Japan yamwaga billion 74

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
SERIKALI ya Japan imetoa msaada wa zaidi ya shilingi bilioni 74 kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya Bagamoyo kupitia Mwenge
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, alisema msaada huo wa fedha utasaidia kupunguza foleni katika barabara hiyo pindi ujenzi huo utakapokamilika.

Alisema barabara hiyo, ina urefu wa kilomita 12.9 italeta maendeleo na kurahisisha suala zima la usafiri na kuondoa kuwepo kwa msongamano mkubwa wa magari unaosababisha kuwepo kwa foleni.

Pia alisema upanuzi huo utalazimu nyumba zilizopo kando ya barabara hiyo kubomolewa kwa kuwa mafundi wataingia ndani mita mbili kila upande wa barabara hiyo kuanzia Mwenge, Tegeta hadi Bagamoyo ili kupisha ujenzi huo.

Alisema wakazi wote watakaobomolewa nyumba zao, watalipwa fidia kutokana na tathmini itakayofanyika kila mtu atapewa fidia yake kwa kigezo cha uthamani wa nyumba itakayobomolewa.

NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.

JE WABONGO WENZANGU TUTATEGEMEA MISAADA MPAKA LINI JAMANI?
 
SERIKALI ya Japan imetoa msaada wa zaidi ya shilingi bilioni 74 kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya Bagamoyo kupitia Mwenge
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, alisema msaada huo wa fedha utasaidia kupunguza foleni katika barabara hiyo pindi ujenzi huo utakapokamilika.

Alisema barabara hiyo, ina urefu wa kilomita 12.9 italeta maendeleo na kurahisisha suala zima la usafiri na kuondoa kuwepo kwa msongamano mkubwa wa magari unaosababisha kuwepo kwa foleni.

Pia alisema upanuzi huo utalazimu nyumba zilizopo kando ya barabara hiyo kubomolewa kwa kuwa mafundi wataingia ndani mita mbili kila upande wa barabara hiyo kuanzia Mwenge, Tegeta hadi Bagamoyo ili kupisha ujenzi huo.

Alisema wakazi wote watakaobomolewa nyumba zao, watalipwa fidia kutokana na tathmini itakayofanyika kila mtu atapewa fidia yake kwa kigezo cha uthamani wa nyumba itakayobomolewa.

NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.

JE WABONGO WENZANGU TUTATEGEMEA MISAADA MPAKA LINI JAMANI?

Achalia mbali suala la msaada kinachosikitisha anasema msaada utapunguza foleni kwa hiyo hapo lengo ni kupunguza sio kumaliza, unaona thinking ya watanzania, tunafikia mwisho wa pua hatuende]i mbele zaidi. So in two years time foleni itarudi palepale.

Halafu Katibu mkuu naye analeta utani kama bosi wake, mkopo in kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kilomita 12.9 halafu yeye anasema barabara itajengwa toka mwenge hadi bagamoyo, kipande ambacho umbali wake ni zaidi ya kilomita 12.9. Hivi watanzania ni lini tutakuwa serious. With this kind of attitute mnadhani kweli tutaendelea???
 
Achalia mbali suala la msaada kinachosikitisha anasema msaada utapunguza foleni kwa hiyo hapo lengo ni kupunguza sio kumaliza, unaona thinking ya watanzania, tunafikia mwisho wa pua hatuende]i mbele zaidi. So in two years time foleni itarudi palepale.

Halafu Katibu mkuu naye analeta utani kama bosi wake, mkopo in kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kilomita 12.9 halafu yeye anasema barabara itajengwa toka mwenge hadi bagamoyo, kipande ambacho umbali wake ni zaidi ya kilomita 12.9. Hivi watanzania ni lini tutakuwa serious. With this kind of attitute mnadhani kweli tutaendelea???

Nadhani ni kosa la mwandishi kwa kuwa vyombo vingi vinasema Mwenge mpaka Tegeta(junction ya kwenda wazo hill)......nimepima leo na kupata 12786 metres exactly......ODO reading that is

Ila nashangaa toka mwenge mpaka morocco pameachwa.....hii si sawa kuvaa suti na kandambili?......
 
Ila nashangaa toka mwenge mpaka morocco pameachwa.....hii si sawa kuvaa suti na kandambili?......

Ukipanua Mwenge mpaka Morogo, gharama itakuwa kubwa sana kutokana na majengo mengi ni ya thamani, na yamejengwa karibu na barabara. Nadhani pengine ndio maana wameamua kupaacha.

Ni kama kupanua barabara katikati ya posta!
 
Uko mpango mwingine tofauti kupanua kutoka Morocco hadi mwenge huo ni mradi mwingine. Naaamini tathmini imeshaanza. Kuhusu ngambo Ngali na hoja ya kupunguza badala ya kumaliza foleni hiyo haipo ndugu yangu as long kuna magari foleni itaendelea kuwepo tu suala ni kupunguza kama wanavyodai. Hata LA ambako kuna freeways zenye njia nanenane foleni bado zipo tu ila barabara nzuri husaidia kuzipunguza...
 
Ukipanua Mwenge mpaka Morogo, gharama itakuwa kubwa sana kutokana na majengo mengi ni ya thamani, na yamejengwa karibu na barabara. Nadhani pengine ndio maana wameamua kupaacha.

Ni kama kupanua barabara katikati ya posta!

Sidhani........wakati Upanga(Ali Hassan Mwinyi siku hizi) Road inapanuliwa,eneo toka Palm Beach mpaka pale Peugeot house kulikuwa na wasiwasi huo lakini waqtaalam waliweza kupanua bila kuweka tuta(island) katikati na leo tunafaidika........hiii ya morocco ni pale Alpha House ndio siasa kibao....wakipanua tu hawa parking.....tukitaka njia nne zitatoka tu mbona tatu zipo na nafasi bado ipo
 
Msaada - Msaada - Misaada mpaka lini. Sisi ni omba omba a.k.a TZ - MATONYA.
Aibu.
 
bilioni 74 inaweza jenga dar mpaka bagamoyo na kulipa fidia?
 
Back
Top Bottom