Je, AC ya gari inatumia mafuta?

Je, AC ya gari inatumia mafuta?

Compressor ya AC inazungushwa direct na engine kupitia belt. Kuna baadhi ya magari mapya (newer models) compressor zao hazitumii engine, zinatumia umeme tu so hili linaweza fanya kazi hata gari likiwa kwenye ON position na haitumii mafuta.
Kwa yanayotumia engine kuzungusha compressor ni lazima gari liwe started kabisa na engine inaguruma, ikiwa kweny ON tu ni feni inayofanya kazi na AC iko off
Uzi umeufunga mkuu
 
Compressor ya AC inazungushwa direct na engine kupitia belt. Kuna baadhi ya magari mapya (newer models) compressor zao hazitumii engine, zinatumia umeme tu so hili linaweza fanya kazi hata gari likiwa kwenye ON position na haitumii mafuta.
Kwa yanayotumia engine kuzungusha compressor ni lazima gari liwe started kabisa na engine inaguruma, ikiwa kweny ON tu ni feni inayofanya kazi na AC iko off
Na hii ndio huleta utafauti katika matumizi ya mafuta kati ya gari model ya zamani na hizi mpya ambazo mifumo mingi umeme hutumika.
 
Compressor ya AC inazungushwa direct na engine kupitia belt. Kuna baadhi ya magari mapya (newer models) compressor zao hazitumii engine, zinatumia umeme tu so hili linaweza fanya kazi hata gari likiwa kwenye ON position na haitumii mafuta.
Kwa yanayotumia engine kuzungusha compressor ni lazima gari liwe started kabisa na engine inaguruma, ikiwa kweny ON tu ni feni inayofanya kazi na AC iko off
Kwakuwa wengi wetu tunatumia magari ya zamani kidogo inamaanisha tunatumia magari ambayo compressor inazungushwa na injini ya gari.......

Kwa muktadha huo itakuwa kwamba injini itabeba kamzigo ka ziada kuzungusha compressor....... najiuliza kwani compressor ni nzito sana hadi injini itumie mafuta mengi ya ziada?
Kwa vyovyote vile hata kama kutakua na ulaji mafuta wa ziada unaotokana na kuwasha AC basi itakua ni kiwango kidogo mmno ambacho hakina hathari yoyote
 
Kuna baadhi ya magari compressor zake zinatumia umeme so hazihitaji engine. Sema ni model za hivi karibuni
ndio maana nikaweka space kwa kuna gari za bei ghali zina huo mfumo wa compressor za umeme, ila Ac ya umeme kwa magari sio practical maana ufanyaji kazi kwa muda mfupi sana kabla ya battery hazijakuwa flat charge, Volvo waliweka system hiyo Battery Ac kwa battery mbili za 230 Mah walikuwa hawapati masaa mawil ya air con , imebidi waongeze battery tatu kwa ajili ya leisure amabyo ipo separate battery za kuwashia gari ,

Shughuli nzima ya kugandamiza freon gas sio ndogo ndio sababu hata mada inazungunzia hilo , maana compressor inapofanya kazi lazima mzigo uongezeke kwenye engine na ndio sababu gari huongeza ulaji wa mafuta ,wataalamu wa mahesabu wanasema mzigo inaobeba engine kwa ajili ya compressor inayopooza cabin ya saloon car , ni mkubwa zaidi kuliko mzigo wa kubeba abiria watatu kwenye saloon hiyo, kwa maana halisi ni kuwa unaweza ukatoka na familia yako yote kwenye gari na usihisi tofauti ya ulaji wa mafuta kama hujawasha Ac , ila hata kama hujabeba mtu ,upo peke yako kwenye gari ukiwasha Ac utaiona tofauti kubwa ya ulaji wa mafuta.
 
Kwakuwa wengi wetu tunatumia magari ya zamani kidogo inamaanisha tunatumia magari ambayo compressor inazungushwa na injini ya gari.......

Kwa muktadha huo itakuwa kwamba injini itabeba kamzigo ka ziada kuzungusha compressor....... najiuliza kwani compressor ni nzito sana hadi injini itumie mafuta mengi ya ziada?
Kwa vyovyote vile hata kama kutakua na ulaji mafuta wa ziada unaotokana na kuwasha AC basi itakua ni kiwango kidogo mmno ambacho hakina hathari yoyote
Kiukweli mafuta yanayotumika ni kidogo tu sema issue ni kwamba huku kwetu bongo sisi wenyew tunaweka mafuta kidogo tu ya buku 10 (km liter 5 hv) kwahyo hyo tofaut, japo kua ni ndogo sisi tutaiona sabab mafuta tunayoweka ni kidogo.

Na kinachofanya mafuta yatumike zaid ni tabia ya kuwasha AC then unazima baada ya dkk 10, then unawasha tena alaf unazima tena baada ya dkk 10. Kinachotokea ni kwamba compressor ishasafirisha gesi na tayari kuna baridi alaf wewe ukizima inapoa tena. Unawasha tena compressor inapata kazi ya kufanya hewa iwe ya baridi tena. Kazi inakua kubwa. Lakini ukiwasha na ukaiacha, gari lenyewe lina thermostat la litawasha compressor mpk hewa iwe ya barid na kuizima, itakua inawash na kuzima compressor yenyewe kuhakikisha hewa haipoi. Kazi inakua ni ndogo
 
Nimekuelewa mkuu na upo sahihi kabisa. Gari za kisasa huitaji umeme tu kuendesha AC kama ilivo kwa friji na AC za majumbani na ndicho nilichomaanisha hapo juu.
Gari yangu imetengenezwa 2016
unapata aircon kwa muda gani kabla battery hazijakuwa flat? mana kwa battery za kawaida huwezi kupata muda mrefu, gari kutengenezwa 2016 sio hija sana maana system ya electric compressors kwenye magari ipo kwa karibu miaka 15 sasa , shida ipo kwenye reliability ndo sababu hata magari ya 2020 bado wanatumia belt driven compressors. ni ya uhakika zaidi,
inagawa system ni moja kwa fridge na ac , lakini fridge hutumia nguvu kidogo kuliko Ac , mantiki ni kuwa fridge inapooza kitu kilichofungiwa , Ac yenyewe inapooza hewa ya joto all the times
 
ndio maana nikaweka space kwa kuna gari za bei ghali zina huo mfumo wa compressor za umeme, ila Ac ya umeme kwa magari sio practical maana ufanyaji kazi kwa muda mfupi sana kabla ya battery hazijakuwa flat charge, Volvo waliweka system hiyo Battery Ac kwa battery mbili za 230 Mah walikuwa hawapati masaa mawil ya air con , imebidi waongeze battery tatu kwa ajili ya leisure amabyo ipo separate battery za kuwashia gari ,

Shughuli nzima ya kugandamiza freon gas sio ndogo ndio sababu hata mada inazungunzia hilo , maana compressor inapofanya kazi lazima mzigo uongezeke kwenye engine na ndio sababu gari huongeza ulaji wa mafuta ,wataalamu wa mahesabu wanasema mzigo inaobeba engine kwa ajili ya compressor inayopooza cabin ya saloon car , ni mkubwa zaidi kuliko mzigo wa kubeba abiria watatu kwenye saloon hiyo, kwa maana halisi ni kuwa unaweza ukatoka na familia yako yote kwenye gari na usihisi tofauti ya ulaji wa mafuta kama hujawasha Ac , ila hata kama hujabeba mtu ,upo peke yako kwenye gari ukiwasha Ac utaiona tofauti kubwa ya ulaji wa mafuta.
Yeah ni kweli. Ku run A/C kwa umeme ni kazi pia. Sabab A/C kwenye engine kwa kawaida huwa inaongeza load ya 3HP mpk 8HP.
Magari yanayotumia umeme tu ku run compressor mara nyingi yanakua na betri hadi 3. Na mara nyingi ni magari ambayo unakuta hadi socket ya 110V/220V kwenye gari, kma baadhi ya 2018/2020 Ford F250.
Na mengine ni magari ya full electric (EV) na yale Hybrid (Electric + Normal engine)
 
Mfano, gari linapokuwa kwenye idle state (silence) kama umewasha AC utasikia muungurumo wa gari unapanda na kushuka pale thermostat inapofanya kazi yake ya kuzima na kuwasha AC. Najua wengi watabisha, lakini kuna utofauti wa matumizi ya mafuta ukitumia AC na usipotumia AC hasa kwa magari madogo.
Hii nilikua naisikia sana kwenye hizi land cruiser sikujua kama ni kwasababu ya AC.
 
Ikiwa unavuta mzigo wa kilo tano, ukiongezewa kilo 2 si itabidi uongeze nguvu za kuuvuta?

AC mfumo wake unazungushwa na Engine ya gari, unapoiwasha AC, compressor inaongeza mzigo kwa engine.

Hata ukiwa unatumia generator ya umeme, mlio hua unabadilika unapowasha vifaa vinavyotumia huo umeme.

Na kwakua engine inapozunguka inatumia mafuta, inapoongezewa mzigo itatumia mafuta mengi zaidi.
Simple and clear explanation.
 
Back
Top Bottom