Waberoya
Platinum Member
- Aug 3, 2008
- 15,157
- 10,816
Safi FMES; naona maoni yako yanaweza kupigiliwa msumari kama huu
Kama tunataka kuikoa nchi yetu haraka iwezekanavyo, tusimuonee aibu yeyote yule ambaye anakuwa kikwazo. Awe CHADEMA, CUF, CCM etc., ni nchi yetu iliyowekwa mhanga hivi sasa.
Tunavyoendelea kuiachia nchi kwenye mikono ya manyang'au ndio itakavyokuwa vigumu zaidi kuikomboa. Lakini kama tukiendelea tu kuwapigia makofi watu wabovu kwa vile tu ni wa chama unachokishabikia, tusije tukajilaumu nchi ikibaki mikononi mwa JK na timu yake milele.