Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
SERIKALI ya Japan imetoa msaada wa zaidi ya shilingi bilioni 74 kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya Bagamoyo kupitia Mwenge
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, alisema msaada huo wa fedha utasaidia kupunguza foleni katika barabara hiyo pindi ujenzi huo utakapokamilika.
Alisema barabara hiyo, ina urefu wa kilomita 12.9 italeta maendeleo na kurahisisha suala zima la usafiri na kuondoa kuwepo kwa msongamano mkubwa wa magari unaosababisha kuwepo kwa foleni.
Pia alisema upanuzi huo utalazimu nyumba zilizopo kando ya barabara hiyo kubomolewa kwa kuwa mafundi wataingia ndani mita mbili kila upande wa barabara hiyo kuanzia Mwenge, Tegeta hadi Bagamoyo ili kupisha ujenzi huo.
Alisema wakazi wote watakaobomolewa nyumba zao, watalipwa fidia kutokana na tathmini itakayofanyika kila mtu atapewa fidia yake kwa kigezo cha uthamani wa nyumba itakayobomolewa.
NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.
JE WABONGO WENZANGU TUTATEGEMEA MISAADA MPAKA LINI JAMANI?
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Khijjah, alisema msaada huo wa fedha utasaidia kupunguza foleni katika barabara hiyo pindi ujenzi huo utakapokamilika.
Alisema barabara hiyo, ina urefu wa kilomita 12.9 italeta maendeleo na kurahisisha suala zima la usafiri na kuondoa kuwepo kwa msongamano mkubwa wa magari unaosababisha kuwepo kwa foleni.
Pia alisema upanuzi huo utalazimu nyumba zilizopo kando ya barabara hiyo kubomolewa kwa kuwa mafundi wataingia ndani mita mbili kila upande wa barabara hiyo kuanzia Mwenge, Tegeta hadi Bagamoyo ili kupisha ujenzi huo.
Alisema wakazi wote watakaobomolewa nyumba zao, watalipwa fidia kutokana na tathmini itakayofanyika kila mtu atapewa fidia yake kwa kigezo cha uthamani wa nyumba itakayobomolewa.
NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.
JE WABONGO WENZANGU TUTATEGEMEA MISAADA MPAKA LINI JAMANI?