Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi

Tunataka Tanzania tajiri yenye demokrasia.
 
Mkuu. Wenye akili tunajua wakati mzuri wa kujiangalia ni pale unapowaona "wakikusifia na kukumbatiakumbatia"
Ukiona wanaanza kulialia ujue uko kwenye right track (We songa mbele!)
Si kweli kuna siku moja moja hata kichaa huwa anasema ukweli, tuendelee kujifariji uchumi unapaa.
 
Hivi ninaposoma comments za wadau humu eti WAZUNGU TUMEWASHIKA PABAYA, pabaya hapo ni wapi, maana naona bado Waziri Mipango anatembeza bakuli kwa hao inaosemekana tumewashika PABAYA.......Kama kuna mahali tumekosea, jamani tusione soni kujisahihisha,muda bado upo na Wananchi wataelewa tu.
 
Vita ya makinikia hii...2 days two articles ...naona hadi article ya kesho wameitoa leo.
Hapa ndipo jaribio la uhuru wa kweli wa nchi lilipo!!
Whatever, tujiulize, kuna ukweli, basi kama hakuna ukweli, tupuuze, kama kuna ukweli tutafakari mustakabali wetu na historia yetu.
 
Duuh hawa jamaa ndio wanaochochea maandamano na vurugu, wanataka kuvuruga amani yetu, tuwapuuze na tumuunge mkono Rais wetu mpendwa JPM
jingalao cocochanel
Upo sahihi. Sidhani kama wanatupenda sana kuwa watupiganie. Lakini Tanzania bado hatuwezi kuishi kama kisiwa au tukajitegemea kwa asilimia mia. Tunatakiwa kutumia akili zaidi na la muhimu kabisa ni kuhakikisha ndani ya nchi hakuna unyanyasaji au mgawanyiko ili tuwe kitu kimoja. Na hii ni moja ya kazi kubwa ya raisi. Kipindi kama hichi cha chokochoko kutoka nje anatakiwa kuhakikisha kuwa hakuna mambo ya uvyama. Na hapa akili kubwa ndo inahitajika na si kitu kingine chochote.
 
Kama North Korea na Venezuela wamezipigia magoti hizi western countries sembuse Tanzania. Tuambieni ukweli Rais Magufuli yupo njia sahihi lakini suala la demokrasia na human rights aziangalie kwa umakini. Kwenye masuala ya taifa tusiangalie uccm ama uchadema kwani vikwazo vya kiuchumi havijui chama
 
Naona hujasoma vizuri au kuelewa kilichandikwa hapo kwenye hilo gazeti na pia hujatulia na kumuelewa Mayala kwanini kaileta hii mada iliopo kwenye hilo gazeti, kwa kifupi hakuna uongo hata moja hapo, tunachotakiwa ni serikali yetu ijitafakari na kuona wapi wanakosea, tukiendele kushabikia upuuzi basi ndio ndio tutazidi kupotea. Sio mtu unajiita mzalendo halafu unaona taifa linadidimia unashindwa hata kukemea, unabakia kuwa mshabiki tu.
 
Mnatafuta mchawi, shambulio la Tundu Lissu ambae alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali ambako limefanyika mchana kweupe kwenye makazi ya maafisa wa serikali na kukosekana hata surveillance camera imeiaibisha serikali.

Waandishi wote wa habari wanao and ila habari za kukosoa maovu ya serikali wanatishiwa vifo

Kudhoofishwa kwa nguvu ya upinzani nchini haya yote msifikiri mnaishi kwenye kisiwa peke yenu
 
Nadhani wanaona gele tunavyosonga mbele kuelekea kuwa donor country siku za hivi karibuni. Walizoea kutupa misaada sasa wanaona tunaelekea kujikomboa na kongwa la umaskini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…