu.Mimi nikifa bora tu nichomwe moto,kwanza inasaidia kuokoa maeneo,wenyewe mnaona sikuizi jinsi viwanja vya makaburi vinavyojaa.

Ila kuna wanasayansi wa Italia wamegundua mbinu nyingine ya kuzika maiti,unazikwa kwenye kitu chenye umbo la yai ukiwa umewekwa position ya mtoto kwenye tumbo la uzazi,halafu hapo juu unapandwa mti.hiko chombo kimetengenezwa kwa material ambazo zinaoza haraka.Kwa njia hii naona ntakua naendelea kuishi nikiwa kama mti,sababu mti utakula virutubisho vinavyo tokana na kuoza kwa mwili.

Hii itapendeza sana,kwani sasa makaburini kutageuka msituni na kusababisha utengenezwaji wa mvua.

Kwa undani zaidi soma Biodegradable burial pod turns your body into a tree - CNN
170424132824-capsula-mundi-three-eggs-exlarge-169.jpg
 
Mkuu Hili Pia Nilitaka Kulizungumzia

Kuliko kuacha Macho yaoze, Figo zioze, Mapafu yaoze mbona watu wasingekubali kwamba viungo ivi vitolewe sadaka kwa waliohitaji

Lakini kama unavyosema 'IMANI' zimetufunga pia tunaamini kwenye kuzikwa na kuoza na kila kitu

Wazo zuri sana Mkuu
Mkuu! Nimetoa maoni yangu page namba moja umeyapitia?
 
Dunia iliumbwa kwa namna ya pekee sana na namna hiyo ni kurecycle kila kitu kilichopo juu ya mgongo wake.

Binadamu, wanyama au kiumbe hai chochote kinapokufa minyoo wanawahi kuchukua viini lishe na kusambazia ardhi then ardhi inapokea na kuipa mimea ili iistawi na binadamu wengine wale na kurutubisha miili yao. Hivyo kuzika ardhini kunawapa fursa minyoo kusambaza vile viini lishe kwa binadamu waliobaki then maisha yanazidi kustawi Duniani.

Hata mvua hajawahi kuja mvua mpya ...maji ni yale yale kutoka baharini na Kwenye maziwa yanapanda juu kama mvuke then yananyesha baadae kama mvua tena..and the cycle continues.

Hivyo kuzikwa ardhini ndio njia sahihi kabisa ya kuifanya Dunia iwe sustainable maana si ajabu roho ni zile zile zinajirudia Duniani bila kujua maana ukizaliwa unakuwa una kumbukumbu ya unapotoka na kwa vile God ana recycle kila kitu...probably souls and spirits zetu zina reincarnate tu kwa kwenda na kurudi Duniani.

Na tunapohifanyaga tuna akili zaidi kuliko yeye basi anacheeeeka huko enzini!

God is the beste designer and first infinity genius.

Cc the crazy mchokozi Mshana Jr
Umedadavua vizuri kwa kuelezea 'The Recycle in the Ecology' kwamba viumbe tunategemeana katika mazingira

Ila pia kwenye cremation yale majivu yakitupwa baharini samaki wanapata chakula

Kwenye 'reincarnation'aya ni masuala ya kiimani sana na sina elimu sana katika swala hili ila nafiri ata kuyatupa majivu baharini au hewani au msituni ni njia ya kusambaza roho yako (kwa kuzingatia imani sio sayansi)

Ila mkuu; huoni kama tukiacha viungo vyetu vioze tu sio haki na kuna baadhi ya wanaobaki wanavihitaji

Je ingekuwa vizuri 'ku-donate' baadhi ya viungo kama macho,figo au ini kwa wachache waliobaki alafu mwili uliobaki ukachomwa
 
Back
Top Bottom