Manumbu
JF-Expert Member
- Oct 28, 2009
- 1,746
- 1,282
Nimewahi sikia kuwa mwanaume wa kiafrika akiishi Japan kwa muda wa kama kuanzia miaka 2 na kuendelea anapoteza uwezo wa kuzaa watoto wa kiume. Badala yake ataweza kuzaa watoto wa kike pekee. Hili linawatokea zaidi wanaume wenye asili ya Afrika. Wenyeji tayari wana kinga ya asili hili haliwasumbui. Je kuna ukweli wowote kuhusiana na hili? kwa wanaume wa kibongo ambao wameishi Japan kwa muda na sasa wamepata watoto wanaweza kutujuza uzoefu wao? Na kama ni kweli nini kifanyike ili mtu aweze kuzaa kama kawaida bila ya kupatwa na hayo madhara ya 'ujapani'? na je hii hali ni kwa Japan pekee au bara lote la asia lenye 'orientals'? Nawasilisha tujuzane.