Janga la Korona, ni mapambano dhidi ya Ugonjwa tu au kuna ajenda nyuma ya pazia!?

Kingjr2

JF-Expert Member
Sep 8, 2018
644
1,271
Tangu mwaka huu uanze dunia imekuwa kwenye mtanziko mkubwa juu ya janga linalotishia uhai wa binadamu na uhai wa uchumi wa dunia, si lingine ni janga la covid-19 au Corona virus.

Hakuna anayebisha kwamba janga hili limetikisa dunia! Tunaona dunia inavyohangaika!

Hapo kwenye kuhangaika kudhibiti Ugonjwa huo ndo kunanipa maswali mengi!

Katika nchi nyingi shule zimefungwa, vyuo, ofisi mbalimbali, huduma za usafiri hasa wa ndege, Taasisi mbalimbali zimesimamisha kazi zake, wafanyakazi wako nyumbani!

Baadhi ya nchi zimeenda mbali zaidi na kulazimika kuwafungia ndani wananchi wake (lockdown)

Kila siku tunapewa takwimu za vifo na maambukizi mapya ya mataifa mbalimbali.

Takwimu zinapanda kila siku kiasi kwamba nchi zinazoripoti kiasi kidogo cha maambukizi zinatiliwa mashaka kuficha taarifa.

Nchi ambazo zimeripoti kutokuwa na maambukizi ya Corona zinaanza kutiliwa mashaka kwamba huenda hawana vifaa thabiti!

Nchi nyingi za dunia ya tatu zimepata maambukizi kutoka nje! Yaani Ugonjwa umekuja na watu!

Kwanini tunalazimisha kila nchi iwe na wagonjwa? Kwanini tutilia mashaka nchi zenye maambukizi kidogo? Kwanini tulazimishe takwimu za kila siku?

Hivi kupewa taarifa kila siku hatuoni kwamba kunaongeza taharuki na hofu kwenye jamii?

Kwanini tusimamishe shughuli za uzalishaji kwa kuwafungia watu ndani badala ya kufunga mipaka?

Shule , baadhi ya ofisi, na Taasisi mbalimbali zimesimamisha shughuli zake hata zile ambazo hazina muingiliano na wageni! Wakati huo huo sehemu zenye muingiliano na wageni zimeachwa huru! Tuko sahihi?

Baadhi ya nchi zimefungia watu wake ndani, wakati huo huo mipaka na viwanja vya ndege viko huru kupokea wageni!? Hii ni sahihi kweli wakati Ugonjwa haujaanzia ndani?

Hii Corona inaweza kuwa mwanzo wa matatizo mengine makubwa hasa ya kiuchumi.

Ukiangalia mbinu zinazotumika kuuzuia, ni mbinu zinazohamasisha uchumi kudidimia! Watu kukaa ndani!?!? Ofisi kufungwa!?!? Shule kufungwa!?!?

Tumekumbana na majanga mangapi na hatukufikia huko!? Leo kampeni ya dunia ni kuzuia watu wasiendelee na utaratibu wa Maisha waliyoyazoea.

Tusipuuze Maneno ya China kwa Marekani! Huenda Corona ni zaidi ya Ugonjwa, imelenga kuuwa uchumi wa dunia!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lengo la maisha siyo uchumi peke yake, maisha ni muhimu zaidi kuliko fedha, kuliko masomo, kuliko kitu kingine chochote.

Tukubali matakwa ya serikali kwa sababu wao wana wajibu wa kuilinda jamii na mahonjwa ya kila aina.

Kwa hili janga la corona ni lazima, wala siyo hiyari kutii masharti ya serikali ili kujikinga na corona.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sidhani Kama upo sahihi kwa hiki ulichoandika. Sio kila kitu lazima upinge ili uonekane mpinzani kuna mengine ukikaa kimya watu hawatataka kukujua kiundani hasa umri na kiwango chako cha elimu.

Jambo la kwanza kujua ni kwamba shughuli za kiuchumi zinafanywa na watu na lazima watu wawe katika afya nzuri kuzifanya kwa ufanisi na pia hakuna Serikali inayopenda kuona watu hawafanyi kazi. Sote tunaona kinachoendelea Italia , katika hali hiyo muafaka ni Nini? Kuruhusu watu waendelee kukutana na kuendelea kusambaza huku watu wakifa wengi au kuzuia watu kukutana?

Moja ya sababu zinazochangia ugonjwa huu kuenea ni mikutaniko ya watu, sehemu kamà shule ni mahali ambapo Kuna mikutaniko mikubwa ya watu ambao wengine hawana uwezo mkubwa wa kujikinga. Katika shule za bweni za watoto wadogo(chini ya darasa la saba) ambao hawajui Corona ni ni Nini, watafanya Nini ili wasieneze kwa wenzao? Je, watoto hao wakiathirika Nani wa kulaumiwa?

Tanzania hali haijawa mbaya ya kuweka "lockdown" na makatazo mengine makubwa lakini hali ikiwa mbaya zaidi hakuna namna zaidi ya kufanya wengine wanachofanya. Hilo ndio Jambo la msingi kufanya

Hii aibu niliyoisoma hapa na pengine kwa msomi ,inasikitisha sana. Bado tuna safari ndefu kama taifa Kama watu Kama wewe wataendelea kuwepo.
 
sie tushukuru tu kwamba hakuna vifo vinginivyo kujifungia ndani kusinge epukika!

hakuna ambaye ameshakuwa shujaa dhidi ya ugonjwa huu ktk nchi zetu iwe aliyefungia raia wake ndani au aliye waacha waendeele na shughuli zao.

ni vile tu ugonjwa huu ni kama ume ignore jamii ya huku. ila ungekuwa unafagia wtu kama itali tungekuwa tunapiga stori zingine hapa
 
Huko nyuma kuna maradhi mabaya sana yalisumbua dunia,baadhi yake yamepatiwa ufumbuzi.
Corona virus ni changamoto ngeni,ipo siku itapatilana dawa au kinga.Kwa sasa jambo muhimu ni kuzingatia ushauri wa madaktari.
 
Sidhani Kama upo sahihi kwa hiki ulichoandika. Sio kila kitu lazima upinge ili uonekane mpinzani kuna mengine ukikaa kimya watu hawatataka kukujua kiundani hasa umri na kiwango chako cha elimu.

Jambo la kwanza kujua ni kwamba shughuli za kiuchumi zinafanywa na watu na lazima watu wawe katika afya nzuri kuzifanya kwa ufanisi na pia hakuna Serikali inayopenda kuona watu hawafanyi kazi. Sote tunaona kinachoendelea Italia , katika hali hiyo muafaka ni Nini? Kuruhusu watu waendelee kukutana na kuendelea kusambaza huku watu wakifa wengi au kuzuia watu kukutana?

Moja ya sababu zinazochangia ugonjwa huu kuenea ni mikutaniko ya watu, sehemu kamà shule ni mahali ambapo Kuna mikutaniko mikubwa ya watu ambao wengine hawana uwezo mkubwa wa kujikinga. Katika shule za bweni za watoto wadogo(chini ya darasa la saba) ambao hawajui Corona ni ni Nini, watafanya Nini ili wasieneze kwa wenzao? Je, watoto hao wakiathirika Nani wa kulaumiwa?

Tanzania hali haijawa mbaya ya kuweka "lockdown" na makatazo mengine makubwa lakini hali ikiwa mbaya zaidi hakuna namna zaidi ya kufanya wengine wanachofanya. Hilo ndio Jambo la msingi kufanya

Hii aibu niliyoisoma hapa na pengine kwa msomi ,inasikitisha sana. Bado tuna safari ndefu kama taifa Kama watu Kama wewe wataendelea kuwepo.
Nimesoma comment zote za waliojadili hii mada hapa! Yako imenivutia kujibu.

Ni bahati mbaya sana umekimbilia kusema "napinga" ili nionekane "mpinzani'

Sikatai kwamba huenda post yangu imenichora kama napinga kitu fulani, la hasha! Ila naona kama umekimbilia kuniita mpinzani pasipo kuelewa lengo kuu la nilichokijadili

Yawezekana elimu yangu ni ndogo kweli, ila elimu yangu hii ndogo haiwezi kunizuia kuwaza nje ya box!

Labda tujiulize kwa pamoja! Kati ya mikusanyiko ya masoko kama kariakoo na miji mingine mikubwa kama Arusha, shughuli za viwanja vya ndege, mipakani, usafiri wa umma kama daladala na hizo shule za watoto wadogo au shughuli za taasisi mbalimbali ni kipi kinatuweka hatarini zaidi kueneza virusi vya Corona!?

Hakuna mahali nimepingana na juhudi zozote zinazolenga kudhibiti kazia hili la Corona! Ni jambo la kumshukuru Mungu Tanzania na nchi za Afrika nyingi ni kama Mungu ametuepusha na madhara makubwa ya janga hili!

Nilichohoji kama ungetafakari kwa kina kabla ya kushambulia elimu yangu ndogo na kuniita "mpinga kila kitu" ni kuacha maeneo hatarishi wazi na kukimbilia kufungia watu ndani na kusimamisha shughuli ambazo huenda Kasi yake ya kueneza virusi ni ndogo!

Hadi taarifa ya mwisho ya Waziri wa Afya wa Tanzania kwa mfano, alisema kesi zote zimeanzia nje ya nchi! Yaani hakuna aliyeambukiza/ambukizwa Corona ambaye hakutokea nje ya nchi!

Sasa hapo nguvu zaidi zinatakiwa kuelekezwa kuzuia nini!?

Binafsi namshukuru Mungu kuona leo China katika mji wa Wuhan shughuli zimeanza kurejea kama zamani japo kwa tahadhari kubwa!

Pamoja na watu kuongea ongea sana hatuna budi kushukuru viongozi wa serikali yetu pia hawakutetereka wala kubabaika katika kuchukua maamuzi hasa hili la kutoa taarifa! Kuna watu wanakosoa tena wakubwa tu na wengine hawaamini idadi inayotolewa na serikali!

Sasa jiulize, kwanini watu wanataka kusikia tu idadi kubwa kubwa!? Kwanini watu wanataka kusikia taarifa kila siku!?

Tuchukue tahadhari, Corona inaua! Ukihisi dalili za Corona wahi kituo cha tiba! Asante!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mtoa maada nawewe unakwama sana, sijaona point, ushauri wa wataalamu si kufunga mipaka,shule bali kuepusha misongamano
 
sie tushukuru tu kwamba hakuna vifo vinginivyo kujifungia ndani kusinge epukika!

hakuna ambaye ameshakuwa shujaa dhidi ya ugonjwa huu ktk nchi zetu iwe aliyefungia raia wake ndani au aliye waacha waendeele na shughuli zao.

ni vile tu ugonjwa huu ni kama ume ignore jamii ya huku. ila ungekuwa unafagia wtu kama itali tungekuwa tunapiga stori zingine hapa
Word

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua tunaweza kuwa na mawazo mengi Sana katika kupambana na janga Hili na mawazo yote yapo sahihi kabisa aidha kulock down au kufunga mipaka.

Lkn tutafakari kwa kina Sana. Corona Ni janga kubwa Sana la Dunia lkn sio janga pekee la Dunia liliwahi kutokea kwanza Ni declare interest mm sio wale wenye hoja ya kwamba watu wakae ndani(country lockdown) na kufunga mipaka.Tunatumia analysis ya takwimu ya nchi gan ya maambukizi ya corona na kijilinganisha na sisi Tanzania na kudraw conclusion kwamba we have to do the same Kama walivyofanya wao(lockdown).

Kule south Africa, Kenya n.k Hadi Sasa wanatuzidi kwa maambukizi mapya pamoja na jitihada za kulockdown na kufunga mipaka.Lkn pia tusipende kulinganisha na mataifa ambayo kiuchumi yapo vizuri kwa mtu mmoja mmoja (individual economy) na uchumi wa Taifa kwa ujumla(National economy) kiasi kwamba wanaouwezo wa kufanya hivyo na wakawasapoti wananchi wao kwa kiasi kidogo Sana tofauti na watu wanavyofikiria.

Ushauri wangu shughuri zote za kila siku ziendelee Kama kawaida ila tuendelee kupeana elimu na kuepuka kujenga Taharuki kubwa kiasi Cha kuwahadaa watu kuendelea na majukumu yao.

Pili uwekwe utaratibu hata kwa kutumia jeshi letu kusimamia mikusanyiko isiyokuwa ya lazima sana. Hali sio shwari kabisa katika Hili la mikusanyiko, watu hawajali kabisa.
Ahsanteni Sana



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo kadhaa yanatia wasiwasi
1. Kwanini kulazimisha kuwa na wagonjwa wengi kila siku?
Kwamba ukisema huna wagonjwa unaonekana mbaya kwa dunia na sisi tuliomo nchini tunasema serkali inatudanganya je tunataka wawepo? Je wewe mtaani kwako si ushahidi wakile kipo sasa?
Maybe CONSIPIRACY THEORY inacheza na akili za watu duniani


2. Kwanini inaelezwa kwa vitisho sana tofauti na takwimu zake Motarity rate, je ugonjwa huu na mengine yana athiri na kuua kwa uwiano gani. Maybe CONSIPIRACY

3. Hakuna kufanyakazi. Hii ndio HATARI kuliko ugonjwa wenyewe
Matokeo ni UCHUMI kuyumba
Wizi ,utaongezeka kwa aina zake
Utapiamlo ni ugonjwa utaua zaidi
Njaa itaangamiza wengi
Gap ya umaskini itasababisha vurugu mapinduzi ya kisiasa. Maybe CONSIPIRACY .

Historia inasimulia Total LODKDOWN mwaka 70 AD Yudae.
Watu walikula watoto wao
Walidhoofika kwa njaa
Finaly massive bloodshed

Jikinge na COVID 19 Homa ya mapafu inaua, fuata kanuni za afya na maelekezo muhimu ya serkali .
Fanyakazi . Njaa kubwa inakuja duniani, hata watakao kuwa nacho watakila kwa taabu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukipata maambukizi ya virusi vya Corona leo inachukua wastani wa wiki mbili dalili za ugonjwa kuonekana na ni mungu tu anajua katika kipindi icho unajiona mzima ukiendelea na shughuli zako umeambukiza watu wangapi.

Kinachotokea leo EUROPE (Italy na Spain) kumbuka ndio kwanza wana wiki mbili za lockdow ina maana mpaka sasa wamekuwa wana deal na maambukizi ya wale waliopata Corona before lockdown na health system zao chali; kwenda mbele wanaibuka waliopata maambukizi baada ya lockdown ambao ndio watakuwa wengi zaidi ndio maana unasikia wanasema peak ya vifo bado aijafika.

Sasa kama hiyo idadi ya mwanzo imekuwa shughuli, wakati kuna second wave ambayo inatarajiwa kuwa kubwa zaidi itakuwaje kwenye health systems; now imagine wasingechukua hatua za lockdown at all?

Endeleeni kujifurahisha kama mlivyozoea na kuleta mambo ya mzaha.

Uchumi tunadhani ni wetu tu Europe wanapiga hesabu za bailout baada ya Corona za kiwango cha WW2 na vita ilikuja na gharama za kuaribika kwa miundombinu, uzalishaji na matatizo kibao ya kijamii ndio ujue kiasi gani uchumi wao pia umearibika kupitia Corona mpaka kudai bailout itakayofanana na vita vikuu.
 
Watakupinga lakini umewaza vizuri sana!,
Mambo kadhaa yanatia wasiwasi
1. Kwanini kulazimisha kuwa na wagonjwa wengi kila siku?
Kwamba ukisema huna wagonjwa unaonekana mbaya kwa dunia na sisi tuliomo nchini tunasema serkali inatudanganya je tunataka wawepo? Je wewe mtaani kwako si ushahidi wakile kipo sasa?
Maybe CONSIPIRACY THEORY inacheza na akili za watu duniani


2. Kwanini inaelezwa kwa vitisho sana tofauti na takwimu zake Motarity rate, je ugonjwa huu na mengine yana athiri na kuua kwa uwiano gani. Maybe CONSIPIRACY

3. Hakuna kufanyakazi. Hii ndio HATARI kuliko ugonjwa wenyewe
Matokeo ni UCHUMI kuyumba
Wizi ,utaongezeka kwa aina zake
Utapiamlo ni ugonjwa utaua zaidi
Njaa itaangamiza wengi
Gap ya umaskini itasababisha vurugu mapinduzi ya kisiasa. Maybe CONSIPIRACY .

Historia inasimulia Total LODKDOWN mwaka 70 AD Yudae.
Watu walikula watoto wao
Walidhoofika kwa njaa
Finaly massive bloodshed

Jikinge na COVID 19 Homa ya mapafu inaua, fuata kanuni za afya na maelekezo muhimu ya serkali .
Fanyakazi . Njaa kubwa inakuja duniani, hata watakao kuwa nacho watakila kwa taabu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi zilizoathirika zaidi

ASIA
1. CHINA
2. IRAN
3. SOUTH KOREA
4. JAPAN

AFRICA
1. SOUTH AFRICA
2. Morocco
3. Algeria
4. Tunisia

NORTH AMERICA
1. USA
2. CANADA

SOUTH AMERICA
1. BRAZIL
2. ARGENTINA

EUROPE
1. ITALY
2. SPAIN
3. FRANCE
4. GERMANY
5. UK


Inaelekea huu ugonjwa unawapenda Sana matajiri na unawaogopa sana maskini. Kama hii sio fact basi ni DHAHIRI KUNA KITU KINAFICHWA NYUMA YA CORONA.

UTABIRI WANGU

Ambao hawaja"suffer" kipindi Cha Corona wata"suffer" Sana baada ya Corona.
 
Kwa kweli ukiangalia ama kusikiliza maoni ya watu ni kana kwamba baadae hali itakuwa ngumu maybe.

Chakuzingatia ni kwamba maisha ya mwanadamu hayawi bila ya changamoto. Na changamoto yoyote ukiikabili vyema hukuinua viwango fulani vya akili.

Muhimu kuliko yote tujue hakuna namna ya kuyaweza maisha bila ya Mungu! Tukubali tukatae.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka sasa hata waliopata athari kubwa ya huu ugonjwa bado wanajiuliza maswali ambayo hayana majibu ila bado wanatafakari au wanaficha mengine
Hili la kulazimisha watu tukae ndani (kwa nchi zilizoathirika zaidi)
Huenda lina kitu cha kuficha ili taharuki isitokee
Kuna mtu tumebishana nae sana, anasema huu ugonjwa ni airborne lakini kila wakati nikitafakari naona inawezekana maana hata wao kila siku wanasema a What we know and what we don’t know
Na WHO nao hawako nyuma kwa hili ila wataalamu wengine hawataki lisemwe hili
Je Kuna nini nyuma ya pazia?
Siku ya Sita leo sijatoka nje ila hali sio hali na ndio kwanza tumeambiwa inaweza kuendelea mpaka miezi 6
Ugonjwa huu siuelewi kabisa na tuombe usishambulie sana Africa maana kama unavyomaliza watu ulaya sidhani kama tutalimudu
Fuata masharti ya wataalamu kaa ndani kama unaweza



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom