Je, AC ya gari inatumia mafuta?

Je, AC ya gari inatumia mafuta?

kijazi07

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2016
Posts
1,035
Reaction score
2,211
Naombeni kueleweshwa ni kwa namna gan AC ya gari inatumia mafuta.

Mfano nikiwa nimeweka gari on bila kuliwasha kabisa alafu nikawasha AC mafuta yanatumika?
 
🤣 🤣 🤣 ngoja waje wajuzi. Lakini jibu la kwangu ni NDIYO. Comnsumption ya mafuta inakua juu pale unapotumia AC kwa sababu compressor ya AC inaongeza mzunguko wa injini (RPM)
 
ngoja waje wajuzi. Lakini jibu la kwangu ni NDIYO. Comnsumption ya mafuta inakua juu pale unapotumia AC kwa sababu compressor ya AC inaongeza mzunguko wa injini (RPM)
Sasa kama sijawasha gar mafuta yanaendaje
 
Sasa mkuu unapata wapi ac bila engine kua on?

AC inategemea mzunguko wa engine hili kufanya kazi kwa hyo kinachokula mafuta ni engine na sio AC
 
Mfano, gari linapokuwa kwenye idle state (silence) kama umewasha AC utasikia muungurumo wa gari unapanda na kushuka pale thermostat inapofanya kazi yake ya kuzima na kuwasha AC. Najua wengi watabisha, lakini kuna utofauti wa matumizi ya mafuta ukitumia AC na usipotumia AC hasa kwa magari madogo.
 
ngoja waje wajuzi. Lakini jibu la kwangu ni NDIYO. Comnsumption ya mafuta inakua juu pale unapotumia AC kwa sababu compressor ya AC inaongeza mzunguko wa injini (RPM)
Kwa hyo mkuu umekubali kabisa akizima gari akiwasha AC itafanya kazi nakula mafuta
 
Ikiwa unavuta mzigo wa kilo tano, ukiongezewa kilo 2 si itabidi uongeze nguvu za kuuvuta?

AC mfumo wake unazungushwa na Engine ya gari, unapoiwasha AC, compressor inaongeza mzigo kwa engine.

Hata ukiwa unatumia generator ya umeme, mlio hua unabadilika unapowasha vifaa vinavyotumia huo umeme.

Na kwakua engine inapozunguka inatumia mafuta, inapoongezewa mzigo itatumia mafuta mengi zaidi.
 
1Ni sawa na kuwacha koki ya mtungi wa gesi wazi bila ya kuwasha moto.
2 Unauwa betri ya gari pia.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Kwa hyo mkuu umekubali kabisa akizima gari akiwasha AC itafanya kazi nakula mafuta
AC haifanyi kazi gari ikiwa kwenye SWITCH ON ama ACC. Inafanya kazi gari likiwa limewashwa tu. Naona sikulisoma vzr swali. Elewa hivyo
 
Naomben kueleweshwa ni kwanamna gan AC ya gar inatumia mafuta

Mfano nikiwa nimeweka gar on bila kuliwasha kabisa alafu nikawasha AC mafuta yanatumika??
Naongelea kitu kama hiki yan unaweka Gar On then unawasha AC je hapa mafuta yanatumika?

Uki start gari najua yanatumika je ukiweka tu on bila kustart gar mafuta yanatumika?
20200818_173851.jpg
View attachment 1541268
 
AC hautumii mafuta ili kufanya kazi yake Bali hutumia umeme. Unaweza kuwasha AC pasipokuwasha injini ya gari yako.
Matumizi ya mafuta huongezeka pindi utumiapo AC kwasababu gari italazimika kutengeneza umeme wa ziada kwaajili ya AC, hivyo matumizi ya mafuta huongezeka. Lakini ni kwa kiasi kidogo sana.
#ZINGATIA; matumizi ya AC pasipo kuwasha injini ya gari hupelekea betri kufa mapema.
 
AC hautumii mafuta ili kufanya kazi yake Bali hutumia umeme. Unaweza kuwasha AC pasipokuwasha injini ya gari yako.
Matumizi ya mafuta huongezeka pindi utumiapo AC kwasababu gari italazimika kutengeneza umeme wa ziada kwaajili ya AC, hivyo matumizi ya mafuta huongezeka. Lakini ni kwa kiasi kidogo sana.
#ZINGATIA; matumizi ya AC pasipo kuwasha injini ya gari hupelekea betri kufa mapema.
Ohoo sasa nimekupata safi sana
 
Kwa ufahamu wangu, mfumo wa A/C huwa una compressor kwa lengo la kufua au kugandamiza gas ndani ya system. Compressor huendeshwa na Engine kwa njia ya mikanda (belt). Engine hutumia mafuta mengi pindi unapoipa mzigo zaidi kwahiyo pale unapowasha A/C unakuwa umeipa mzigo engine na kupelekea kuhitaji mafuta zaidi kwa lengo la kuongeza nguvu.

Gari ikiwa on unachoweza kuwasha ni blower tu lakini ikiwa katika idle ndiyo unaweza kuswitch A/C na ikapiga kazi.
 
Ikiwa unavuta mzigo wa kilo tano, ukiongezewa kilo 2 si itabidi uongeze nguvu za kuuvuta?

AC mfumo wake unazungushwa na Engine ya gari, unapoiwasha AC, compressor inaongeza mzigo kwa engine.

Hata ukiwa unatumia generator ya umeme, mlio hua unabadilika unapowasha vifaa vinavyotumia huo umeme.

Na kwakua engine inapozunguka inatumia mafuta, inapoongezewa mzigo itatumia mafuta mengi zaidi.

yeah
 
AC hautumii mafuta ili kufanya kazi yake Bali hutumia umeme. Unaweza kuwasha AC pasipokuwasha injini ya gari yako.
Matumizi ya mafuta huongezeka pindi utumiapo AC kwasababu gari italazimika kutengeneza umeme wa ziada kwaajili ya AC, hivyo matumizi ya mafuta huongezeka. Lakini ni kwa kiasi kidogo sana.
#ZINGATIA; matumizi ya AC pasipo kuwasha injini ya gari hupelekea betri kufa mapema.


Hapo umelenga point kabisa.

Injini inatumika kama generator, unapowasha AC ni sawa umeongeza mzigo (Load) kwenye mfumo wa kuzalisha umeme wa gari. Kwa hivyo injini inapata resistance na kuongeza mzunguko ili kukabiliana na uzito ulioongezeka katika uhitaji wa umeme wa kuendesha AC.

Effect hiyo inaonekana zaidi gari inapokuwa haitembei au kama inatembea mwendo wa chini. Lakini kama upo safari ya masafa katika mwendo kasi basi sio tatizo na hitaona tofauti.
 
Hapo umelenga point kabisa.

Injini inatumika kama generator, unapowasha AC ni sawa umeongeza mzigo (Load) kwenye mfumo wa kuzalisha umeme wa gari. Kwa hivyo injini inapata resistance na kuongeza mzunguko ili kukabiliana na uzito ulioongezeka katika uhitaji wa umeme wa kuendesha AC.

Effect hiyo inaonekana zaidi gari inapokuwa haitembei au kama inatembea mwendo wa chini. Lakini kama upo safari ya masafa katika mwendo kasi basi sio tatizo na hitaona tofauti.
Upo sawa kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom