Je Cremation Ni Mbaya?!

Je Cremation Ni Mbaya?!

Ni wazi kabisa kuwa misiba ya kimagharibi ni gharama mno na inapoteza sana rasilimali,mara mbao sijui vyuma sijui zege yaani ujinga ujinga tu.Mimi nikifa bora tu nichomwe moto,kwanza inasaidia kuokoa maeneo,wenyewe mnaona sikuizi jinsi viwanja vya makaburi vinavyojaa.

Ila kuna wanasayansi wa Italia wamegundua mbinu nyingine ya kuzika maiti,unazikwa kwenye kitu chenye umbo la yai ukiwa umewekwa position ya mtoto kwenye tumbo la uzazi,halafu hapo juu unapandwa mti.hiko chombo kimetengenezwa kwa material ambazo zinaoza haraka.Kwa njia hii naona ntakua naendelea kuishi nikiwa kama mti,sababu mti utakula virutubisho vinavyo tokana na kuoza kwa mwili.

Hii itapendeza sana,kwani sasa makaburini kutageuka msituni na kusababisha utengenezwaji wa mvua.

Kwa undani zaidi soma Biodegradable burial pod turns your body into a tree - CNNView attachment 806217
Nafikiri hapa umeleta nadharia nzuri ya burial...
Mazishi hayafai kuwa gharama na pia yanafaa kutunza Mazingira

Hao wa Italy kwa Mfano wanapunguza matumuzi mabaya ya miti kuchonga majeneza( Umuhimu wa Jeneza Ni Nini) na pia wanatunza mazingira

Mfano Kumzika mtu nyumbani na kutengeneza kaburi kwa zege na mapambo lukuki inaonekana kama tumemuenzi Ndugu yetu ila baadae eneo ili litakuwa gumu kufanya nalo biashara au kuwa pendeleo la watu kuishi

Kwa sasa nafikiri kuchomwa sio vibaya
 
Tatizo ni taratibu za kiimani ambazo tumekua nazo. Mimi kwa mawazo yangu binafsi huwa nawaza nikifa nitoe sadaka viungo ambavyo vinaweza kutumika kwa watu wengine walio hai na kitakachobaki basi kikachomwe tu. Sidhani kama roho ikishatoka kiwiliwili huwa na thamani tena.
Kiungo changu simuachii mtu
Je figo au ini lako akipewa mwanamke malaya ?
Anaenda kudanga huko
 
Umedadavua vizuri kwa kuelezea 'The Recycle in the Ecology' kwamba viumbe tunategemeana katika mazingira

Ila pia kwenye cremation yale majivu yakitupwa baharini samaki wanapata chakula

Kwenye 'reincarnation'aya ni masuala ya kiimani sana na sina elimu sana katika swala hili ila nafiri ata kuyatupa majivu baharini au hewani au msituni ni njia ya kusambaza roho yako (kwa kuzingatia imani sio sayansi)

Ila mkuu; huoni kama tukiacha viungo vyetu vioze tu sio haki na kuna baadhi ya wanaobaki wanavihitaji

Je ingekuwa vizuri 'ku-donate' baadhi ya viungo kama macho,figo au ini kwa wachache waliobaki alafu mwili uliobaki ukachomwa
kudonate viungo Kwa watu wenye nia njema si vibaya

Ila changamoto ni nia ya binadamu inapokuwa haihanurika..mtalazimishana kufa kisa viungo mpige hela.

Na hilo ndio linaloepukwa
 
Mkuu Hili Pia Nilitaka Kulizungumzia

Kuliko kuacha Macho yaoze, Figo zioze, Mapafu yaoze mbona watu wasingekubali kwamba viungo ivi vitolewe sadaka kwa waliohitaji

Lakini kama unavyosema 'IMANI' zimetufunga pia tunaamini kwenye kuzikwa na kuoza na kila kitu

Wazo zuri sana Mkuu
Kabisa mkuu.
 
Dunia iliumbwa kwa namna ya pekee sana na namna hiyo ni kurecycle kila kitu kilichopo juu ya mgongo wake.

Binadamu, wanyama au kiumbe hai chochote kinapokufa minyoo wanawahi kuchukua viini lishe na kusambazia ardhi then ardhi inapokea na kuipa mimea ili iistawi na binadamu wengine wale na kurutubisha miili yao. Hivyo kuzika ardhini kunawapa fursa minyoo kusambaza vile viini lishe kwa binadamu waliobaki then maisha yanazidi kustawi Duniani.

Hata mvua hajawahi kuja mvua mpya ...maji ni yale yale kutoka baharini na Kwenye maziwa yanapanda juu kama mvuke then yananyesha baadae kama mvua tena..and the cycle continues.

Hivyo kuzikwa ardhini ndio njia sahihi kabisa ya kuifanya Dunia iwe sustainable maana si ajabu roho ni zile zile zinajirudia Duniani bila kujua maana ukizaliwa unakuwa una kumbukumbu ya unapotoka na kwa vile God ana recycle kila kitu...probably souls and spirits zetu zina reincarnate tu kwa kwenda na kurudi Duniani.

Na tunapohifanyaga tuna akili zaidi kuliko yeye basi anacheeeeka huko enzini!

God is the beste designer and first infinity genius.

Cc the crazy mchokozi Mshana Jr
Na hili ndilo Jibu Sahihi.
 
Kiuhalisia ni kweli watu wanakufa,ila kwanini kila mtu hufikiri kuwa lazima atakufa?najua sie tuliyo hai tunaona watu wakifa na sie tunajisemea kuwa ipo siku nasi lazima tutakufa,lakini mbona tunaona watu wakiwa mafukara lakini hatusemi kuwa nasi lazima tutakuwa mafukara au tunaona watu waliyopata ulemavu lakini hatusemi nasi tutakuwa walemavu?

Je,kipi kinafanya wote tuone lazima tutakufa(na si vinginevyo) tena bila kujari ni aina gani ya kifo?

Je, huku kufikiri lazima tufe sio imani tu hii?
 
Kiuhalisia ni kweli watu wanakufa,ila kwanini kila mtu hufikiri kuwa lazima atakufa?najua sie tuliyo hai tunaona watu wakifa na sie tunajisemea kuwa ipo siku nasi lazima tutakufa,lakini mbona tunaona watu wakiwa mafukara lakini hatusemi kuwa nasi lazima tutakuwa mafukara au tunaona watu waliyopata ulemavu lakini hatusemi nasi tutakuwa walemavu?

Je,kipi kinafanya wote tuone lazima tutakufa(na si vinginevyo) tena bila kujari ni aina gani ya kifo?

Je, huku kufikiri lazima tufe sio imani tu hii?
Nafikiri kisayansi mwili wa binadamu ni dhaifu na mortal... bacteria, viruses,protozoas..na aina nyingine ya vidudu(microbes) vina uwezo wakuuchukua uhai wa binadamu

Ila kadri navyo binadamu anapozeeka na seli zake zinazeeka,..

Kifo kipo na sio nadharia ya imani lakini ya kiuhalisia na kisayansi
 
kudonate viungo Kwa watu wenye nia njema si vibaya

Ila changamoto ni nia ya binadamu inapokuwa haihanurika..mtalazimishana kufa kisa viungo mpige hela.

Na hilo ndio linaloepukwa
Je ku-donate kwa mwenye nia nzuri akabadilika akawa mwenye nia mbaya

Nafikiri ata kama mtu ana nia mbaya....hamna sadaka kubwa atakuwa anajua anaishia nayo kama kiungo cha mtu

Ebu fikiri ata kama uyo 'Malaya' akajua kwamba izi sio figo zangu...niamini atabadilika
 
Upanga barabara ya Maliki kipande cha kutoka shule ya msingi Muhimbili kwenda juu pale palikuwa makaburi. Kwa kweli kipande kizima kile Upanga kuanzia makaburi ya Tambaza mpaka International School kuna makaburi ya zamani mengi sana pale yamejengewa juu yake. Lakini hiki kipande cha barabara ya Maliki nakiongelea kwa sababu wakati barabara inataka kujengwa palikuwa na makaburi.

Serikali ikafukua makaburi na kuyahamisha.

Maana yake ni kwamba unapozikwa leo, unawazibia nafasi wanaokuja kesho.

Katika kipindi cha miaka 100 kama kila mtu atazikwa hapa duniani, tutajaza sehemu kama nchi nzima ya Gambia kwa makaburi.

Mimi nilishasema kitambo wanichome moto tu. Majivu Long Island Sound.
 
Gharama za mazishi zimekua kubwa kutokana na watu kuiga na hasa mambo ya tamaduni za kimagharibi,
Siku hizi kwenye misiba unakuta mpaka watu wanashona sare! kila mtu akifikwa na msiba atataka anunue jeneza la gharama zaidi ili asionekane yupo nyuma au choka mbaya au asionekane kua hakumthamini marehemu!

Napenda wanavyozikana waislamu,tajiri na masikini wote wanavalishwa sanda na wote wanabebwa kwenye jeneza lile lile kwenda kuzikwa!

Maiti zao hakuna cha kuvalishwa suti za gharama wala viatu vya gharama,wote ni sawa kwa tajiri na masikini,Gharama na mbwembwe zinazotumika kuwazika marehemu hazimsaidii lolote marehemu huko aendako bali matendo yake mema aliyoyafanya wakati wa uhai wake ndio yatakayo msaidia.
 
Zile dawa za kutunzia maiti zina chafua sana underground water,majeneza yanaharibu misitu.Cremation is the to go kwani hata kusafirisha maiti simple,.
 
Nafikiri kisayansi mwili wa binadamu ni dhaifu na mortal... bacteria, viruses,protozoas..na aina nyingine ya vidudu(microbes) vina uwezo wakuuchukua uhai wa binadamu

Ila kadri navyo binadamu anapozeeka na seli zake zinazeeka,..

Kifo kipo na sio nadharia ya imani lakini ya kiuhalisia na kisayansi

Sababua zenye kupelekea kifo zipo nyingi sio hizo tu ambazo wewe umeeleza, lakini pia mtu anaposema kuwa lazima atakufa huwa hafikirii kwamba ni kwa sababu ya maradhi,uzee wala ajari bali huwa anajua tu lazima atakufa.

Uwepo wa kifo ndiyo kweli upo ni kama vile ambavyo ulemavyo nao upo lakini hakuna mwenye kufikiri kuwa lazima atakuwa mlemavu.

Ndiyo maana nasema huku kufikiri lazima tufe(na si vinginevyo) yaweza kuwa ni imani.
 
Back
Top Bottom