Mynd177
JF-Expert Member
- Dec 3, 2022
- 2,041
- 3,502
Kumbe saa nne mkuu.. must wait for that...Itatokea kuanzia saa nne usiku. Saa 4:24 Mirihi itazibwa na Mwezi na itaachwa saa saa sita na dakika mbili.
Kumbe saa nne mkuu.. must wait for that...Itatokea kuanzia saa nne usiku. Saa 4:24 Mirihi itazibwa na Mwezi na itaachwa saa saa sita na dakika mbili.
ASSAT ni taasisi ya serikali au NGO fulani?!Mwaka mpya wa 2023 unaashiriwa na tukio la kipekee angani la Mwezi kuficha sayari ya Mirihi (Mars) siku ya Jumanne tarehe 03 Januari. Usiku wa siku hiyo sayari angavu nyekundu ya Mirihi itazibwa na Mwezi ulio karibu kwa kiasi masaa mawili kuanzia saa 4:15 usiku. Kuanzia saa 4:24 Mirihi itaanza kufunikwa ma Mwezi kutoka ukingo wake wa chini kulia. Hutaona sayari hiyo hadi baada ya saa moja na nusu hivi saa sita ya manane Mirihi itakapo jitokeza tena kutokea ukingo wa chini kushoto. Yaani tukio hili ni la kupatwa kwa sayari ya Mirihi.
Ramani hii inaonesha sehemu za Dunia ambako tukio hili litaonekana,
hasa bara la Afrika sehemu za mashariki, kati, na kusini.
View attachment 2462693
Na picha hizi zinaonesha Mirihi itakavyokuwa jirani kabisa na Mwezi kuanzia saa 4:15 usiku na utakavyoonekana sayari itavyojitokeza mara baada ya saa sita usiku.
View attachment 2462695
Tukio kama hili la kupatwa kwa sayari na kufichwa na Mwezi ni la nadra sana na hasa kwa vile linatokea wakati watu bado wapo macho na kulishuhudia.
Hauhitaji darubini au chombo chochote kufurahia tukio hili na halina madhara yoyote. Ni la kusisimua uelewa wa mambo ya angani. Ni rahisi kutambua Mirihi angani kwa sasa kwa vile inang’aa sana kutokana na kuwa jirani zaidi na Dunia na kuangaliana na Jua hivo huwezi kukosa kuona uwekundu wa Mirihi. Pamoja na hiyo siku ya tukio Mwezi utakuwa jirani na nyota hiyo nyekundu.
View attachment 2462698
Jioni ya siku ya tukio, mara baada ya magharibi saa moja jioni anga imejaa sayari nne zilizopangika katika mstari mnyofu. Picha ya anga yote inaonesha mpangilo wa sayari na Mwezi katika mstari mmoja. Zuhura (Venus) itakuwa
jirani na upeo wa mahjaribi. Juu yake, angani kati ni sayari ya Zohali (Saturn) inayong’aa kwa ukali tulivu. Juu zaidi utaona karibu na utosi ni sayari angavu sana ya Mshtarii (Jupiter). Ukiendekea zaidi utosini upande wa mashariki
utaona Mwezi ukiwa jirani na Mirihi nyekundu.
Ufuatilie uone hali angani siku ya Jumanne tarehe 03 Januari na uweze kujenga dhana ya hasa kitu gani kinatokea angani wakati uaangilia Mirihi nyekundu inapofichikwa na Mwezi. Kaa macho kwa kuweza kuanglia tukio hili kwa darubini.
Imetolewa na Dr. N.T. Jiwaji, Astronomy and Space Science Association of Tanzania (ASSAT) ntjiwaji@yahoo.com
Hahaha kweli hali ngumu, kichwa kinashindwa kupokea taarifa za kiastronomy na kuzifanyia uchambuzi yakinifu🤣🤣Wacha tu ipatwe watu tumevurugwa 😂😂asante kwa taarifa lakin
Mi nasubiria the moment of the first man to land on Mars tu. Naona Elon Musk na project yake amezamilia 2023 mtu kutua MarsKumbe saa nne mkuu.. must wait for that...
niko mubashara hapa natizama.Kumbe saa nne mkuu.. must wait for that...
ndiyo maana nimesema kama hauli mboga za majani usiangalie, utaishia kuumia macho.Nipo live mbona sioni kitu
Na ww umepatwa MarsB dei yangu leo
Hakuna upigaji mkuu, tukio lilikuwa wazi na bado linaendelea.Wakuu tupeni Update ,mnaona hayo mambo ya wapigaji wa NASA?
subiria mida ya saa sita hivi itakuwa imejitokeza upande wa pili.Hapa nilipo mwezi umefunikwa na wingu sioni kitu
Pole sana. uko nch gani huku kwetu bukoba sky ipo clear mno...Hapa nilipo mwezi umefunikwa na wingu sioni kitu
Ni Upigaji tu wa NASA hamna chochote ,sioni chochote zaidi ya mwezi tu unang'aa kama kawaida(refelection ya mwanga wa jua) ,siioni sayari ya Mars sehemu yeyote.Hakuna upigaji mkuu, tukio lilikuwa wazi na bado linaendelea.
Ila mpaka sasa sayari ya Mars imepatwa na mwezi, mida ya saa sita tunatarajia itajitokeza upande wa pili.