Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 24,621
- 43,890
Mpendwa Baba Askofu, Dr.Alex Malasusa (Honoris causa), nchi yetu imeshuhudia tukio baya zaidi kuwahi kutokea katika historia. Tukio la kushambuliwa kwa Katibu Mkuu wa baraza la Maaskofu, Fr.Dr.Charles Kitima (PhD). Baada ya tukio hilo viongozi mbalimbali wa kidini wametoa kauli za kulaani na kuitaka serikali ichukue hatua. Lakini hatujaona tamko rasmi la KKKT kukemea tukio hili la kishetani.
Kwa kuwa kanisa letu ni la Kiinjili ambalo msingi wake ni haki, tunaomba kusikia msimamo wako kama Mkuu wa Kanisa. Kwa kuzingatia kwamba KKKT ni Kanisa la pili kwa ukubwa nchini likiwa na waumini milioni 10.8 (kwa mujibu wa The Lutheran World Federation | The Lutheran World Federation), likitanguliwa na Kanisa Katoliki lenye waumini milioni 18, dunia inataka kusikia KKKT tunasimama wapi katikati ya uovu mkubwa namna hii.
Soma Pia: Padri Kitima ashambuliwa na watu wasiojulikana. Inadaiwa hali yake ni mbaya
Tunaamini kwamba ukiwa kama Mkuu wa Kanisa utatoa tamko kali la kukemea, kulaani na kutoa maelekezo ya nini kifanyike ili jambo hili baya lisijirudie tena katika nchi yetu. Sola Christus, Sola Scriptura, Sola Fide, Sola Gratia (Kristo tu, Neno tu, Imani tu, Neema tu).!
Kwa kuwa kanisa letu ni la Kiinjili ambalo msingi wake ni haki, tunaomba kusikia msimamo wako kama Mkuu wa Kanisa. Kwa kuzingatia kwamba KKKT ni Kanisa la pili kwa ukubwa nchini likiwa na waumini milioni 10.8 (kwa mujibu wa The Lutheran World Federation | The Lutheran World Federation), likitanguliwa na Kanisa Katoliki lenye waumini milioni 18, dunia inataka kusikia KKKT tunasimama wapi katikati ya uovu mkubwa namna hii.
Soma Pia: Padri Kitima ashambuliwa na watu wasiojulikana. Inadaiwa hali yake ni mbaya
Tunaamini kwamba ukiwa kama Mkuu wa Kanisa utatoa tamko kali la kukemea, kulaani na kutoa maelekezo ya nini kifanyike ili jambo hili baya lisijirudie tena katika nchi yetu. Sola Christus, Sola Scriptura, Sola Fide, Sola Gratia (Kristo tu, Neno tu, Imani tu, Neema tu).!