Je, Anthony Edwards ndio Next NBA Legend?

kali linux

JF-Expert Member
May 21, 2017
2,188
5,668
1716323894311.png

Hello bosses and roses, it has been a while...

Leo ngoja nimuongelee huyu kinda wa NBA kwa jina la Antony Edwards au Ant-Man, dogo wa 2001 tu hapa anaekipiga kwenye team ya Minnesota TImberwolves.

Huyu dogo ni hatari, kama umefuatilia NBA playoffs utaona kaongoza timu yake kuingia semi-final kwa mara ya kwanza in 20 years lkn pia kaongoza timu yake ishinde hizo semi-finals na kuingia final kwa mara ya kwanza kabisa toka timu ya wolves ianzishwe.

Huyu dogo ana energy fulani hivi kama alokua nayo marehemu Kobe Bryant, lakini pia uchezaji wake unataka kufanana na Michael Jordan hivo kupelekea watu wengine kuweka utani kwamba ni mtoto wa nje wa MJ.

Binafsi nikimuangalia akiwa anacheza naona ni combination ya Kobe Bryant na Michael Jordan ndani ya mtu mmoja.

Makinda wengi wamejikuta wanapotea sababu ya kukosa nidhamu na kutokuwa makini ndani ya uwanja hivyo kupelekea majeraha, mfano mzuri ni Ja Morant, ni dogo aliepata mafanikio makubwa sana ila tabia zake nje ya uwanja kama vile kuonesha bunduki hadharani na pia kutokuwa makini ndani ya uwanja ambapo kulimpelekea kupata majeraha kumemfanya afungiwe mara kadhaa kushiriki NBA na kukosa baadhi ya mechi muhimu. Ila kwa upande wa Anthony Edwards ni tofauti. Dogo anacheza moves hatari ndani ya uwanja ila yupo makini kuepusha majeraha, vile vile hana scandal mbovu mbovu nje ya uwanja.

Mwisho nitoe pole kwa waliompa Nuggets Game 7, najua imewashangaza sana kuona Wolves ameshinda. Nuggets mwanzoni alitawala mchezo, Kuna muda Nuggets alikua anaongoza hadi kwa tofauti ya alama 15, ila quarter ya mwisho akanyooshwa na kuishia kupigwa kwa tofauti ya points 6 (96 kwa 90).
 
Minesotta Timberwolves isingeweza fungwa na Watu wanaosapot, wazee wa rangi nyingi, Watu wa hisani za Marekani😁 ...But kwanza Minesotta Timberwolves sio timu inayobebwa na mtu mmoja..timu nzima iko compact sana..Tuanzie Defensively kuna Mfaransa Rudy Gobert na KAT ni Noma,Offensively pia ni hatari, Antman,KAT,Conley ni habari nyingine.

Wote wanatimiza majukumu yao kikamilifu..Point guard anavusha ball kwelikweli unaona transition hii apa,Wanaweka pick, wanashoot 3pts, wana'pass yaani wametimia.

Nikija kwa Antman ni Habari nyingine nakubaliana nawewe ni combo ya Kobe na MJ,Jamaa ana energy kinoma na atafika mbali sana..ila Akikutana nasisi Celtics☘️Tunamnyoa mapema mno game4.
 
Get yo
Hello bosses and roses, it has been a while...

Leo ngoja nimuongelee huyu kinda wa NBA kwa jina la Antony Edwards au Ant-Man, dogo wa 2001 tu hapa anaekipiga kwenye team ya Minnesota TImberwolves...
Get your facts right

Timberwolves walifika finals ya western conference play offs msimu wa 2003/2004

Walipoteza 2-4 kwa Lakers.

Kwa hiyo sio mara ya kwanza kufika fainali
 
Ofcoz, wolves kiukweli wapo compact, wamejitosheleza. Hata ukichek stats za Ant kwenye game ya jana zilikua ni average kwa ile team, alifunga point 16 out of total 96 points.

Ila sasa Ant anapata spotlight sababu ana uwezo extraordinary na focus ya ajabu na pia contribution yake ni kubwa sana hasa sabb ni complete package, Anaweza cheza defense na offense. Anascore, anaguard, ana-assist, anashoot 3s, yaan ni fujo. Ukitaka kuona umuhimu wake cheki mchezo wa wolves jamaa akiwa bench

KAT nae ni habari nyingine, Joker (Jokic) ana habari zake

By the way, Celtics kwa Dallas hachomoi, niko pale.

Fainali ni dallas vs wolves, na hapo ndo itakua ngumu kujua nani atashinda.
Celtic vs Dallas ? Dallas vs Wolves?
West final ni Dallas vs Wolves
East final ni Indiana vs Celtcs
Then NBA finals
dallas/wolves vs indiana/celtics
 
Minesotta Timberwolves isingeweza fungwa na Watu wanaosapot, wazee wa rangi nyingi, Watu wa hisani za Marekani😁 ...But kwanza Minesotta Timberwolves sio timu inayobebwa na mtu mmoja..timu nzima iko compact sana..Tuanzie Defensively kuna Mfaransa Rudy Gobert na KAT ni Noma,Offensively pia ni hatari, Antman,KAT,Conley ni habari nyingine..Wote wanatimiza majukumu yao kikamilifu..Point guard anavusha ball kwelikweli unaona transition hii apa,Wanaweka pick, wanashoot 3pts, wana'pass yaani wametimia...Nikija kwa Antman ni Habari nyingine nakubaliana nawewe ni combo ya Kobe na MJ,Jamaa ana energy kinoma na atafika mbali sana..ila Akikutana nasisi Celtics☘️Tunamnyoa mapema mno game4.
Unamuachaje McDaniels hapa ? Games mbili za mwisho kafunga 20+ i think. Hata game 7 wakati focus iko kwa Ant Man yeye ndio aliwaumiza Nuggets.
 
Ubingwa wa mwisho Celtics ni akina Paul Pierce I think 2008. Hizo nyingine history enzi za akina Larry Bird. Ni kama useme Bulls wako vizuri now kisa 6 rings za akina Jordan.na

Ubingwa wa mwisho Celtics ni akina Paul Pierce I think 2008. Hizo nyingine history enzi za akina Larry Bird. Ni kama useme Bulls wako vizuri now kisa 6 rings za akina Jordan.
Angalia record ya celtics past ten years kwenye play offs linganisha na wolves
Celtics huwezi kuifananisha the fell off bulls...
Tusubiri kda utasema
Nina imani na Boston
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom