Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Hebu tuwe na mjadala tofauti kidogo na huu ugonjwa wa corona maarufu kama COVID19.
Tuanze na tabiri mbali mbali.Kuna machapisho na makala yaliyotabiri huu ugonjwa hapo kabla na sasa imetokea kama utabiri ulivyotabiri
Je, hizi tabiri zilikuwa za kweli ama ni mipango ya muda mrefu ya wale waliotutangulia kufikiri? Kwa maoni yangu tabiri husika zilikuwa sahihi na si mipango ya wachache tunaowahisi kwakuwa wao ndio wahanga wakubwa kwenye hili.. Na kuna maono na nguvu ya ajabu kwenye huu utabiri
Aina za corona
Tunaambiwa kuna aina zisizopungua 20 za corona na karibia kila mtu ana aina mojawapo ya vimelea vya corona. Lakini corona AKA COVID19 ndio ndio mbaya sana na inayoisumbua dunia kwa sasa.. Kwenye utabiri iliitwa COVID19. Na ikatokea mwaka 2019. Je, hii ni coicedence ama ni tukio la kupangwa? Kama ni tukio la kupangwa. Je, ni nani kalipanga? Kwanini? Kwa maslahi gani? Kwanini 2019 na si mwaka mwingine wowote?
Mkanganyiko wa aina ya vimelea. Nimesoma kuna mojawapo ya makala inaelezea huu mkanganyiko kwamba je kimelea chake ni kirusi ama ni bacteria? Je, ni nini kinaeneza kwa njia ya hewa kati ya kirusi na bacteria? Je, ni nini kinaeneza kwa njia ya kushikana kati ya kirusi na bacteria?
Makala za siri zilizovuja
Ukweli ni upi kwamba kirusi/bacteria wa corona kilitengenezwa China kwa nia ya kuwaambukiza waandamanaji wa Kong Kong ili kudhuru ufahamu wao na wapoteane kwa kuugua? Na kwamba Mmarekani alistukia hiyo ishu na kumuomba mchina formula yake kwa matumizi yake ya baadae na mchina akagoma? Lakini mmarekani akatumia ulaghai kupitia majasusi wake na katika harakati za kupata kichupa chenye MBEGU Wachina wakastukia na kwenye kukigombea kikaanguka kikamwagika na kuleta hili janga.
Conspiracy ni nyingi kwenye hili lakini pia tunajua maslahi ya mmarekani pale Hong Kong na hujuma plus figisu anazofanya ili maandamano husika yalete matokeo tarajiwa.
Kutafuta mchawi
Tayari mataifa mawili yenye nguvu kubwa duniani mmarekani na mchina wameshanyoosheana vidole sana.. Kila mmoja akimtuhumu mwenzake kama chanzo na tayari hata kabla hali haijatulia mawakili wa Marekani wameshalimbilia mahakamani kumfungulia mchina shauri la madai ya uzembe na fidia ya dola trillion 20.
Ukweli ni upi kuhusu corona
Kuna vyanzo vinasema wanachougua watu sio corona bali ni kitu kingine kibaya kabisa ila ukweli unafichwa hasa na mchina na wanasema habari zinazoripotiwa ni tofauti kabisa na uhalisia.. Kwa mfano China inasemekana waliokufa ni mamilioni... Rejea mada ya laini million 21 zisizopatikana huko China baaada ya ugonjwa kupiga
Kwasasa ukweli ni vigumu kuujua na itachukua miaka na pengine hata karne pale wahusika watakapojitokeza hadharani na kuomba radhi.. Lakini bythen zitakuwa ni habari mfu
Sasa kitisho ni nini?
Kitisho kikubwa kilichopo mbele yetu sio corona ya sasa bali corona itakayorudi.. Corona inatayokuja kivingine.. Corona itakayobamiza Afrika. Kitisho kikubwa ni hapo mbeleni upgraded COVID19 iliyoboreshwa itakapotumika kama biological weapon. Kama silaha za maangamizi kwa adui.
Pale COVID19 iliyoboreshwa kama silaha ya kivita kwa bei ndogo salama na isiyo na hasara. Tumeshuhudia vifo vinavyofikia mia 800 kwa masaa 24 tuu huko Hispania na Italy. Hii ni idadi kubwa mno ya vifo kwa siku moja kwenye uwanja wa vita inayohitaji vifaa vingi vya kijeshi na hasara kubwa na gharama kubwa.
Kitisho na hofu kubwa ni pale corona iliyoboreshwa formula yake itakapodakwa na magaidi na vichaa wa hii dunia. Kwasasa watu wako busy maabara wakijaribu kutengeneza tiba na kinga ya COVID19. Ni katika mchakato huo bila kujua ama kwa kujua wanaumba kitu kingine kikubwa zaidi kibaya zaidi. Yaani wasumbufu hawatapigwa maroketi tena wala mabomu bali wataangushiwa tu kichupa kidogo chenye vimelea vya corona iliyoboreshwa na baada ya hapo itakuwa tu kuokota maiti.
Corona itarudi baada ya miaka 10. Hapa ndio ule utabiri wa bilionea Bill Gates utatimia. Utabiri wa kuangamiza waafrika million 10 kupitia huu ugonjwa. Na muda huo ukifika watakaokufa kwa wingi sana ni waafrika. Ambao pia ni rahisi mno kuwawekea quarantine wasitoke nje ya bara lao. Wakati huo wenzetu hawa wanaokufa leo kama kuku wa kideri watakuwa wameshajua chanjo na kinga na hawatakuwa tayari kuitoa Afrika na kama watakubali ni kwa masharti magumu mno.
Tuwacheke sasa. Lakini kilio chetu hakiko mbali. Tuziishi hizi nyakati lakini kiama kinakuja. Tukutane 2030
Jr
Tuanze na tabiri mbali mbali.Kuna machapisho na makala yaliyotabiri huu ugonjwa hapo kabla na sasa imetokea kama utabiri ulivyotabiri
Je, hizi tabiri zilikuwa za kweli ama ni mipango ya muda mrefu ya wale waliotutangulia kufikiri? Kwa maoni yangu tabiri husika zilikuwa sahihi na si mipango ya wachache tunaowahisi kwakuwa wao ndio wahanga wakubwa kwenye hili.. Na kuna maono na nguvu ya ajabu kwenye huu utabiri
Aina za corona
Tunaambiwa kuna aina zisizopungua 20 za corona na karibia kila mtu ana aina mojawapo ya vimelea vya corona. Lakini corona AKA COVID19 ndio ndio mbaya sana na inayoisumbua dunia kwa sasa.. Kwenye utabiri iliitwa COVID19. Na ikatokea mwaka 2019. Je, hii ni coicedence ama ni tukio la kupangwa? Kama ni tukio la kupangwa. Je, ni nani kalipanga? Kwanini? Kwa maslahi gani? Kwanini 2019 na si mwaka mwingine wowote?
Mkanganyiko wa aina ya vimelea. Nimesoma kuna mojawapo ya makala inaelezea huu mkanganyiko kwamba je kimelea chake ni kirusi ama ni bacteria? Je, ni nini kinaeneza kwa njia ya hewa kati ya kirusi na bacteria? Je, ni nini kinaeneza kwa njia ya kushikana kati ya kirusi na bacteria?
Makala za siri zilizovuja
Ukweli ni upi kwamba kirusi/bacteria wa corona kilitengenezwa China kwa nia ya kuwaambukiza waandamanaji wa Kong Kong ili kudhuru ufahamu wao na wapoteane kwa kuugua? Na kwamba Mmarekani alistukia hiyo ishu na kumuomba mchina formula yake kwa matumizi yake ya baadae na mchina akagoma? Lakini mmarekani akatumia ulaghai kupitia majasusi wake na katika harakati za kupata kichupa chenye MBEGU Wachina wakastukia na kwenye kukigombea kikaanguka kikamwagika na kuleta hili janga.
Conspiracy ni nyingi kwenye hili lakini pia tunajua maslahi ya mmarekani pale Hong Kong na hujuma plus figisu anazofanya ili maandamano husika yalete matokeo tarajiwa.
Kutafuta mchawi
Tayari mataifa mawili yenye nguvu kubwa duniani mmarekani na mchina wameshanyoosheana vidole sana.. Kila mmoja akimtuhumu mwenzake kama chanzo na tayari hata kabla hali haijatulia mawakili wa Marekani wameshalimbilia mahakamani kumfungulia mchina shauri la madai ya uzembe na fidia ya dola trillion 20.
Ukweli ni upi kuhusu corona
Kuna vyanzo vinasema wanachougua watu sio corona bali ni kitu kingine kibaya kabisa ila ukweli unafichwa hasa na mchina na wanasema habari zinazoripotiwa ni tofauti kabisa na uhalisia.. Kwa mfano China inasemekana waliokufa ni mamilioni... Rejea mada ya laini million 21 zisizopatikana huko China baaada ya ugonjwa kupiga
Kwasasa ukweli ni vigumu kuujua na itachukua miaka na pengine hata karne pale wahusika watakapojitokeza hadharani na kuomba radhi.. Lakini bythen zitakuwa ni habari mfu
Sasa kitisho ni nini?
Kitisho kikubwa kilichopo mbele yetu sio corona ya sasa bali corona itakayorudi.. Corona inatayokuja kivingine.. Corona itakayobamiza Afrika. Kitisho kikubwa ni hapo mbeleni upgraded COVID19 iliyoboreshwa itakapotumika kama biological weapon. Kama silaha za maangamizi kwa adui.
Pale COVID19 iliyoboreshwa kama silaha ya kivita kwa bei ndogo salama na isiyo na hasara. Tumeshuhudia vifo vinavyofikia mia 800 kwa masaa 24 tuu huko Hispania na Italy. Hii ni idadi kubwa mno ya vifo kwa siku moja kwenye uwanja wa vita inayohitaji vifaa vingi vya kijeshi na hasara kubwa na gharama kubwa.
Kitisho na hofu kubwa ni pale corona iliyoboreshwa formula yake itakapodakwa na magaidi na vichaa wa hii dunia. Kwasasa watu wako busy maabara wakijaribu kutengeneza tiba na kinga ya COVID19. Ni katika mchakato huo bila kujua ama kwa kujua wanaumba kitu kingine kikubwa zaidi kibaya zaidi. Yaani wasumbufu hawatapigwa maroketi tena wala mabomu bali wataangushiwa tu kichupa kidogo chenye vimelea vya corona iliyoboreshwa na baada ya hapo itakuwa tu kuokota maiti.
Corona itarudi baada ya miaka 10. Hapa ndio ule utabiri wa bilionea Bill Gates utatimia. Utabiri wa kuangamiza waafrika million 10 kupitia huu ugonjwa. Na muda huo ukifika watakaokufa kwa wingi sana ni waafrika. Ambao pia ni rahisi mno kuwawekea quarantine wasitoke nje ya bara lao. Wakati huo wenzetu hawa wanaokufa leo kama kuku wa kideri watakuwa wameshajua chanjo na kinga na hawatakuwa tayari kuitoa Afrika na kama watakubali ni kwa masharti magumu mno.
Tuwacheke sasa. Lakini kilio chetu hakiko mbali. Tuziishi hizi nyakati lakini kiama kinakuja. Tukutane 2030
Jr