Janga jipya: Zanzibar yaishiwa Mchanga, sasa kuagizwa nje ya nchi

Wajifunze nchi nyingine wanafanyaje kwenye changamoto kama hiyo.
Maana ardhi ya zanzibar sio nchi kavu tu, Kuna mahecta ya ardhi chini ya bahari ila changamoto ni gharama ya kuuchimba.hata kama unachumvi inawezekana kukawa na namna ya kuufanya ufae
Badala ya kuimport mchanga wanaweza kuimport mbao nyepesi kama gharama zitaruhusu. Sio lazima tuishi kwenye nyumba za blocks.
 
Hamad Rashid ametangazia dunia kwamba Nchi ya Zanzibar imeishiwa mchanga kwaajili ya Ujenzi, hivyo wameruhusu kuagiza mchanga toka nje bila kodi.

Serikali ya Zanzibar imeomba wadau wajitokeze kuagiza mchanga nje ya nchi ili ujenzi uweze kuendelea.

Kwa sasa lori la mchanga linauzwa kwa laki moja na na bado haupatikani kwani kila sehemu walipokuwa wanachimba umeisha.

========

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imekusudia kuagiza mchanga nje ya nchi kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa kwa rasilimali hiyo hapa nchini.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Waziri wa kilimo Maliasili Mifugo na uvuvi Hamad Rashid amesema Zanzibar haina mchanga utakaokidhi mahitaji ya ujenzi kutokana na kiwango kikubwa cha rasilimali mchanga kuchimbwa kwa kasi unguja na pemba.

Hata hivyo amesema ili kupunguza tatizo hilo lazima serikali kutumia matumizi mbadala wa mchanga katika harakati za ujenzi au mbinu za kutumia mchanga kidogo na kubuni rasilimali nyengine badala ya mchanga ili kupunguza tatizo ambalo linaathiri hapa nchini.

Aidha amesema hali imekuwa mbaya kutokana na matumizi mabaya ya ardhi inayosababisha athari kuongezeka hivyo serikali inatumia hatua za dharura kudhibiti uchimbwaji wa mchanga lazima utaratibu wa utoaji vibali ubadilike kutokana na upungufu uliopo ili kudhibiti rasilimali chache ilobaki.

Ametoa wito kwa wananchi kuwacha kuchimba mchanga kiholela na wanaochimba katika maeneo ya kuvunia kuwachana na serikali itatenga maeneo mbadala yatakayo tumika kwa shughuli hizo na kwa utaratibu maalum.

Utafiti uliofanywa hivi karibuni kwa Unguja na Pemba imeonesha kuwa Unguja inachimba hekta 3 kila mwezi na Pemba nusu hekta kila mwezi ambapo kwa mwaka 2016 uchimbaji huo umefikia tani Million moja laki nane na arobaini na sita elfu.

Credit: Amina Omar mwanahabari wa Zanzibar
Zanzibar ni nchi? Kwanini wasichukue mchanga bagamoyo? Nje ya nchi ndiyo wapi?
 
Yaani huko mchanga ni haba na wanauziwa lori 100,000 sie huku mchanga wa kumwaga lakini lori linauzwa 200,000. Wataalam wa uchumi hii imekaaje?
 
Ndio maana bakharesa anachukua mchanga wa baharini na kupeleka fumba, wakati maeneo hayo ya mtoni marien hadi mtoni branch likiathirika kwa maji ya bahari kuwa na kasi kubwa kutoka na project ya Hotel ya mtoni marien.

Wananchi wanajaribu kuchukua hatua za kisheria, kupeleka barua wizara inayo husika ya mazingira, hapo awali wananchi wa eneo hilo walikuwa wakivutana kutoka na tofauti za kisiasa.
 
Wawaige wa South Africa, wao huwa wana meli inafata mchanga port Elizabeth kuleta Durban. Hivyo na Wa Zanzibar watafute meli iwe inafata mchanga tanga au dar
 
Hamad Rashid ametangazia dunia kwamba Nchi ya Zanzibar imeishiwa mchanga kwaajili ya Ujenzi, hivyo wameruhusu kuagiza mchanga toka nje bila kodi.

Serikali ya Zanzibar imeomba wadau wajitokeze kuagiza mchanga nje ya nchi ili ujenzi uweze kuendelea.

Kwa sasa lori la mchanga linauzwa kwa laki moja na na bado haupatikani kwani kila sehemu walipokuwa wanachimba umeisha.

========

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imekusudia kuagiza mchanga nje ya nchi kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa kwa rasilimali hiyo hapa nchini.
View attachment 465030
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Waziri wa kilimo Maliasili Mifugo na uvuvi Hamad Rashid amesema Zanzibar haina mchanga utakaokidhi mahitaji ya ujenzi kutokana na kiwango kikubwa cha rasilimali mchanga kuchimbwa kwa kasi unguja na pemba.

Hata hivyo amesema ili kupunguza tatizo hilo lazima serikali kutumia matumizi mbadala wa mchanga katika harakati za ujenzi au mbinu za kutumia mchanga kidogo na kubuni rasilimali nyengine badala ya mchanga ili kupunguza tatizo ambalo linaathiri hapa nchini.

Aidha amesema hali imekuwa mbaya kutokana na matumizi mabaya ya ardhi inayosababisha athari kuongezeka hivyo serikali inatumia hatua za dharura kudhibiti uchimbwaji wa mchanga lazima utaratibu wa utoaji vibali ubadilike kutokana na upungufu uliopo ili kudhibiti rasilimali chache ilobaki.

Ametoa wito kwa wananchi kuwacha kuchimba mchanga kiholela na wanaochimba katika maeneo ya kuvunia kuwachana na serikali itatenga maeneo mbadala yatakayo tumika kwa shughuli hizo na kwa utaratibu maalum.

Utafiti uliofanywa hivi karibuni kwa Unguja na Pemba imeonesha kuwa Unguja inachimba hekta 3 kila mwezi na Pemba nusu hekta kila mwezi ambapo kwa mwaka 2016 uchimbaji huo umefikia tani Million moja laki nane na arobaini na sita elfu.

Credit: Amina Omar mwanahabari wa Zanzibar
Kwan sirikiali ya Zanzibar si ndio serikali ya tz si wasaidiane tu
 
Hii Kali! Pale ufukweni kweli mchanga umeisha wote!!! Wachimbe waongeze kina cha bahari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom