Je, CCM kuingilia uhuru wa Bunge, imevunja katiba?

Mkandara:

Watu hatusomi katiba na kuzielewa. Mkutano wa NEC hauna makosa yoyote kikatiba kwa sababu moja kubwa.

Mbunge anachaguliwa akiwa ni mwanachama wa chama cha kisiasa. Hivyo akifukuzwa au akiacha uanachama wa chama chake basi anakuwa amepoteza ubunge wake.

Na katiba ya CCM inasema kuwa kazi moja ya NEC ni kungalia kuwa viongozi wa CCM wanafuata na kutimiza agenda za chama. Hivyo kama watu walikuwa wana malalamiko kuhusu Sitta, NEC ni sehemu mwafaka kusikilizwa malalamiko hayo. Na baada ya kusikiliza NEC inaweza kutoa hatua za kichama.

Na kama hatua ya NEC itakuwa ni kumfuta mbunge au kiongozi uanachama, basi automatically sheria nyingine za katiba ya nchi zitafuatia. Kama vile kupoteza madaraka.

Kwa mfano Mrema aliporudisha kadi yake ya CCM, alipoteza ubunge.

Hivyo msikae hapa mnapiga kelele wakati hizo ni taratibu za CCM. Kolimba, Kitine waliitwa kwenye vikao vya NEC. Hivyo hii sio mara ya kwanza.


Mzee kujadili mwenendo wa Bunge na kutaka kuzima hoja zinazo itafuna Nchi ndiyo issue hapa mengine haya ni yao wenyewe CCM.Ila kulikemea Bunge na hata kumkata speaker kuwaumiza wapinzani na hoja zao ni kazi ya NEC ya CCM ?
 
Mimi sidhani hili la CCM kuzungumza na wabunge wake lina uhusiano wowote na katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. CCM inayotaratibu zake za ndani ya chama ambazo wanachama wa chama hiki wanaongozwa wakati wote.
Sungi,
Nashukuru umeanza na kusema "mimi sidhani". Issue hapa ni Ibara ya 100 ya Katiba, inayotamka bayana kuwa mijadala ndani ya Bunge haitahojiwa na "chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano.." Hata mahakama imenyimwa haki hiyo, ndiyo maana Kanuni za Bunge zinatoa utaratibu wa ndani ya Bunge. Unless unataka kusema "Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) siyo "chombo". Pili, unapowataka wafunga mdomo wabunge, ni udikteta wa ajabu. Wabunge jukumu lao ndani ya Bune siyo kulinda maslahi ya Chama, bali kwanza maslahi ya Taifa kwa mujibu wa dhamira zao. Huu ndio msingi wa hoja, hivyo siyo swala la "kudhani" bali ni matakwa ya Katiba ni nini, na nini kwanini Ibara hiyo iliwekwa.
 
Mzee kujadili mwenendo wa Bunge na kutaka kuzima hoja zinazo itafuna Nchi ndiyo issue hapa mengine haya ni yao wenyewe CCM.Ila kulikemea Bunge na hata kumkata speaker kuwaumiza wapinzani na hoja zao ni kazi ya NEC ya CCM ?

CCM hawajafanya kitu chochote kile nje ya katiba. CHADEMA au CUF wangekuwa madarakani wangeweza kufanya yale yanayofanywa na CCM.

Hivyo mapungufu yanayojitokeza hapa ni mapungufu ya kikatiba.
 
Mkuu tuwe makini ktk hili hapa kwani tusije kumjengea ngao kubwa speaker Sitta..
Ebu nikupe mfano nje ya mada hii kidogo.. tuseme Chadema ndio wameshinda na kumchagua Spika wa bunge ambaye
Hivi kweli mnataka kusema Sitta angekuwa mbunge na spika wa Chadema na akafanya kinyume cha chama kwa kukataa kabisa mada zinazohusiana na Mafisadi kusimamishwa kinyume cha wabunge wa Chadema....basi Uongozi wa Chadema ungekuwa hauna haki kumsimamisha Uongozi Spika huyo kwa sababu analindwa na katiba ya nchi?..Meaning hivi leo Spika Sitta angekuwa anafanya kama Mafisadi wanavyotaka tungekuwa hatuna sheria ya kumwajibisha!..
Mkuu soma kipengele cha pili kinatanguliwa na maneno haya:- Bila ya kuahiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika..
Wana JF,
Kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, ingelikuwa CCM inahitaji kumwajibisha Spika ambaye ametokana na Chama chao, wangeliweza kabisa kumshughulikia kupitia "Kamati ya Chama inayotambuliwa na Kanuni ya Bunge" Baada ya kukubaliana ndani ya Kamati ya Wabunge wa CCM, wanaanzisha motion ya kutokuwa na Imani na Spika. Kwa njia hiyo, Ibara ya 100 itakuwa salama, kwa sababu tutakuwa ndani ya utaratibu uliowekwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano, na kuwekewa utaratibu ndani ya Kanuni ya Bunge. Hoja hizo zingelikuwa zimebaki ndani ya Bunge bila kutoka nje ya Bunge.
 
Mkuu tuwe makini ktk hili hapa kwani tusije kumjengea ngao kubwa speaker Sitta..
Ebu nikupe mfano nje ya mada hii kidogo.. tuseme Chadema ndio wameshinda na kumchagua Spika wa bunge ambaye
Hivi kweli mnataka kusema Sitta angekuwa mbunge na spika wa Chadema na akafanya kinyume cha chama kwa kukataa kabisa mada zinazohusiana na Mafisadi kusimamishwa kinyume cha wabunge wa Chadema....basi Uongozi wa Chadema ungekuwa hauna haki kumsimamisha Uongozi Spika huyo kwa sababu analindwa na katiba ya nchi?..Meaning hivi leo Spika Sitta angekuwa anafanya kama Mafisadi wanavyotaka tungekuwa hatuna sheria ya kumwajibisha!..
Mkuu soma kipengele cha pili kinatanguliwa na maneno haya:- Bila ya kuahiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika..

Mkuu Mkandara, somehow you are failing to look at the bigger picture and you are actually trying to personalize an issue that is obviously of a much much bigger public interest and concern.

Sisi wengine tunaliangalia hili swali kama linahusu zaidi heshima ya Ofisi ya Spika wa Bunge na majukumu ya wawakilishi wa wananchi wanapokuwa Bungeni bila kujali itikadi zao. Kitendo cha NEC ya CCM kujaribu kuingilia mijadala na maamuzi ya Bunge na kuwaziba midomo wa bunge kwa kisingizio cha kulinda maslahi ya CCM ni dhambi kubwa inayotakiwa ilaaniwe na wote wanaoitakia mema taifa.

Ukiangalia kwa makini utagundua kwamba hawa wajumbe wa NEC wanalichukulia Bunge kama subordinate ya CCM - hali hii tuliwahi kuwa nayo wakati wa mfumo wa chama kimoja kushika hatamu. CCM ndio iliyokuwa serikali, Bunge na Mahakama vyote kwa pamoja kwa sababu sifa kuu ya kuongoza hivi vyombo ilikuwa ni kuwa kada wa CCM mwenye kadi.

Pamoja na kwamba tuko kwenye mfumo wa vyama vingi, ujinga wa CCM kushika hatamu bado umewajaa wana CCM. Haya ni mawazo ya kijeuri, kipumbavu na ya dharau kubwa kwa wananchi (milioni 40) walioshiriki katika kuwachagua wawakilishi wao bungeni. Hakuna kipengele chochote ndani ya katiba kinachomtaka Spika apatikane kupitia vyama vya siasa tu iwe CCM, Chadema au CUF.

Uhuru wa Bunge lazima ulindwe kwa gharama zozote zile - bila hivyo hatufiki.
 
Sungi,
Nashukuru umeanza na kusema "mimi sidhani". Issue hapa ni Ibara ya 100 ya Katiba, inayotamka bayana kuwa mijadala ndani ya Bunge haitahojiwa na "chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano.." Hata mahakama imenyimwa haki hiyo, ndiyo maana Kanuni za Bunge zinatoa utaratibu wa ndani ya Bunge. Unless unataka kusema "Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) siyo "chombo". Pili, unapowataka wafunga mdomo wabunge, ni udikteta wa ajabu. Wabunge jukumu lao ndani ya Bune siyo kulinda maslahi ya Chama, bali kwanza maslahi ya Taifa kwa mujibu wa dhamira zao. Huu ndio msingi wa hoja, hivyo siyo swala la "kudhani" bali ni matakwa ya Katiba ni nini, na nini kwanini Ibara hiyo iliwekwa.

Dr. W. Slaa:

Ni katiba hiyohiyo inayosema kuwa mbunge ni lazima awe mwanachama wa chama cha kisiasa. Na anapopoteza uanachama wake, automatically anapoteza ubunge wake.

Hivyo basi mbunge yoyote hana uhuru zaidi ya yale yanayokubaliwa na chama chake.

Hivyo sio CCM inayoleta udikteta bali ni katiba yenyewe. Kwa sasa hivi una uhuru wa kuzungumza kwa sababu upo chama cha upinzani. Lakini CHADEMA ikipata madaraka kwa kutumia katiba ya CCM ni uhakika mta-exercise yanayofanywa na CCM sasa ya kufunga watu midomo.
 
Mkuu Mkandara, somehow you are failing to look at the bigger picture and you are actually trying to personalize an issue that is obviously of a much much bigger public interest and concern.

Sisi wengine tunaliangalia hili swali kama linahusu zaidi heshima ya Ofisi ya Spika wa Bunge na majukumu ya wawakilishi wa wananchi wanapokuwa Bungeni bila kujali itikadi zao. Kitendo cha NEC ya CCM kujaribu kuingilia mijadala na maamuzi ya Bunge na kuwaziba midomo wa bunge kwa kisingizio cha kulinda maslahi ya CCM ni dhambi kubwa inayotakiwa ilaaniwe na wote wanaoitakia mema taifa.

Ukiangalia kwa makini utagundua kwamba hawa wajumbe wa NEC wanalichukulia Bunge kama subordinate ya CCM - hali hii tuliwahi kuwa nayo wakati wa mfumo wa chama kimoja kushika hatamu. CCM ndio iliyokuwa serikali, Bunge na Mahakama vyote kwa pamoja kwa sababu sifa kuu ya kuongoza hivi vyombo ilikuwa ni kuwa kada wa CCM mwenye kadi.

Pamoja na kwamba tuko kwenye mfumo wa vyama vingi, ujinga wa CCM kushika hatamu bado umewajaa wana CCM. Haya ni mawazo ya kijeuri, kipumbavu na ya dharau kubwa kwa wananchi (milioni 40) walioshiriki katika kuwachagua wawakilishi wao bungeni. Hakuna popote kwenye inayomtaka Spika apatekane kupitia vyama vya siasa iwe CCM, Chadema au CUF.

Uhuru wa Bunge lazima ulindwe kwa gharama zozote zile - bila hivyo hatufiki.

Ahsante sana Mag3, nakubaliana kabisa na point yako hapo juu.
 
Dr. W. Slaa:

Ni katiba hiyohiyo inayosema kuwa mbunge ni lazima awe mwanachama wa chama cha kisiasa. Na anapopoteza uanachama wake, automatically anapoteza ubunge wake.

Hivyo basi mbunge yoyote hana uhuru zaidi ya yale yanayokubaliwa na chama chake.

Hivyo sio CCM inayoleta udikteta bali ni katiba yenyewe. Kwa sasa hivi una uhuru wa kuzungumza kwa sababu upo chama cha upinzani. Lakini CHADEMA ikipata madaraka kwa kutumia katiba ya CCM ni uhakika mta-exercise yanayofanywa na CCM sasa ya kufunga watu midomo.
Zakumi,
Nadhani bado tumeshindwa kutenganisha mambo mawili. La kwanza, ni Ibara ya 100 ambayo inaweka kinga kwa mambo specific. Hayo hayatahojiwa popote. Sikusema popote, kuwa Mbunge ana kinga absolute kwa kila kitu. Ana kinga absolute, kwa hoja zilizotolewa ndani ya Bunge. Hoja, mawazo au majadiliano hayo ndiyo hayatahojiwa kwenye chombo kinginge chochote. Akivunja maadili ya Chama katika mambo mengine, hana Kinga yeyote.
Pili, Swala la Spika kuwa kwenye Kamati Kuu ya CCM au NEC ni la Katiba ya CCM. This is contrary to good practice in a democratic system. Nimekuwa nikitoa mfano kila mara kuwa Timu ya Mpira ya Tanzania ikicheza na Kenya, na Referee akatoka Kenya, na Referee huyo wakati wa pumziko akajifungia kwenye chumba cha mapumziko na Timu yake ya Kenya (and vice Versa), utategemea nini ( hata angelitaka kuonekana impartial, impression ya kawaida ni kuwa anapendelea). Kwa wenzetu, mtu akichaguliwa Spika anajiuzulu nafasi zake zote kwenye chama chake( wengine hujiuzulu hata kiti cha Jimbo na jimbo linakuwa vacant) ili aonekane kweli ni Referee kwa wote. Nchi kadhaa ambako culture ya impartiality imekuwa developed to a high degree, anabaki kwenye nafasi yake lakini anachunga kweli impartiality in its real sense. Kanuni ya 8 ya Kanuni za Bunge, Toleo la 2007 zinamtaka Speaker au Naibu Speaker asijihusishe na upande wowote, jambo ambalo kimatendo ni vigumu iwapo umebeba nafasi zote za chama ikiwa ni pamoja na kuwa mlezi wa Mkoa( ambapo uwezekano wa ku - clash na wabunge wako).
 
Dr. W. Slaa:

Ni katiba hiyohiyo inayosema kuwa mbunge ni lazima awe mwanachama wa chama cha kisiasa. Na anapopoteza uanachama wake, automatically anapoteza ubunge wake.

Hivyo basi mbunge yoyote hana uhuru zaidi ya yale yanayokubaliwa na chama chake.

Hivyo sio CCM inayoleta udikteta bali ni katiba yenyewe. Kwa sasa hivi una uhuru wa kuzungumza kwa sababu upo chama cha upinzani. Lakini CHADEMA ikipata madaraka kwa kutumia katiba ya CCM ni uhakika mta-exercise yanayofanywa na CCM sasa ya kufunga watu midomo.


Zakumi
Unajua wabunge wale wa CCM huwa hawachuliwi na wana CCM pekee yao ? Iweje sasa bada ya kuchaguliwa wana anza tabia ta Chama kwanza na kuacha watu wao majimboni ? Nini nafasi ya wapiga kule majimboni ndani ya NEC yao ? Wananchi nadhani wamesha jionea watauliza maswali haya mwaka 2010 na nadhani Watanzania hawatataka kuwachagua watu wa kwenda kufanya yale iyatalayo NEC ya CCM na huu ndiyo mwanzo wa kuiondoa madaraka .Wamevunja katiba straight katika hili .Badala ya kubisha kasome uone ibara ya 100 inasemaje .Soma ibara ya 100 (1) na (2) na ibara ya 101
 
Wana JF,
Kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, ingelikuwa CCM inahitaji kumwajibisha Spika ambaye ametokana na Chama chao, wangeliweza kabisa kumshughulikia kupitia "Kamati ya Chama inayotambuliwa na Kanuni ya Bunge" Baada ya kukubaliana ndani ya Kamati ya Wabunge wa CCM, wanaanzisha motion ya kutokuwa na Imani na Spika. Kwa njia hiyo, Ibara ya 100 itakuwa salama, kwa sababu tutakuwa ndani ya utaratibu uliowekwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano, na kuwekewa utaratibu ndani ya Kanuni ya Bunge. Hoja hizo zingelikuwa zimebaki ndani ya Bunge bila kutoka nje ya Bunge.


Jamani tuacheni kupiga kupiga michapo, some action is needed here...Can someone confirm kwamba: Kweli Katiba imekiukwa hivyo kitendo cha NEC kumchokonoa na kumtishia Spika ni kosa la Jinai?

Kama ni Ndio: What should happen, and who should help us all to execute the right thing to restore the dignity and uphold the rule of law as enforced by our katiba?

Kama kweli hii kitu ni kosa kikatiba, tukiliacha kutakuwa tuna set a very bad precedence! We must correct, and correct it within this year!
 
Jamani tuacheni kupiga kupiga michapo, some action is needed here...Can someone confirm kwamba: Kweli Katiba imekiukwa hivyo kitendo cha NEC kumchokonoa na kumtishia Spika ni kosa la Jinai?

Kama ni Ndio: What should happen, and who should help us all to execute the right thing to restore the dignity and uphold the rule of law as enforced by our katiba?

Kama kweli hii kitu ni kosa kikatiba, tukiliacha kutakuwa tuna set a very bad precedence! We must correct, and correct it within this year!


Kama ni kweli Mnyoofu ni kwamba kama Katiba imekiukwa na ushahidi ni huo wa kuhoji madaraka ya Bunge , pamoja na kuwa na tume ya uchaguzi huru basi Tundu Lissua apige hodi Mahakama kuu tutamchangia nauli na hata pesa ya kukla wakati anatafuta haki za watanzania .Am I correct ?
 
- NEC ya CCM kumshambulia Spika kwa maamuzi anayoyafanya bungeni ni kuvuruga katiba ya jamhuri, pamoja na sababu zingine za kikatiba Spika wa bunge huchaguliwa na wabunge wote wa pande mbili, kuna wa upinzani ambao huwa wana-cross the line na kumchagua Spika wa CCM, kwa hiyo huyu sio Spika wa CCM tu ila ni wa Jamhuri,

- NEC wako wrong, kama wanataka kumnyang'anya Spika uananchama wa CCM, basi iwe kwa kutofuata maadili ya chama, lakini hawawezi specifically na publicly wakadai kwamba ni kwa sababu anakiumiza chama chao bungeni, hapo Spika anazo haki zote kikatiba kuwahi kwenye mkono wa sheria na sheria itamrudishia Uspika wake, bungeni.

Na this is only a matter of common sense tu, hahiitaji kusoma anything kuelewa this argument kwamba ni politically valid.

Respect.

Field Marshall Es!
 
- NEC ya CCM kumshambulia Spika kwa maamuzi anayoyafanya bungeni ni kuvuruga katiba ya jamhuri, pamoja na sababu zingine za kikatiba Spika wa bunge huchaguliwa na wabunge wote wa pande mbili, kuna wa upinzani ambao huwa wana-cross the line na kumchagua Spika wa CCM, kwa hiyo huyu sio Spika wa CCM tu ila ni wa Jamhuri,

- NEC wako wrong, kama wanataka kumnyang'anya Spika uananchama wa CCM, basi iwe kwa kutofuata maadili ya chama, lakini hawawezi specifically na publicly wakadai kwamba ni kwa sababu anakiumiza chama chao bungeni, hapo Spika anazo haki zote kikatiba kuwahi kwenye mkono wa sheria na sheria itamrudishia Uspika wake, bungeni.


Field Marshall Es!

CCM hawatamfukuza uanachama wala kufukuza u-spika FOR NOW!ishu hii watanzania wengi wameshaisoma
 
Mimi sidhani hili la CCM kuzungumza na wabunge wake lina uhusiano wowote na katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. CCM inayotaratibu zake za ndani ya chama ambazo wanachama wa chama hiki wanaongozwa wakati wote.

Mmmh!

Spika wa bunge hawekwi chini kitako na chama chochote cha siasa, kwa sababu yeye ni kiongozi wa muhimili mmoja muhimu unao unda serikali.
Kisheria CCM wamefanya Uhuni wa hali juu kuropoka kwamba Spika hawasaidii, wamefanya hivyo kwa sababu siku zote CCM wanajikweza na kudhani wako juu ya sheria.

Kundi pekee la Watanzania wenye Haki( Sheria ) ya kumuweka Kidako Spika wa Bunge ni Wabunge wenyewe.

Hiki kinachofanywa na CCM sasa hivi ni ununda wa kuvurunda mambo ili mradi wao haramu wa kushika hatamu ufanikiwe.

CCM sasa hivi wanapambana na kila mtu kila kitu na zaidi wanapambana wenyewe kwa wenyewe, ni Timbilitimbili(Kinyalu) hajulikani nani Mume nani mke humo mwenye ndani ya CCM.
Kila mtu anasimamisha Du!

Wamefikia ile Stage Wazungu wanaita " FAT AND HAPPY"
 
Sungi,
Nashukuru umeanza na kusema "mimi sidhani". Issue hapa ni Ibara ya 100 ya Katiba, inayotamka bayana kuwa mijadala ndani ya Bunge haitahojiwa na "chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano.." Hata mahakama imenyimwa haki hiyo, ndiyo maana Kanuni za Bunge zinatoa utaratibu wa ndani ya Bunge. Unless unataka kusema "Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) siyo "chombo". Pili, unapowataka wafunga mdomo wabunge, ni udikteta wa ajabu. Wabunge jukumu lao ndani ya Bune siyo kulinda maslahi ya Chama, bali kwanza maslahi ya Taifa kwa mujibu wa dhamira zao. Huu ndio msingi wa hoja, hivyo siyo swala la "kudhani" bali ni matakwa ya Katiba ni nini, na nini kwanini Ibara hiyo iliwekwa.

Dr. Slaa,
Neno "chombo" katika Art.100 ya Katiba yetu inamaanisha vyombo (branches) vitatu vinavyotajwa na Katiba - Bunge (Parliament), Rais (Executive) na Mahakama (Judiciary). Art.100 ni mojawapo ya "checks and balance" tool iliyowekwa na Katiba kulinda upekee wa hivi vyombo vitatu. NEC sio chombo kulingana na maana ya "chombo" katika Ibara 100 ya Katiba. Ndio maana, comment yangu ya awali ni ya bado ya msingi. Sub article (2) ya ibara hii inaendelea kukaza uhuru wa mbunge kutoa maoni bila la hofu ya kushtakiwa mahakamani kwa lolote atakalolisema akiwa kwenye vikao vya Bunge.
 
Dr. Slaa,
Mkuu wangu mimi nipo ktk kuuliza zaidi ili swala hili liwe wazi kwa sisi wote. Umesema Ibara ya 100 ya katiba ya Jamhuri inakataza kuhojiwa kwa mijadala ya Bunge na chombo chochote.. sawa nakubali lakini je, kuna mjadala au hoja yoyote ya Bungeni iliyojadiliwa na Kikao hicho cha CCM?..ama walimjadili Spika ktk Utendaji kazi wake na sii hoja, muswada ila mtazamo wa baadhi wabunge kuwa anakiuka sheria za chama kwa kuchukua upande wa wapinzani..ndio maana nauliza kuwa hivi Spika angekuwa upande wa Mafisadi ni wakati gani chama kinatakiwa kumjadili Spika nje ya Bunge.. Na let's say mkitaka motion of no confidance mafisadi wanaipinga pia.. where do we go from here!
Na statement kama za wajumbe wanaosema Spika anawaunga mkono wapinzani nadhani hii ni slaha kubwa kwa vyama vya Upinzani kwani yaonyesha wazi swala la Ufisadi ni nguzo ya Upinzani na CCM ipo ktk kuji defend!.. ushindi wenu hapa mkuu wangu, nukuu kama hizi ni matunda kwa Chadema.
Mkuu wangu nasema hivi kwa sababu ya huko tulikotoka, mfano mzuri ni Mkapa na mashtaka yote yanayomkabili yanalindwa na katiba (according to..) na kama ujuavyo, wewe mwenyewe umekwama kutokana na Bunge kutoafiki hoja yako na hawawezi kukuunga mkono..Sote tumebakia kushika matama wakati mzee mzima akistaafu na mabillioni..
Bahati nzuri Spika yupo upande wetu na tutaendelea kumtetea lakini what if ingekuwa kinyume, sio ndio ya Mkapa tena hayo!
 
Dr. Slaa,
Mkuu wangu mimi nipo ktk kuuliza zaidi ili swala hili liwe wazi kwa sisi wote. Umesema Ibara ya 100 ya katiba ya Jamhuri inakataza kuhojiwa kwa mijadala ya Bunge na chombo chochote.. sawa nakubali lakini je, kuna mjadala au hoja yoyote ya Bungeni iliyojadiliwa na Kikao hicho cha CCM?..ama walimjadili Spika ktk Utendaji kazi wake na sii hoja, muswada ila mtazamo wa baadhi wabunge kuwa anakiuka sheria za chama kwa kuchukua upande wa wapinzani..ndio maana nauliza kuwa hivi Spika angekuwa upande wa Mafisadi ni wakati gani chama kinatakiwa kumjadili Spika nje ya Bunge..

Mkuu Mkandara, unaelewa nini Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, John Chiligati, anapotamka maneno kama haya
Bunge limeanza kuwa kama mchezo wa (kikundi cha televisheni cha vichekesho) The Comedy na kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele.
Kama huku si kuonyesha dharau kwa Bunge, ni kitu gani ? Bunge si la CCM peke yake, ni la Umma wa watanzania wote na Spika si wa Bunge la CCM, ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania.

Wanaoropoka ovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo limejiona kama ni wateule wa kuzungumzia sakata hilo (la ufisadi) bila ya kujua wabunge wote wana haki ya kuzungumzia suala hilo, lakini kwa utaratibu tena kwa kupitia katika vikao vya kamati za wabunge.
Hapa wanaongelea utaratibu wa Bunge au utaratibu wa CCM. Vyovyote vile tamko hili peke yake ni ukiukwaji mkubwa wa sheria ambao Bunge lazima limwajibishe yeyote yule aliyelitoa.
Mbunge anawakilisha wote - CCM na wasio CCM, and that's the bottomline.
Walioropoka ovyo kama walevi ni wajumbe wa NEC ya CCM.
 
Dr. Slaa,
Mkuu wangu mimi nipo ktk kuuliza zaidi ili swala hili liwe wazi kwa sisi wote. Umesema Ibara ya 100 ya katiba ya Jamhuri inakataza kuhojiwa kwa mijadala ya Bunge na chombo chochote.. sawa nakubali lakini je, kuna mjadala au hoja yoyote ya Bungeni iliyojadiliwa na Kikao hicho cha CCM?..ama walimjadili Spika ktk Utendaji kazi wake na sii hoja, muswada ila mtazamo wa baadhi wabunge kuwa anakiuka sheria za chama kwa kuchukua upande wa wapinzani..ndio maana nauliza kuwa hivi Spika angekuwa upande wa Mafisadi ni wakati gani chama kinatakiwa kumjadili Spika nje ya Bunge.. Na let's say mkitaka motion of no confidance mafisadi wanaipinga pia.. where do we go from here!
Na statement kama za wajumbe wanaosema Spika anawaunga mkono wapinzani nadhani hii ni slaha kubwa kwa vyama vya Upinzani kwani yaonyesha wazi swala la Ufisadi ni nguzo ya Upinzani na CCM ipo ktk kuji defend!.. ushindi wenu hapa mkuu wangu, nukuu kama hizi ni matunda kwa Chadema.
Mkuu wangu nasema hivi kwa sababu ya huko tulikotoka, mfano mzuri ni Mkapa na mashtaka yote yanayomkabili yanalindwa na katiba (according to..) na kama ujuavyo, wewe mwenyewe umekwama kutokana na Bunge kutoafiki hoja yako na hawawezi kukuunga mkono..Sote tumebakia kushika matama wakati mzee mzima akistaafu na mabillioni..
Bahati nzuri Spika yupo upande wetu na tutaendelea kumtetea lakini what if ingekuwa kinyume, sio ndio ya Mkapa tena hayo!

MH Mkandara, natanguliza heshima.

Kumjadili Spika katika utendaji wake wa kazi na si hoja?
Ni sawa na kuitukana kanzu bila kumtukana aliyeivaa.

Spika kazi yake kubwa ni kuhakikisha Bunge linaendeshwa kwa kanuni.

Hapo bado kabisa hakuna chombo kinachoweza kuhoji jinsi spika anavyoendesha kazi yake zaidi ya Wabunge na kamati zake.
Utendaji wake wa kazi- Yaani namna Spika aliendeshavyo Bunge ambalo kazi yake kubwa ni kuchambua miswada na kutunga sheria.

Spika kazi yake ina uhusiano wa 100% na Hoja zote za Bungeni.
huwezi kutenga utendaji kazi wa Spika na Hoja za Bunge.
Ukijadili utendaji wa Spika umejadili usimamiaji wake wa hoja na kwa lugha ya moja kwa moja umejadili hoja.
Ukimpa Spika mwongozo wa kufanya kazi yake ni sawa kabisa na kuingilia shughuli za kila siku za Spika na Bunge.
Ukijadili chochote afanayacho Spika wa Bunge unaingilia utendaji wa Spika na Bunge kwa ujumla.

CCM wamejadili utendaji wa Spika kwa maana hiyo wamejadili namna Spika asimamiavyo mwenendo wa hoja Bungeni, kisheria wameingilia mijadala ya bunge kwa mlango wa KIA( Chai Maharage) na huo ni Utovu wa nidhamu na Jinai kwa pamoja.

CCM wana nafasi moja ya kumbana Spika nayo ni kupitia katika vikao vya Wabunge wa CCM tu, na bado kumbana huko kunakuwa kwa ndani kwa ndani na si rasmi kitaifa. Ni sawa sawa kabisa na ukweli kwamba ukiwa balozi wa nyumba 10 kisha mkeo akakuramba makofi huko chumbani usiku kwa usiki tena kimya kimya na kukupa msimamo wa hukumu kisha kesho yake ukaonyesha unyenyekevu wakati wa kuhukumu kesi ya ugoni inayomuhusu shoga yake.Mkeo anakuwa amekubana vizuri kwa kutumia mazingira na hali halisi.
Mkeo huyo huyo hana haki ya kukupa kibano hadharani na kukuambia hana imani na wewe kwa namna ushughulikiavyo kesi zinazohusu mashoga zake wagoni.

CCM wametulea mambo yao ya Chumbani wakati masikio yetu hayana nafasi ya kusikiliza uchuro wao.
 
CCM hawa ni walevi kabisa; wanasahau kuwa spika siyo lazima awe mwanachama wa chama chochote cha siasa. Anachotakiwa ni kuwa mtanzania mwenye akili timamu na acaheguliew na wabunge.
 
Mimi sidhani hili la CCM kuzungumza na wabunge wake lina uhusiano wowote na katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. CCM inayotaratibu zake za ndani ya chama ambazo wanachama wa chama hiki wanaongozwa wakati wote.

Kwa hiyo kama wanataratibu zao za ndani ndiyo wanasahau kuwa mpaka kufika humo ndani wamepitia mlangoni na katiba ni mlango wa kila kitu ukivunja mlango unakaribisha kila aina ya shaka ndani maana utakuwa huna kinga tena dhidi ya hatari zitazokuja kwa kutokea nje.

CCM haiwezi kuwa na taratibu zake zinazopingana na taratibu zilizowaweka hapo (Katiba).
 
Last edited:
Back
Top Bottom